sangujoseph
Senior Member
- Nov 30, 2015
- 164
- 183
By Sangu Joseph
Leo nimekikumbuka kisa kilichonichekesha baada ya kukutana na wimbo wa Aslay Rudi Darasani hasa kile kipande ambacho video vixen anatamba kwamba alienda kuwaona wageni, Akiwa amevaa short pensi, na Tabu Mtingita ambaye ndiye kungwi aliyetoa boko anamwambia unajikuta Beyonce.
Kilichonifanya nikumbuke mimi nilibahatika kusoma na Star Aslay Isihaka pale Tandika Sekondari japo nilimpita darasa moja.
Wakati ngoma yake ya Naenda Kusema kwa Mama (2011) inatamba, interview kila media kiufupi kama zote, siku moja alienda kwenye kituo cha redio cha Clouds FM. Sasa wakati anaulizwa maswali na Dahuu alisema kwamba siku hizi shule hachapwi wala viongozi wa shule hawampi fagio akafagie.
Basi Jumatatu yake baada ya kufika shule akakutana na kiongozi (Kiranja kauzu) mmoja alikua anaitwa Theodory Mwingira; alisikia yale mahojiano, basi jamaa hiyo siku alichelewa kufika yule mshikaji akampa adhabu ya kufagia, kufyeka na kuzoa taka kwenye eneo lenye nyasi nyingi.
Kutokana na u-star aliokuwa nao kiukweli ilikuwa ngumu sana kulifanya hata kama ningekua mimi. Aslay akawa anaingilia huku anatokea huku, kiufupi alikuwa analinda brand, basi yule kiranja kauzu akaenda kusema kwa ticha kauzu alikua anaitwa Likalambile, anafundisha Mathematics hatari na kama mnavyojua Walimu wa Mathe wanakuaga wakali sana. Basi Aslay aliitwa na ticha alipigwa bakora mpaka alitoroka shule kwa bakora za yule mwalimu.
Ikawa bonge moja la stori shule nzima Aslay kachezea kichapo tena yule Mwalimu alimpiga akimwambia 'Nenda kaseme kwa Mama'
Ila ambacho nilijifunza, shule zetu hazina utaalamu wa kulea watoto wenye vipaji ila wanauwezo wa kulea watoto wenye akili za darasani. Nadhani kuna haja shule zetu kuwa-treat sawa watoto wenye vipaji na wenye akili za darasani.
#KijanaMzalendo #IloveTZ Nicheki Instagram na Twitter na Facebook sangujoseph Kwa makala na uchambuzi ninaoufanya
Sent using Jamii Forums mobile app
Leo nimekikumbuka kisa kilichonichekesha baada ya kukutana na wimbo wa Aslay Rudi Darasani hasa kile kipande ambacho video vixen anatamba kwamba alienda kuwaona wageni, Akiwa amevaa short pensi, na Tabu Mtingita ambaye ndiye kungwi aliyetoa boko anamwambia unajikuta Beyonce.
Kilichonifanya nikumbuke mimi nilibahatika kusoma na Star Aslay Isihaka pale Tandika Sekondari japo nilimpita darasa moja.
Wakati ngoma yake ya Naenda Kusema kwa Mama (2011) inatamba, interview kila media kiufupi kama zote, siku moja alienda kwenye kituo cha redio cha Clouds FM. Sasa wakati anaulizwa maswali na Dahuu alisema kwamba siku hizi shule hachapwi wala viongozi wa shule hawampi fagio akafagie.
Basi Jumatatu yake baada ya kufika shule akakutana na kiongozi (Kiranja kauzu) mmoja alikua anaitwa Theodory Mwingira; alisikia yale mahojiano, basi jamaa hiyo siku alichelewa kufika yule mshikaji akampa adhabu ya kufagia, kufyeka na kuzoa taka kwenye eneo lenye nyasi nyingi.
Kutokana na u-star aliokuwa nao kiukweli ilikuwa ngumu sana kulifanya hata kama ningekua mimi. Aslay akawa anaingilia huku anatokea huku, kiufupi alikuwa analinda brand, basi yule kiranja kauzu akaenda kusema kwa ticha kauzu alikua anaitwa Likalambile, anafundisha Mathematics hatari na kama mnavyojua Walimu wa Mathe wanakuaga wakali sana. Basi Aslay aliitwa na ticha alipigwa bakora mpaka alitoroka shule kwa bakora za yule mwalimu.
Ikawa bonge moja la stori shule nzima Aslay kachezea kichapo tena yule Mwalimu alimpiga akimwambia 'Nenda kaseme kwa Mama'
Ila ambacho nilijifunza, shule zetu hazina utaalamu wa kulea watoto wenye vipaji ila wanauwezo wa kulea watoto wenye akili za darasani. Nadhani kuna haja shule zetu kuwa-treat sawa watoto wenye vipaji na wenye akili za darasani.
#KijanaMzalendo #IloveTZ Nicheki Instagram na Twitter na Facebook sangujoseph Kwa makala na uchambuzi ninaoufanya
Sent using Jamii Forums mobile app