Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hayo ndiyo madhara ya kupanua kikosi maana yeyote anaweza kuingiza , Naona wakiingiziwa magoli mengi sana ikianza ligi ya mabingwa kwa sababu timu yao imepanuliwa kikosi.Kikosi kipana jana kimepanuliwa na wajelajela.
Yaan hizi timu zetu za simba na yanga ni shida. Zikifungwa tu ai kutoa sare wanaanza kutafuta mchawi.Kwahiyo ninyi hamtaki kufungwa?
Yaani mkifungwa tu nongwa acha utoto basi.
Wewe na huyo jamaa yako ni wakuda sana. 😁😁😁😂😂😂 sina mbavu kwa huo mwonekano na pozi la huyo Simba.Kuna jamaa angu kanitumia hii.View attachment 1609439
Hoja ni aina ya mpira unaochezwa. Pasi na udwambwi usambwi mwingi bila malengo na mikakati thabiti ya kupata magoli. Kucheza mpira unaovutia na kisha kufungwa ni ujinga kama ujinga mwingine. Lengo liwe kushinda.Maneno ya kishabiki tu hayo ni ya kawaida kwenye michezo, hata timu nyingine zinaweza kutafuta naneno yao ya kuwahamasisha,sijaona shida yoyote ile,kupoteza game moja sio sababu ya kutoendelea kufanya vizuri tena
Umemjibu vizuri huyo mjinga yani wabongo wanajifanya kuujua mpira lakini wakipewa timu wanazingua. Juzi nlimsikia Julio et anaishauri Simba yeye kapewa sijui timu gan kaishia kupuyanga.Hujui mpira wewe...Kufungwa kupo tu...hata ucheze mpira wa vurugu kama walivyofanya Prison. Jiulize Prison hushinda mechi ngapi kwa msimu na mpira wao unaoshauri Simba icheze?
Eti "wamefungwa kisa mpira biliani" yaani hujui hata kwanini Simba inaitwa Lunyasi unataka kujifanya shabiki? Kila timu inafalsafa yake na husajili kocha na wachezaji kutokana na falsafa yake.
Mpira ndo ulivyo kama hutaki kufungwa kacheze Video game ili ucheze kwa mfumo wako usitupangie.
Muulize hiyo ni sanamu ya jini gani?Kuna jamaa angu kanitumia hii.View attachment 1609439
Tatizo sio mpira carpet. Tatizo ni marefa wanao acha rafu mbaya ziendelee Kwa muda mrefu na matokeo yake kupelekea ngumi uwanjani.Mpira ni magoli.
Hii dhana ya kucheza entertaining football naona ni ya kijinga sana.Maana inategemea vitu vingi sana ili ifanikiwe. Mfano mechi ya jana na Prisons. Prisons wamecheza Mpira wa nguvu na vurugu sana.Uwanja wenyewe hauruhusu hizo pasi za rula.Kasi ya wachezaji wa Simba siyo kubwa.Upangaji wa timu na game plan mbovu.Huwezi kupata matokeo kwa jinsi hiyo.
Simba wawekeze kwenye kupata ushindi na waachane na maneno ya Haji. Kuna baadhi ya watangazaji wanasifia eti "soft touch" huu ni upuuzi mkubwa. Mpira wenyewe ni wa kiume hivyo uwekezaji wa nguvu lazima uende sambamba na akili na kipaji.
Kutokana na hii dhana na falsafa ya pira biriani imesababisha wachezaji kama Miqueuson na Morrison waache aina ya mchezo wao uliokuwa unaleta hatari sana kwa timu pinzani.Haya mambo ya chenga twawala ni ya kizamani sana