Nafungua Butcher Shop kubwa ya kisasa, Nahitaji msaada wenu kwa yafuatayo

Nafungua Butcher Shop kubwa ya kisasa, Nahitaji msaada wenu kwa yafuatayo

fishmarket

New Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
1
Reaction score
1
Hi guys,

Nimetenga pesa kwajili ya kufungua fresh meat Butcher, kubwa na ya Kisasa maeneo ya Sinza (Meeda/Lufungira).

Butcher yangu haitauza red meat. Natazamia kuuza bidhaa zifuatazo:

1. Samaki ( Sato, Red snapper na wengineo )
2. Kuku ( wa Kienyeji na Kisasa )
3. Mayai ( Ya kienyeji )

Bei zangu zitakua za nafuu sana sababu strategy yangu ni ya kuuza kila bidhaa kwa faida ndogo.

Pia, Nitaweka huduma ya Home and Office Delivery kwa gharama ya tzs 1,000 tu!


MSAADA:

Naomba msaada wenu katika haya:

1. Wapi naweza kununua mashine ya kukatia nyama, na bei yake ni shillingi ngapi?
2. Wapi naweza kununua weighing scale kwajili ya kupima uzito, ile ya mezani ambayo ni digital na ile ya kuning'iniza inayosoma kwa mshale. Bei zake zikoje hizi mizani?
3. Nahitaji supplier atakaeweza kuniletea Sato kutoka mikoa ya Mwanza/Musoma mpaka Dar kwa bei nzuri. Nitaanza kwa kuchukua 150kg per week, then 200kg per week na kuendelea.
4. Nahitaji suppliers watakaoweza kuniuzia mayai ya kienyeji kwa bei ya jumla, bei isioumiza.
5. Nahitaji Frame ya size nzuri, isiwe ndogo. Maeneo ya Sinza Lufungira kama unaelekea Meeda.
6. Nahitaji ushauri wa Freezer za kununua na wapi nitapata na kwa bei gani.

CONTACT:
Steve,
Mob: +255787220742

ASANTENI.

 
kungekua na mafriza ya solar yaliyothibitishwa bora ungenunua kuliko kutegemea umeme. Nway naona kama umepanga kuanza kwa kasi sana ungeanza polepole usome kwanza raman
 
uwe makini na hao masupplier ambao unataka kuingia nao makataba kwani wanaweza kukluletea samaki ambao sio fresh mwishoe inakula kwako ni bora kwa mwanzo uwe unaagiza mwenyewe kisha unakwenda kuwachukua kwa wasafirishaji wa mzigo wako
 
kungekua na mafriza ya solar yaliyothibitishwa bora ungenunua kuliko kutegemea umeme. Nway naona kama umepanga kuanza kwa kasi sana ungeanza polepole usome kwanza raman

KUna mtu anauza yumo humu humu jf alishawahi kuyatanganza sijui mwaka jana ule atafute freezer za solar nafikiri kitu kama hicho, all ze best
 
Machine ya kukatia nyama milioni moja,
mizani 140,000 - 180,000
Ukitaka mchanganuo zaidi jaribu kutembelea butcher mbalimbali zilizopo Mwenge
 
Fanya analysis ya kutosha ndio uanze biashara unayotaka kuifanya maana kwa maelezo yako inaonekana hata business plan hauna sasa utajua vp kama hiyo biashara inalipa au lah. Maana kama ujui hata bei ya mafreezer na mizani wakati umeshafikiria kuanzisha butcher basi hujafanya analysis nzuri.

Ushauri naheshimu wazo lako ila jaribu kutembelea watu wenye butcher za kisasa kama unayoifikiria waulize na uandike gharama pamoja na changamoto zake pia makisio ya mapato utakayoweza kupata
 
Back
Top Bottom