Nafasi ya mume. . .


sasa aamke saa mbili ili iweje?
mtu ni housewife.....
mbona mna gubu hivyo?
saloon si ndo vizuri apendeze?
akiwa mchafu mtasemaje?
 
Partly yes,

lakini pia na malezi yanachangia
kama umekulia kwenye mmazingira ya kuchunguza jirani kala nini, kavaa nguo ya sh. Ngapi, unakua ukidhani huo ndio mtindo wa maisha.

Ndugu yako awe wa kike au kiume akioa au kuolewa hicho kitabia lazima utakipeleka na kwenye nyumba ya ndugu yako.

kuna mdada mmoja kaana hela, tena hela nzuri mno.
Lakini ni mshari wa ajabu.
Hao wifi zake na shemeji zake wanaipata.

Anagombana hata akiona wifi/mdogo wake kanunuliwa poda ya Mac na mumewe

eti ansema, nao wanajidai kupanda bei, wanapaka Mac wakati walikuwa wamezoea vestline.

Huyo naongelea mtu mwenye firm kubwa hapo Dar.
 

Sasa kakondoo hapo si kwake jamani?
Kama amka yake saa tano haimsumbui mume wake (si ajabu anasupport) kwanini we umkandie?
 
Si ndio umaskini wenyewe? Itakuaje nyinyi mnakula kama inavo takiwa (balanced meal, regular meal) alafu uanze kutaka kujua jirani kala nini? yaani umelelewa katika mazingira ya umasikini, alafu na wewe mwenyewe unaendelea kua na akili za kimasikini! Unamtegemea baba for the first 25 years, alafu unamtegemea kaka (coz baba kazeeka) alafu unamtegemea mume+kaka, alafu unamtegemea buzi, unamtegemea boss etc.No dignity at all.
Kuna familia hazina pato ila zina dignity, hawana mentality ya umasikini. wanatosheka na kile walicho nacho, na wanawafunza watoto (wa kike na wakiume) kujitegemea independently.
 

hahahaha! Baada ya kusikia hayo dada yako nasema tusijuane wakati wa shida wala raha. Nyumbani kwako siji na kwangu pia marufuku. Shida zangu nitakufa nazo na zako kufa nazo.
 
hahahaha! Baada ya kusikia hayo dada yako nasema tusijuane wakati wa shida wala raha. Nyumbani kwako siji na kwangu pia marufuku. Shida zangu nitakufa nazo na zako kufa nazo.

ukitaka hayo uanze na kurudisha misaada yote niliyokupa

mimi kama kaka yako nitakusaidia ukiwa na shida but stay mbali na mke wangu....
ma gubu na ushari kwa mke wangu sitaki.....
 
Kama ni madogo wanafanya kazi kuna shida gani?
Si wanaishi hapo?
Kama kuna watu wadogo, ya nini wakubwa wajilazimishe kufanya kazi?

Ni kweli wifi afanye anapojisikia
as long as kaka yuko Happy na wifi yuko Happy

 
Mamie, ugali wa shkamoo una masharti yake! Sasa nyie mpo hapo na hakuna housigeli wifi yenu apike na kufua wa nini? Kama mumewe hana shida haiwahusu! Kama mnajua ufundi wa ndoa si mkaolewe mtie ufundi kwenye majumba yenu? Mimi namheshimu wifi yangu, mashallah nae ananiheshimu! Na mjikomboe mtoke kwa kaka yenu tuje tuone mlivyo wajuzi! Hela ya saluni hajakuomba wewe, unakereka ili iweje? Kama nyumba chafu ni yake,sio yako! Mi mtu akigombana na wifi yake huwa namshangaa sana kwa kweli!
 
We hujui ukweli wa ndani, ukute ni hivi:
 
hahahaha! Baada ya kusikia hayo dada yako nasema tusijuane wakati wa shida wala raha. Nyumbani kwako siji na kwangu pia marufuku. Shida zangu nitakufa nazo na zako kufa nazo.


Mhhhh! Husninyo!!! Vibaya hivyo!!!! Mambo ya kuapizana ndiyo nini sasa!? :rant::rant::rant:
 
Kuna watu wengi sana humu wametokea katika extended families. Kama sio wazazi wao walilea watoto wa ndugu basi wao walilelewa kwa ndugu. Nashangaa mnavyosema hamtotaka ndugu kisa mkeo hataki. Lol. Kwahiyo kama mkeo alikukuta una majukumu ya kusomesha watoto wa dada au kaka yako ambao wameshafariki, utawatelekeza watoto kisa mkeo hataki? Huo ni upuuzi.
 
