Nadhani hatuna shida kubwa kwa kiwango cha kutangazwa kuwa Tanzania ina maambukizi makubwa sana ya corona

binafsi nahisi issue ya COVID-19 kuna watu wanatak kugeuza opportunity kiuchumi
Opoturnity ni ile fursa unayoweza kuiona kwa muda sahihi, muda wa uchumi wa viwanda tumeziona zipi, kama wao kuna fursa wanaona ambazo hatujawezaona ni wakati wao nasi tusubiri wakati wetu.
 
Hoja yangu ni hii kweli corona ipo na rais amesema na amekiri...
Kwa taarifa yako hata ulaya na Amerika wanafunzi wengi hawana uwezo wa masomo ya sayansi, hivyo wanachukua wabobezi wa masomo hayo toka Asia.

Tafuta shaka nyingine sio hiI hekaya zako za kufikirika. Ni vyema unapokuja na angalizo usimamie ukweli, na sio kuchanga propaganda zinazobeba utashi wa mwenyekiti wa CCM.
 
Naikataa hoja yako,kwanini tulikataa tatizo hili halipo, hatutakihata kuwaelimisha watu wachukue tahadhari, Tumekataa kutoa takwimu muda mrefu, kinyume na mikataba ya kimataifa tuliyoingia. Lete hoja kinzani tusonge mbele.
Mikataba ya kimataifa kwa sehemu kubwa ni kuweka afrika mahali tulipo na tusisonge mbele, moja ya mkataba hatari ni ule wa kibiashara kwa mfano ukiingizwa mkenge na makampuni haya ya kimataifa huchomoki na hata ukitaka haki itendeke ofa anapewa kampuni iliyokuja kuwekeza mfano richond imetukausha mpaka tumekoma.

Mimi binafsi hizo mikataba sijawahi iamini kwa sababu tunapata taarifa nyingi kutoka source mbali mbali kuwa Afrika lazima ibaki pale pale ilipo isifanye jambo tofauti
 
hivi hili la sisi kutangazwa dunia nzima kuwa tz ni nchi hatari ni kweli kwa maoni yako mkuu?

Sisi ni nchi hatari maana ugonjwa kwetu haufahamiki uko kwa kiwango gani.
 
Mpaka Malema anahubiri chanjo ukiwa corrupt ni hatari sikutegemea Malema kunaswa kwenye mtego huu
 

Hiyo mikataba ya kimataifa ina vipengele maalum kwa Afrika tu? Acha upotoshaji usio na tija. Mikataba yote viongozi wetu wameifanya siri, ni kwanini isiwe wazi kisha utuonyeshe mkataba fulani una kifungu fulani hatari kwa Afrika?
 
Opoturnity ni ilefursa unayowezakuiona kwa muda sahihi,muda wa uchumi wa viwanda tumeziona zipi,kama wao kunafursa wanaona ambazo hatujawezaona ni wakati wao nasi tusubiri wakati wetu.
Unaweza vuruga kwa kukataa kama Magu kwa maana inaoneka kuna fursa nyuma yake
 
Hiyo mikataba ya kimataifa ina vipengele maalum kwa Afrika tu? Acha upotoshaji usio na tija. Mikataba yote viongozi wetu wameifanya siri, ni kwanini isiwe wazi kisha utuonyeshe mkataba fulani una kifungu fulani hatari kwa Afrika?
Usiri ni sehemu ya mkataba kwa taarifa yako, Patrice Lumumba alitaka ujadiliwe bungeni mkataba wowote utakaoingiwa na nchi akaishia kuuawa, upo mpaka hapo
 
usiri ni sehemu ya mkataba kwa taarifa yako patrice lumumba alitaka ujadiliwe bungeni mkataba wowote utakaoingiwa na nchi akaishia kuuawa upo mpaka hapo
Sio kwa bunge.
 
Niko huru sana mkuu, naongea utashi wangu ukichunguza maandishi yangu, mimi habari ya CCM niko mbali sana nao siwakubali lakini hili la corona msimamo wa Magu nimeukubali
 
Sio kwa bunge.
Niambie bunge la nchi ipi mikataba wanajadili bungeni na kama mkataba ni kwa nchi kwanini usijadiliwe bungeni, shida iko wapi?
 
HEBU TOA MAONI YAKO NJIA GANI ITUMIKE KUITOKOMEZA CORONA KABISA.?
 
niambie bunge la nchi ipi mikataba wanajadili bungeni na kama mkataba ni kwa nchi kwanini usijadiliwe bungeni shida iko wap?

Mkuu unasimamia kipi, unaonyesha Tanzania ni tofauti, kisha unataka nikupe mfano wa nchi nyingine. Ili tuonyeshe kuwa sisi Tanzania tuna msimamo kama huu wa rais wetu unaousema, mwambie apeleke hiyo mikataba bungeni tuone hiyo misimamo yake dhidi ya hao wazungu.
 

Uchunguzi wa kibaiolojia umethibitisha kuwa hofu hupunguza kinga za mwili na hufanya mwili kuwa dhaifu.
 
Sisi ni nchi hatari maana ugonjwa kwetu haufahamiki uko kwa kiwango gani.
Hatari au Ugonjwa usipofahamika hata Kwa wenye nchi, kinachofuata ni upumbuvu wa wanaotutangaza kuwa ni nchi hatarishi!

Mashaka bila uhalisia halijawahi kuwa ndio jibu la kile unakitafuta
 

Kuhusu hili janga Sisi kama taifa tunasimama na kumtanguliza Mungu kwanza alafu tunatumia na dawa zetu za asili. Alafu pia hata marekani anamtegemea mchina kwa ngano na maharage kwani hakuna taifa lolote duniani linalojikidhi mahitaji yake yote tupo tunahitaji kutegemeana mbona wao hawana tanzanite tunayo sisi?
 
Hatari au Ugonjwa usipofahamika hata Kwa wenye nchi, kinachofuata ni upumbuvu wa wanaotutangaza kuwa ni nchi hatarishi!

Mashaka bila uhalisia halijawahi kuwa ndio jibu la kile unakitafuta

Kwani haufahamiki au kila mtu anaogopa kusema? Hata huyo Maalim Seif kama sio chama chake na yeye kuweka wazi, isingefahamika maana serikali wameficha. Sasa kama watu wanaficha hata hayo yasiyopaswa kufichwa, wengine kwanini wasituweke kwenye nchi hatarishi?
 
Kwa hili la chanjo mimi naunga mkono hoja za serikali haiingii akilini chanjo ipatikane ndani ya miezi tisa tuu na hatujui longtime effect zake mwilini ni zipi bora ingefanyiwa majaribio hata miaka mitano tujue kama ni salama au vp lakini miezi tisa hapana aisee huu ni upigaji wanataka kutuharibu afya zetu pmoja kutupa mzigo wa madeni kwa kupitia chanjo hii. Hii ni biashara kichaa wazungu ni wapigaji aisee
 

Tanzanite mmeitengeneza kwenye kiwanda gani? Unajua kwa uhakika reserve ya Tanzanite iliyopo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…