ukitaka hayo uanze na kurudisha misaada yote niliyokupa
mimi kama kaka yako nitakusaidia ukiwa na shida but stay mbali na mke wangu....
ma gubu na ushari kwa mke wangu sitaki.....
Mhhhh! Husninyo!!! Vibaya hivyo!!!! Mambo ya kuapizana ndiyo nini sasa!? :rant::rant::rant:
umesahau kwamba tulikuwa tunasaidiana? Umesahau umeishi kwangu miaka yote kabla hujaanza kujitegemea? Umeoa hutaki ushirikiano. Hakuna noma.
sasa aamke saa mbili ili iweje?
mtu ni housewife.....
mbona mna gubu hivyo?
saloon si ndo vizuri apendeze?
akiwa mchafu mtasemaje?
wewe wasema ndugu, bora angekuwa kwake au kama kungekuwa na house girl kuliko kuamka saa 5 na malalamiko kibao! Mie wala sina gubu boss, just imagine namkuta mdogo wangu hajarudi shule kisa kaambiwa afue nguo za my wi, yeye kaenda saluni......WHAT IS THIS??? Why asiamke mapema akajifanyia kazi zake ndo akaenda saluni? Si hela yake na mumewe jamani na hakuna anayemdai!!
Hiyo ya kugeuza watoto vijakazi haijakaa sawa. Sema ndio hivyo kukaa kwa mtu kazi, inabidi ufanye tu.
Sio kuwa ndugu hawatakiwi! Issue ni kukaa kwa masharti ya wadhamini mkwe! Mbona ndugu wa mke wakija wasijitutumue kuwapa masharti shemeji zao? Tambua utawala uliopo,maisha lazma yabadilike kaka yenu akioa. Kama ambavyo dada yenu akiolewa maisha yake yanabadilika pia, hawezi kwenda kulala kwa shosti mwenye sendoff, get it?
Sasa kakondoo hapo si kwake jamani?
Kama amka yake saa tano haimsumbui mume wake (si ajabu anasupport) kwanini we umkandie?
Hivi ushirikiano hauwezi kuwepo bila kufuatana majumbani kila siku?
"....damu nzito kuliko,....!" uchungu wa mwana...
..acheni madada waendelee kuwatetea kaka zao bana,
wake wengine ni wanyanyasaji banaa...hahaha..
kumbe hapa swala ni kufatana nyumbani tu? Nilifikiri tunajadili mabadiliko yote yanayotokea baada ya ndoa.
sasa ndo unatakiwa ufurahi nimekuwa nimetoka na kukupunguzia mzigo
kusaidiana tusaidiane lakini tusidaiane fadhila na kulipana 'mzigo'
get it?
Ni muhimu kuwafundisha watoto kazi ila sio kuwageuza vijakazi bwana. Nimeona mwenyewe mtu alivyokua anawafanyia watoto wa ndugu zake mwenyewe. . . mpaka huruma. Unakuta mtu anakumbatiana na wakwake sebleni wakati wengine wanachakazwa huko nje, huko sio kuwafundisha ni kuwakomoa.Kama mtoto ataacha kwenda shule kwa sababu wifiye kampa kazi ya kufua nguo zake hapo kaka mtu inabidi aingilie kati na sio mtu mwingine! Lakini sioni tatizo kumpa mtoto nguo akufulie wknd, tena sio nyingi. Otherwise huyo wifi nae hana hgeli wake? Kumfundisha mtoto kazi ni muhimu, kama kupika pia aagizwe ili ajue! Sio kwa vile anasoma aishi kama gesti, kwani angekuwa kwa mama yake angeacha kusaidia kufua na usafi? Ukikaa na wifi yako vizuri hata akirudi njiani akiona viatu ama kiwalo anakuletea! Manake nae anakuwazia mema jamani!
Angekuwa kwake mie ningehusikaje dear na mambo ya nyumbani kwake na mumewe?? Kuamka kwake saa 5 wala sio tija kama angekuwa anajifanyia mambo yake, sio anaamka saa 5 alafu anategemea baadhi ya majukumu yake (not family in general) afanyiwe!!!
Hilo moja wapo.
Mabadiliko mengine ndugu wanatakiwa wazoee, akishaoa ameoa hivyo mwacheni asumbuke na mke wake. Mkiwa na shida pigeni simu, kama msaada unawezekana mtapewa, kama hauwezekani mnakubali kwamba haiwezekani.