You are not serious, unasema takrima ni mambo ya kawaida wakati inapingwa vikali, ukiambiwa utaviharibu vibinti unasema hayo ni ya kawaida tu kwa wa-Afrika, ninavyokuona mimi kupitia majibu yako nakushauri bora utafute kazi nyingine ya kufanya kuliko kupoteza muda kugombea ubunge.
.Kutokana na ratiba yangu kuwa ngumu katika kipindi hiki, ni wazi sitaweza kuwa na muda mwingi ndani ya JF halikadhalka nikiwa jimbon siaweza kupata connection ya uhakika ya internet na hivyo nitawamiss sana wapendwa.
Atawekaje jina wakati kuna kashfa nzito namna hii juu yake, hapaswi kabisa kutoa jina lake,itakuwa ni kujimaliza kabla ya kuanza.sijaona hoja yake kwani kama anaenda kugombea angeweka jina wazi ili kama ni watu waanze ama kumsaidia au kumpa mbinu, sasa jina hana analeta hoja gani hapa?
ndugu,
samahani nilitoka kidogo.
nawashukuru sana wote waliochangia thread yangu na kwa hakika nimenufaika sana na mawazo yenu wote. Shukrani za pekee kwa wote walioniunga mkono na kunitia moyo. Safari ni ndefu na ita ni vigumu, lakini nafarijika ninapoona kuwa ushindi ni dhahiri upande wangu.
Nikiri kwamba changamoto ya kuwaania ubunge ndani ya ccm ni kubwa sana, yako mambo ya ufisadi, wizi wa kura, kuhadaa wapiga kura, nk. Hayo yamo ndani ya chama chochote cha siasa japo ukubwa wa tatizo ni tofauti toka chama kimoja hadi ingine.
Kuhusu ccm skubaliani kuwa wote ccm ni mafisadi na naweka wazi uwa mimi si fisadi wala sitafuti ubunge niwe fisadi. Nikifanikisha azma yangu, mtakubaliana nami kuwa kwa mara ya kwanza vita ya kweli dhidi ya ufisadi itapganwa na mbunge wa ccm bila shaka nitakuwa mimi, tuombe Mungu, tutafika
Matajiri wa kutisha ndani ya ccm wapo, sikatai lain si wengi kama inavyoaminka. Kuna watu kanitajia majina ya panda, wasira na mkono. Wote nawafahamu na nawaheshimu sana, lakini siogopi kupambana nao kisiasa. Mtaji wangu mkubwa ni nguvu ya wananchi na naamini naweza kushinda hata nikipambanishwa na nani na mwenye shilingi ngapi.
heshima ya pekee kwa mku next level kwa uchambuzi wake makini. Ni kweli kuwa kwa mujibu wa uchambuzi wake na viambatanisho alivyowasilisha, sifai hata kidogo kwa wadhifa ninaoutafuta kwani matendo yale ni kinyume cha maadili. Naomba niwarudishe nyuma kidogo.
Toka siku ya kwanza najisajli JF nilisema kuwa kama jna langu lilivyo ndivo ilivyo dhamira yangu. Nivyo ndio maana sijitambulishi kuwa nagombea ubunge, bali natoa taarifa kuwa katika siku za karibuni sitaonekana mara nyingi hapa JF na wapendwa msijiulize kulikoni.
Siku za mwanzo hapa JF nilikuwa naleta visa vingi sana vya matatizo ya ndoa na namna nilivyojaribu kuvisuluhisha. Katika visa vile sikuwahi kuweka hadharani majina ya wahusika kwa malengo maalum ambayo kila mtu mstaarabu atakubaliana nami kuhifadhi majina yao. Lengo halikuwa kudanganya, bali kulinda heshima na madili.
Hivyo kuna wakati mtu anasema ama anakaa kimya au anatumia majina bandia kwa lengo la kulinda kitu ama kuelewesha vizuri kitu Fulani. Na ndivyo nilivyofanya mimi. Na ndivyo wafanyavyo na wanJF wengine. Hivyo post aliyotumia next level inaonekana kama ni mimi haswa, bali ukweli ni kwama nilihifadhi jina halisi la mhusika na nikaisimilia kama ni mimi wenyewe kwa lengo la kufikisha ujumbe uliokusudiwa na ambao naamini ulfika. Kukereka walikokereka wachangiaji hapa JF ni kiashiria kingine kuwa ujumbe uliokusudiwa ulifika kikamilifu. Labda kosa la kukiri hapa ni kuwa sikusema tangu mwanzo kuwa si mimi bali nimetumia mtindo wa uandishi kama vile mimi ndiye. Hapo naweza kusema smahani kwa kuwapotosha wale niliowaptosha. Kweli hata mimi napinga sana matendo ya kifataki katika jamii yetu.
