Nafikiria kuacha kazi ya ulinzi kabla ya 2025

Nafikiria kuacha kazi ya ulinzi kabla ya 2025

Huko morogoro kqenye heka una hata kachumba kamoja. Mana nafuu ya maisha inaeza kupatikana primarily ukopunguza matumizi hasa ya nyumbani. Ukiacha kazi na mzigo wa kodi na kula au matumizi mengine utajutia maradufu
Hapa unaweza kutengeneza wazo.

Katika heka moja yake atengeneze makazi then aiweke familia huku yeye akiendlea kutafuta fursa nzuri .

Na amesema amesoma kilimo.
 
Hapa unaweza kutengeneza wazo.

Katika heka moja yake atengeneze makazi then aiweke familia huku yeye akiendlea kutafuta fursa nzuri .

Na amesema amesoma kilimo.
Mana hata sio yeye tu mbona watu wengi humuhum jf wameacha kazi za maslahi dun na mpaka leo hakuna kazi nyingine wamepata. Kazi inaachwa kimikakati mana maisha ya possibility ni mabaya kuliko maelezo. Hakuna kitu kibaya kama kuacha kazi mbaya ili ukaitafute nzuri au ukaanzishe biashara.

Hapo aangalie steps za kupita kabla hajafanya maamuz hayo. Ofkooz kaz za ulinzi ni ngum na masimango ya kusaidiwa ji mengi kana kwamba unasaidiwa tu.. lakin madhara ya kuiacha na kuanza kutafuta mbadala wake yanaweza kuwa makubwa zaidi ya hayo
 
Hasara nyingine ya kazi yako ni kutyombew@ mkeo usiku kucha wewe unapokuwa lindo.
Imagine mwaka mzima wewe hudinyi mkeo usiku,unajua Raha ya kudinya usiku wa manane??
 
Wazo lako ni jema ,mimi nimepitia kwenye kazi ya ulinzi,nilianzia Dodoma huko UDom tena kule ng'ong'ona wakat kuna ujenzi baadae wakanihamishia bungeni kulinda vifaa vya kampuni inayofanya maintenance bungeni,ilikuwa 2010,kampuni Ya ulinzi VSS tulikuwa tunapewa kilo moja tu,niiliacha nikahamia Dar,nikajiunga KK security,miezi sita baadae nikajiunga,venture risk menegement,2012 nikajiunga na G4S nikapelekwa zanzibar lengo ukiwa nikiwa nasikilizia mchongo maana nilikuwa na kadiploma ka business admin nako nilikapatia humo humo kwenye ulinzi maana nilikuwa mzee wa night shift,ilipofika 2014 January kwa hiari yangu niliamua kulizaini niliandika barua kwa branch manager ,akaniita akanipa wiki nifikirie maamuzi yangu,maana skuwa na shida na kampuni baado baada ya wiki jibu ni lile lile basi nikapewa barua kuja HQ ya G4S kupata haki zangu ,nikapewa nusu mshahara wa mwezi unaofata kama taratibu tao zinavyosema kwa alierizaini,basi nikapewa barua ya mafao yangu huko PPF baada ya mwezi nikawekewa 1.2m basi nikaanza maisha mengine japo nilipofikia zaidi ya miaka sjasimama kimaisha maana niliingia kusomea tena mambo mengine baadae nikaingia kusomea afya japo mambo hayajasimama sawa kiwango nachohitaji ila tangu miaka 10 niache huko jamaa zangu waliokomaa huko huko baado hakuna kilichobadilika kuanzia mshahara ni ule ule na wamekuwa waoga kuacha kazi zaidi ya swali maana tayari wanafamilia zinawategemea pakubwa,hivyo kutokana uzoefu wangu kwa hiyo mchongo nakushauri acha kabla hujachelewa tayari nyenzo unayo ya ujuzi wa kilimo jichanganye kwenye mchongo wowote upate hata m1 tafuta kakijiji anza kaduka ka pembejeo utafanikiwa tu,kuna maeneo ya wakulima na wafugaji wengi huko ukaguzi ni nadra utafanya hata bila usajili wa ofisi kila la kheri.
 
