Nadaiwa bodi ya mikopo (HESLB)

Kassim Awadh

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2012
Posts
884
Reaction score
187
Nimemaliza chuo 2009, Bachelor. Nilipata 60%. Hadi sasa sijajitokeza kwenye malipo/makato. Nitegemee nini? Muda wa kuanza kulipa (grace period) tokea kumaliza chuo ni miaka ngapi?
 

Attachments

Mimi nilimaliza shahada mwaka 2010,mwaka uliofuata nikaajiriwa kwenye taasisi ya serikali,julai mwaka huu nimeanza kukatwa pesa kwenye mshahara ambayo ni 8% ya "basic salary" nikipigwa na penati 10% kwa sababu ya kuchelewa kuanza kulipa kwa mwaka mmoja.Grace period ni mwaka mmoja.

Deni ni sh 6.248,400/- + 10%
 
Grace period watatoa kulipa silipi, unampa pesa nani hapo mafisadi?
Kwani wewe pesa ulipewa na nani? Angalia hili suala la mkopo ni la kisheria labda utaweza kuwakwepa kwepa kama huna mpango wa kuajiriwa nchini na au huna mpango wa kwenda kusoma nje ya nchi.

Nina jamaa yangu alipata nafasi ya kusoma Ufaransa, alipokwenda kutafuta visa ubalozi wa Ufaransa akaambiwa apeleke document inayoonesha kuwa hadaiwi na loan board. Kwa hiyo elewa kuwa kila baada ya muda wanaexpand means za kuwabana loan beneficialies, na hivi vitambulisho vya uraia nazani hiyo na yenyewe itatumika kama njia ya kupata defaulters.
 

For this case nadhani vema kuwalipa hela yao ukabaki huru! mambo mengine ya kufisidi hela zetu watayajua wenyewe
 
Kwanza una takiwa ujue mkataba wako na bodi ulikuwa una semaje kuhusu mkopo wako na kurejesha.

Kutorejesha mkopo ni sawa na mtu aliye kopa na akakimbia na pesa, pengine watu uita utapeli.

Kwa hiyo ni makosa kisheria, utakapo anza kutafutwa utalipa na fidia kwa usumbufu.

Ni vyema ukarejesha ili na wenzio wapate.
 
Potelea mbali mie nadaiwa tokea 1996 sijalipa na hawatanipata! kodi walizokula zinawatosha nafikiri na wao pia wanaona aibu kufuatilia!
 
Potelea mbali mie nadaiwa tokea 1996 sijalipa na hawatanipata! kodi walizokula zinawatosha nafikiri na wao pia wanaona aibu kufuatilia!

mi ushauri wangu naona bora ufanye repayment ili na wadogo zako wa tanzania waweze kupata mkopo brother
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…