Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 57,951
- 32,619
Mimi na mume wangu tuna maisha mazuri sana hasa linapokuja suala la sex. Hata hivyo siku nikiwa nimemtamani sana mume wangu (horny day) tukiwa kwenye sex hasa ninapofika kileleni huwa najisikia kulia machozi, sijui kwa nini? Je, ni kawaida kwa mwanamke kulia machozi wakati au baada ya sex?
Nahisi mume wangu huwa hajisikii vizuri (comfortable) kwa kuwa anahisi labda huwa naumizwa.
Je, hii huwatokea na wengine?
Ni mimi Jane J.
Asante kwa swali zuri hata hivyo ni kweli kwamba kama wakati wa sex na hasa unapofika kileleni huwa unajikuta unatiririsha machozi ya uhakika ni hakika unaweza kuchanganykiwa, kukatishwa tamaa na wakati mwingine. Hata hivyo nikuhakikishie tu kwamba hii huwatokea wanawake wengi na ni kitu cha kawaida. Ukweli wanawake wengi hujikuta wanabubujikwa na machozi bila sababu ya msingi wakati, na hata baada ya sex, na kuwaacha wapenzi wao wasijue cha kufanya.
Kuna wakati sababu ya kutoa machozi hujulikana na kuna wakati ni siri kubwa.
Ukweli ni mwitikio wa kawaida kihisia (emotions) kwani wapo watu hujikuta wakibubujikwa na kicheko, au kujikuta ana kiu au njaa ya chakula na wengine hulala fofofo na kuwa kama wamezimia na wengine hupiga kelele na hata kuimba au kutoa matusi ya nguoni na hii ni mwitikio wa kawaida kihisia kwa kufika kileleni.
Unapofika kileleni mwili hufanya majumuisho ya kuachia raha ya jumla na hii husukuma mwitikio wa tukuko (emotions/feelings) na kwako huo mwitikio ni kububujika machozi.
Pia ifahamike kwamba sex kati ya wawili wanaopendana ni suala la kumilikiana na kuingizana ndani ya kila mmoja kwenye nafsi ya mwenzake na wakati mwingine mwitikio unaotokea huwa nje ya ufahamu (unconscious level) wa hao wawili namna walivyounganishwa na matokeo yake mwanamke ambaye kwake suala la hisia huunganishwa na sex hujikuta akibubujikwa na machozi bila yeye mwenyewe kufahamu sababu halisi.
Jambo la msingi ni kwamba kama unajisikia raha na huku kuna kilio na machozi ni suala la mwenzako kuelewa kwamba ni mwitikio wa kazi yake nzuri ya kukufikisha pale unahitaji na si vinginevyo.
Haina haja kuwa na hofu kwani ni jambo la kawaida