Tetesi: Nafasi zote zilizotangazwa na Tume ya Taifa ya uchaguzi za kusimamia Uchaguzi kushikwa na makada wa CCM!

Nimekwambia kuwa nimepata habari from "realiable source" inaniambia kuwa lile tangazo la NEC, ni "bortion" tu, wakati mpango umesukwa ndani ya NEC, ya kuwaleta wakereketwa wa CCM pekee, kushika nafasi hizo za kusimamia chaguzi hizo!
Hiyo mbona haitaki tochi! Wewe ushatowa habari achana nao hawa vikaragosi. Kama wanataka maelezo zaidi basi wakubali mdahalo.
 
Unavithibitisho vya hili unalolisema? Unasema WATAKAOOMBA NI MAKADA WA CCM ina maana Nyinyi ACT, CUF, TLP,UMD, NCCR, NRA, CHAUMA, AFP, DP, CHADEMA, UPDP, UDP na wengineo hawaruhusi kuomba au inakuaje hapo. Inamaana barua yamaombi unayoandika kuna sehemu umeambiwa useme wewe ni Kada wa Chama fulani?

Sawa Kama hilo litashindikana VYAMA VYETU VYA SIASA vitataka MAWAKALA je lini wanatangaza hizo nafasi tukaombe?

Maana Mawakala zaidi ya laki tatu watahitajika Nchi mzima hizo ni ajira tosha za muda. Na kuna vyama vinalipa hadi 200k kwa siku tusiache hizo fursa. Tukaanza kuilaumu wanaolipa 25/30
 
Hili ndilo linalotokea katika nchi hii..kama wewe sio mchama lao hata kama una sifa zote hatapata kazi. Mfano wakurugemzi ambao kigezo zamani ilikua usomi na utaalam wa mtu sasa hivi uchama ndy kigezo kikuuu..hii ni Habari mbaya kw sisi na wale waliosoma lakn hawana vyama. Mfumo huu usipofumuliwa kuna ubaguzi mbaya unaenda tokea siku za mbele.!!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Huu ubaguzi unaoendelea nchini, wa ili upate kazi, inabidi utoke chama cha mbogamboga, hakika unakwenda liangamiza Taifa hili
 
Mipango yao ya hovyo kila mwaka inafahamika lakini huwa haina maana yoyote, haiwasaidii chochote.
 
Watakuwa makafara ya ushindi wa CCM,Tundu lissu ameshasema mwaka huu hakuna utani,unasimamia uchaguzi harafu unafanya madudu ujue wananchi hawatavumilia hila ,watagawana nyama kisha unachemshwa watu wanakula na kunywa supu.
Hahaha
 
Watakuwa makafara ya ushindi wa CCM, Tundu lissu ameshasema mwaka huu hakuna utani,unasimamia uchaguzi harafu unafanya madudu ujue wananchi hawatavumilia hila, watagawana nyama kisha unachemshwa watu wanakula na kunywa supu.
Kumbuka kuna maisha baada ya uchaguzi. Utakuja kuyarudia haya maneno yangu
 
Nimekwambia kuwa nimepata habari from "realiable source" inaniambia kuwa lile tangazo la NEC, ni "bortion" tu, wakati mpango umesukwa ndani ya NEC, ya kuwaleta wakereketwa wa CCM pekee, kushika nafasi hizo za kusimamia chaguzi hizo!
Huo ni umbea wa kutafuta hurumaa ili wewe utengeneze kiki zako. Hovyo kabisa nyiee
 
Kwa kujishtukia huku hata nchi hatuwapi mtakuwa mnajitekenya tekenya kwa mabeberu
 
Kumbe ndio maana niliona mahali fulani jiwe anasema wawape kura madiwani na wabunge wa ccm maana yeye hata wasipomchagua atashinda tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…