Mnatutukanaga sisi wabeba box hatuna lolote. Tunachamba marinda ya wakongwe hadi tumechizika. Haya bana kila la heri.

Dr Restart HIMARS inamankusweke

Nyau de adriz
Wewe kenge usiniweke kundi Moja na wewe mchambaji.

Ila wanakudharau Bure tu. Hukosi 15$ at minimum per hour.

Hela yake tu unapata kwa siku moja tu. Kwa average ya 8 hours a day.

Mamaeeeee
 
Siku ukiwa na muda ingia masokoni hasa haya masoko ya vyakula kama mabibo, buguruni, sterio nk utapata idea ya kitu cha kufanya achana na na huko kariakoo au karume, mawinga wengi wanafake maisha na utapeli + kujuana kwingi ila kama ni mjanja mjanja kutakufaa pia.

Mshahara wa 250k na una familia ni mdogo na ukizingatia unaupata mwisho wa mwezi, hapo hata bia huwezi kunywa.

Muda wa maamuzi ni sasa.
 
Kazi ya ulinzi ni ngumu sana bro naamini hata wewe haikua rahisi awali kufikiria kuifanya ila ipo sababu iliyopelekea hadi sasa unaifanya.
Unatakiwa uiache lakini usiache kwakua una hasira jiridhishe na mmaamuzi uwe na tawi la kushikilia baada ya kuachia hiyo kazi
 
Kazi ya ulinzi ni ngumu sana bro naamini hata wewe haikua rahisi awali kufikiria kuifanya ila ipo sababu iliyopelekea hadi sasa unaifanya.
Unatakiwa uiache lakini usiache kwakua una hasira jiridhishe na mmaamuzi uwe na tawi la kushikilia baada ya kuachia hiyo kazi
Mifano tunayo humu jf
 
Mfungulie mkeo genge au kuuza vitafuno mtaan ili kupunguza ukali wa maisha

Wakati huo fanya just chini uwe unasave 50,000 kila mwezi in two years ili upat e ya kuanzia ukiondoka
 
Hasara nyingine ya kazi yako ni kutyombew@ mkeo usiku kucha wewe unapokuwa lindo.
Imagine mwaka mzima wewe hudinyi mkeo usiku,unajua Raha ya kudinya usiku wa manane??
Anamdinya akiwa off. Si wanakuwaga na off.
 
Habari za muda huu hapa,

Naishi Dsm Nina familia ya mke na mtoto mmoja.

Kazi --nimeanza kufanya kazi ya ULINZI kwenye kampuni binafsi la Gardworld, nikiwa hapa hapa Dsm.
Maisha yamekuwa magumu sana na hakuna maendeleo yoyote nayoyaona zaidi ya kulipia Kodi,na kupata Hela ya kula basi,Ukizingatia huu ni mwaka wa 3 Sasa nipo kwenye kazi hii.

Awali tulikuwa tunalipwa 250k take home baadae ikaja kupanda Hadi 370k take home,kibaya zaidi LINDO nilililokuwepo mkataba ukafa ikabidi tupewe termination letter na watu wengi sana waliachishwa kazi ilikuwa 2022 kuingia 2023 ,nikasain garda west kama kampuni ndogo yake na mshahara kubakia 250k Tena.

Nimefanikiwa kununua eneo la eka Moja Morogoro.

Hii kazi Sasa naona niache nikafanye shughuli ata za kilimo shamba kuliko kuendelea kuteseka namna hii,unalala nje mbu wako, mvua yako,jua lako, mashanyanyaso mengi, hupati haki zako za Msingi.

Mawazo yenu wadau,au nitakuwa nakosea kuacha kazi hii ambayo haina manufaa zaidi sana ni kudumaza akili tu.

Elimu yangu nimesoma diploma ya Agri business lakini nimetuma maombi ya kazi mara nyingi sijabahatika kupata kazi ya career yangu.