Hawajui labda wifi yao hajalala usiku kucha! Na mumewe hiyo saa tano ndo kampigia kumuambia amka mpenzi, ukasuke yeboyebo uagize na supu pake next ya saluni. Jioni nikija tutoke zetu! Wao wanachonga tu!
Halafu tunajisahau kweli! Mi wifi yangu aliniletea kesi ya kaka (kaka kanizidi 10 yrs), nikamuambia hii hata kwa baba haifiki. Mtiti wake kaka hakuamini, kabakia ooh wadogo zangu hamni-support! Nikamuambia siwezi ku-support dhulma. Kesho na mie nikiwa na kesi ya hivi ntakuja kwa sura ipi hapa?
Sasa kakondoo hapo si kwake jamani?
Kama amka yake saa tano haimsumbui mume wake (si ajabu anasupport) kwanini we umkandie?
 
mpaka dada waje kuleta maneno kuna jambo moja hapo

shule ndogo na kukosa kazi ya kufanya.......

ukitaka kumlinda mkeo,somesha dada zako
hakikisha wanapata kazi za maana.......

na somesha mkeo pia ikibidi........

L.o.l , duh mbona sasa jamaa atakuwa na kibarua kikubwa hapo cha kupeleka watu shule!!
 

...Mara nyingi ugomvi unasababishwa na mambo ya kufuatana fuatana huyu mbona anafaidi sana kwa kaka yetu, mbona ananunuliwa sana nguo, viatu, kanga, vipodozi vya bei mbaya, mbona wao wanakula vizuri sana kuliko sisi mbona huyu wifi hafanyi hiki au kile kwa kaka yetu mvivu sana huyu wifi yetu maana kila siku kaka anakula chakula kinachopikwa na HG. Matokeo ya haya ndiyo mwanzo wa varangati na kutoelewana kwa mawifi. Wangenyamaza kimya na kutotaka kujua undani wa kila kitu kinachoendelea kati ya kaka yao na mke wake labda matatizo mengi sana yangeepukwa.

 
Sio kuwa ndugu hawatakiwi! Issue ni kukaa kwa masharti ya wadhamini mkwe! Mbona ndugu wa mke wakija wasijitutumue kuwapa masharti shemeji zao? Tambua utawala uliopo,maisha lazma yabadilike kaka yenu akioa. Kama ambavyo dada yenu akiolewa maisha yake yanabadilika pia, hawezi kwenda kulala kwa shosti mwenye sendoff, get it?
 
Watoto ni watoto, kama ni lazima wakae hapo wanaweza wakaishi kwa masharti, heshima muhimu. Ila mtu mzima ni ngumu kuanza kumpangia kazi, muda wa kuamka, kumnyang'anya remort uangalie taarifa ya habari wakayi yeye anataka tamthilia, kumweka sawa anapoanza kulalamika kwanini kunapikwa maharage badala ya nyama wakati pesa ipo (japo sio yake) n.k. Na ndio maana ni muhimu kila mtu atafute kwake ili aweze kuishi vile apendavyo bila kukera ama kukerwa na wengine.
 
Mume atawezaje ku-exercise nafasi yake wakati tayari wote wawili mme na mke wana nafasi sawa kwenye ndoa?

Haki za wanawake.
Kama mke ana nafasi sawa na mme basi na atatue hilo pia.

My stand: haki za wanawake inachochea migogoro ya ndoa.

Beijing
 
BAK ndio maana hodi hodi zinatakiwa zihesabiwe. Unajua ukienda kwa mtu ukalala siku mbili anaweza hata akajitahidi kuamka mapema na kukupikia hata kama sio kawaida yake, ila hawezi kukufanyia hivyo mwezi mzima. Ratiba yake ni yake kwasababu yuko kwake na yeye ndie mwamuzi, mwenye haki ya kulalamika ni mke/mume wake pekee.

@King'asti. . .
Hapo sasa. Makubaliano yao hujui ila matokeo yanakuumiza.
 
Uko sawa BAK. Lakini uki-entertain maneno yanaendelea kuja. Kuna wake pia nao wana tabia ya kuwafuatilia wifi zao, kama kakako kakupa sh ngapi etc. Mi nadhani ni malezi na life style, usipoendekeza hayakupati. 'usilete ufundi kwa mwenzio, ngoja upate nafasi uwe na kwako tuje tukuone', period! Usi-comment any observation ya kwa ndugu,kaka wala rafiki!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…