Nabii Geor Davie asababisha ndoa kuvunjika

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Mahakama ya hakimu mkazi jijini Arusha leo imevunja rasmi ndoa ya bibi Pamela na mumewe baada ya kuthibitika pasi na shaka kuwa alikuwa na mahusiano nje ya ndoa na nabii Jodevi wa ngurumo za upako wa jijini Arusha.

Mtoto wa wanandoa hao mwenye umri wa miaka 15 ndiye aliyetoa ushadihi wote ukiwemo wa nabii kufika nyumbani na kupelekewa juice kwenye gari yake yenye vioo vyeusi na kukaa humo kwa muda mrefu na mamaake pia nabii kufika nyumbani usiku baba akiwa hayupo na kuambiwa akalale huku nabii akibaki na mama sebuleni muda mrefu akifanyiwa maombi maalum

Vile vile ushahidi na msg za simu na kwenye laptop na mambo mengine mengi yamethibitisha pasi na shaka mahusiano ya wawili hao na hatimaye mahakama kuamua kuvunja ndoa hiyo takatifu

Chanzo: Wapo radio
=======================

CHANZO: Habari Leo
 
Mkuu mshana jr,

Hao watu wanatupeleka wapi sie kondoo tulopotea....!?

Basi kama ndivyo twendelee kula nyasi kama lile Kanisa letu jipya ambalo twagombea kujiandikisha/kujiunga toka Africa ya Kusini....!?

Tafadhali nikumbushe na ile NDOA ya Emmanuel Mbasha dhidi ya tuhuma kwa yule Gwajima, wajua nalitoka kiduchu....

Naamini ni mangi mno unayo, nigeiye japo kwa uchache ili nami niamue ni yuepi Nabii /Mchungaji nimfuate.

Ahsanta na nipo kipembeni hapa.
 
Mimi nilishasema hapa kuwa yule ana nguvu za kishetani alinunua Nigeria. Miujiza yake ni ya kichawi. Ni nani anakumnuka ile pete yake alikuwa akikunyooshea inatoa miali kama ya mwanga wa tochi.

Akirusha mkono eti shoti ya umeme inakupata unadondoka.pepo. Manabii wa uongo watajitokeza siku za mwisho. Tuwe makini. Na mzee wa upako Lusekelo bila kuwasahau Gwajima na Mwingira ndiyo hao hao tu sema baada ta kuisema ile pete take haoa JF sioni akiivaa tena.
 
Baadhi ya viongozi wa dini kwasasa shetani yumo ndani yao....ukisikia habr zaoo mmmmh.
 
Hawa ni mafuska waliokubuhu. Kuanzaia yule nabii feki wa Nigeria TB joshua, Gwajima wa misukule, mwingira wa efatha, Joe devi, yule wa kimara wa miaka 50 kaacha mke na kuoa binti wa miaka 20 na wengi wapendao kujipa vyeo vya unabii ni mafuska wa kutupwa na wote hao niliowataja wamevunja ndoa za waumini wao kwa ufuska.

Kazi kwenu mnaowapa hizo sadaka wanzochezea.
 

Mwamini Mungu wako tu fuata njia ya haki na jiepushe na dhambi, imani safi ni kutazama wagonjwa kusaidia yatima na wajane na kujilinda na dunia usitende dhambi

Utaniuliza dhambi ninini?
Dhambi ni tendo lolote lile ambalo lina madhara kwako na kwa wengine, linaharibu moyo na kutibua fikara, linaleta matokeo hasi na mambo yote ya jinsi hiyo


MENGINE WAACHIE WALIMWENGU
 
 
Last edited by a moderator:
Umekosea anaitwa Mheshimiwa Mstahiki Baba Nabii wa Karne, Ngurumo ya Upako Nabii na Mtume Goerdavie
 

Mkuu,

Ujumbe wako mzito mno, na umeeeka wazi kinaga ubaga bila kutafuna maneno.... daah!

Hivi una muda gani hujaliingia Kanisa /Synagogue...!?

Na kama muda mrefu, je, sababu ni hiyo uloitaja hapo juu...!?


Kama jibu ni "NDIYO", je, watushauri nini ambao pia tupo kizani kama ambavyo udhaniavyo weye....!?
 
 
Last edited by a moderator:
ukitaka kuwa na amani achana na dini kama mimi dini karibia zote mtaji wake mkubwa ni ujinga wa watu after 1000 yrs makanisa mengi na misikiti yatakuwa magodown au migahawa.
 
ukitaka kuwa na amani achana na dini kama mimi dini zote mtaji wake mkubwa ni ujinga wa watu after 1000 yrs makanisa na misikiti yatakuwa magodown au migahawa.
shalet japo ni uhuru wako wako wa maoni lakini mmh umechukua overall judgement kitu ambacho kina mapungufu
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…