Tuendelee kukabiliana na matendo ya aina hii bila kuchoka na naamini ushindi ni wetu.
mkuu ndege ya uchumi heshima mbele.
nakubaliana na hilo la kimtokacho mtu......
lakini mie sijanajisika, mashambulizi haya yanatokana na mitazamo ya watu tu. unajua wanawatisha vijana wasijaribu kutangaza hadharani makusudio ya kuwania uongozi,
hivi kama tungefunga scaner hapa JF ikam-scan kila mtu moyo wake, linywa chake na miguu yake, nani angesimama? mi nakubali wanitundike msalabani lakini nitaejea tena apa JF siku moja kuwashukuru wote , hakika siku moja nitakuwa mshindi!
tuombe uzima
.
Kama ni ratiba its ok.Kwa vile uko nchi za watu, labda hujajua Tanzania mitandao imeenea nchi nzima with 3G with HSDPA USB Moderm. Nunua laptop ya Sony Vaio TX - up to seven hours. 11.1" widescreen na extra battery, Au nunua Lenovo ThinkPad X60s battery life masaa 8 au funga kazi na Laptop mpya ya IBM Masaa 12!, we won't miss you.
Karibu Uwanjani.
So unataka tuamini kuwa hata hii ya kugombea ubunge si kauli yako, ila umevaa uhusika wa mtu fulani aliyepo ughaibuni !!... Hivyo post aliyotumia next level inaonekana kama ni mimi haswa, bali ukweli ni kwama nilihifadhi jina halisi la mhusika na nikaisimilia kama ni mimi wenyewe kwa lengo la kufikisha ujumbe uliokusudiwa na ambao naamini ulfika.
... Labda kosa la kukiri hapa ni kuwa sikusema tangu mwanzo kuwa si mimi bali nimetumia mtindo wa uandishi kama vile mimi ndiye.
So unataka tuamini kuwa hata hii ya kugombea ubunge si kauli yako, ila umevaa uhusika wa mtu fulani aliyepo ughaibuni !!
hahahahahahaaaaaaaaa, umenivunja mbavu mkuu!
sisi ni waafrika na mambo kama haya yapo enzi na enzi.
nashukuru pasco kwa ushauri wako mzuri, nitajitahidi kuzingatia.
labda kwa wale wasiojua vizuri mambo ya siasa, kazi ya kugombea si rahisi hata idogo, inahitaji mikakati na mbinu za hali ya juu na za muda mrefu. muhimu ni "kutaka" unachogombea kwa dhati na uonyeshe kuwa unataka. wababishaji hawatakiwi kwani watashindwa vibaya sana kabla hata hawajaanza. kumbuka pia kuwa wako wengi wanaotaka na baadhi wana nguvu kubwa zaidi.
kwa wale wanaotaka niweke wazi jina na jimbo ninalokwenda, nafikiri kwa sasa si muafaka kwani huwezi kumjua mshindani wako ana mbinu gani. huenda hata wakawa hawa wenzetu walioamua kupindisha ukweli hapa jamvini kwa lengo la kunikatisha tamaa.
lizy namshauri asome vizuri kila hoja na sio kila neno. nasikitika kuwa watu wanasoma zaidi maneno kuliko hoja. ni hatari sana.
mwisho kabisa narudia tena kuwa nitawamiss sana wanaJF wote na hatimaye nitarejea tena hapa jamvini kwashukuru wote nikiwa mshindi.
Mungu ibariki tanzania,
asanteni sana kwa kunisoma na kunichangia
Kumbe mambo haya yanachekesha eeeeh?
You must have totally lost your mind brother!
......he!he!he! JF hiyo! alinikera sana na kale katabia kake kaubakaji, halafu kaja kujisifia hapa.......then katukana wapwa kuleeeeee......hala anataka kwenda mjengoni?...arrrrg!Kiongozi nimekukubali. Huyu jamaa umemng'ang'ania kama ruba.
Jioni nitafute pale kwa ankal. Kuna bia kadhaa za baridi unanidai pale.
Louder pleaaaaaaaaaseeee!
Kumbe mambo haya yanachekesha eeeeh?
You must have totally lost your mind brother!
Vipi Mkuu semester ya pili ya mwaka wa pili imeshaanza?Kutokana na ratiba yangu kuwa ngumu katika kipindi hiki, ni wazi sitaweza kuwa na muda mwingi ndani ya JF
Kumbe mambo haya yanachekesha eeeeh?
You must have totally lost your mind brother!
hahahahahamzee wa docebit... Yaani kama nakuona ulivyomaind huyu dude!!! Inawezekana kabisa anaandika ka-study au assignment ya sociaology huko alipo na hapa ndio venyu ya kupata respondents badala ya questionnaires
Kumbe mambo haya yanachekesha eeeeh?
You must have totally lost your mind brother!