Mshahara wa 250000 Kwa Jiji hili la Dsm naona napoteza muda wangu tu.

Naomba ushauri wowote nitasoma Kila comment.
Dahh pole sana.
Hii kazi niliwahi kufanya mwaka 2021 kampuni hyo hyo ya Garda world kwa muda wa miezi sita pale coca-cola.

Aisee hii kazi iskie tuu, lkn ni moja ya kazi sana yenye changamoto nyingi kama ifuatavyo.
1. AFYA NA UHAI.
Afya yako inakua hatarini kutokana na mkesha wa usiku kucha hivyo utapigwa na mbu, baridi Kali pamoja na viungo vya miwili kuchoka. Lakini pia maisha yako hatrn kutokana na vibaka wenye silaha.
2. MASLAHI HAFIFU.
Hapa mshahara utakaopata ni wakukusogeza NDANI ya mwezi husika lkn kuhusu malengo ni ngumu.
3. JELA.
Ukiwa mlinzi tegemea matatu yatakutokea endapo uvamizi wa majambazi utatokea. Kupambana nao wakupe kilema cha maisha ama wakuue au laa ukimbie lkn ujiandae na JELA.
MACHACHE MAZURI KUHUSU KAZI HII.
1. Unaweza kubahatika kupangiwa Malindo ya ubalozi Huwa wanalipa helanzuri .
2. Unaweza kupata promotion ya kuwa kiongoz lkn lazima uwe mnoko kwa wenzako.
3. Unaweza kupata LINDO ambalo halina changamoto sana hivyo kazi utaoyona nzuri.
HITIMISHO.
KWAKWEL wakati nafanya hii kazi nilijiambia moyoni , sikuja duniani kuwa mzinzi na hayo ndo yalikua majibu yangu hata kwa wale viongozi waliokua wanoko ambao ukisnzia tuu picha shwaaa.

USHAURI KWAKO NA VIJANA WENGINE WAPAMBANAJI.
Tafuta hata boda boda ya mkopo, komaa na Jiji MUNGU ATAKUSAIDIA ndugu yangu.
Kijana yeyote, katika maisha yako kazi iweke chaguo la mwisho kabisa baada ya kujaribu vitu vyote duniani hapa vimeshindikana.
Ile kazi ni kama mfungwa huru. Yani kila mtu wewe ni boss wako mpka mfagizi wa nyumba.
Nna mengi ila kwaleo yanatosha
 
Kama mtafutaji mwenzako na mtoto wa kiume pia naweza kukupa ushauri kidogo.

Ukiona mwanaume mwenzako anakuja na mada kama hizi tena haombi pesa ila ushauri inabidi umfikirie mara mbili. Sometimes mambo yanatutinga na huna wa kuongea nae ndio maana unakutana na mada kama hizi.

Kuna jamaa miaka kipindi namaliza shule ya msingi kitambo kidogo, alinifundisha mbinu fulani ya kuitumia kama unataka kuwa na busara.

Aliniambia fikiria kitu chochote kile cha kipuuzi na kipumbavu ambacho unahisi ukikisema mbele za watu lazima washtuke. Akanipa kama sekunde kumi za kufikiria. Kisha akaniuliza kama nimekipata, nikajibu ndio huku nikiwa na hamu kweli ya kukisema lakini you know what? Alinikata moto kwa kunizuia nisiseme.

Hivyo ndio tunavyomasta kutoongea upumbavu mbele za watu na kuwa mtu mwenye busara.

Ulikua na chaguo la kutocomment kwa kuwa huna cha kumshauri ila ukaona kumfananisha na binti ni chaguo sahihi.

Don't take it personal bro, ushauri tu.
Binti Magnifico,
Umevunja Kanuni ya unayoita 'busara' ni aibu mtoto wa kiume kuomba omba ushauri kwa kazi ambayo uliitafuta mwenyewe. IPO siku atakua kuomba ushauri kuwa boss wake anamtongoza male Tigo sijui mtamshaurije?
 
Back
Top Bottom