analysti
JF-Expert Member
- Aug 24, 2009
- 731
- 614
mikela, kununua tv nyingine na kuhamia chumbani haina tofauti na kuhama nyumba kwa sababu tu ya kutofautiana kitu na mwenzio/wanao. kama baba kuna umuhimu wa kujua wanao wanaangalia nini, na wanafanya nini wawapo nyumbani. hii ina maana na baba pia ata-sacrifice kutoangalia mpira na boxing, na mama nae na movies zake pia ziwe rehani. pia ni muhimu kufundisha watoto kushare resources na watu waliopo nyumbani kwao. kuna watu ofisini ukisafiri nao humo garini atataka msikilize kwaya yake tu (anakuja na cd kabisaa), mle hoteli aliyoizoea na kulala anapotaka yeye! nadhani kunaanzia huku. wafundishe wanao kuwa tunaweza kuangalia cartoon, na national geographic wajifunze kitu pia. na ccn ili wajue world news. humo kwenye movie za kiswahili na ki-nijeria nisitie neno manake sioni watakachojifunza zaidi ya miondoko feki na english mbobu, ila inahitaji kuwashawishi pia!
hata kama unanunua tv ya chumbani ni kwa ajili ya kuangalia news za alfajiri wakati unamuwinda mama nanilii kwa morning glory. sio kwa ajili ya kukimbia wanao na cartoon. ni mtizamo tu lakini...
Marvelous point!!