Nahisi Jamaa yangu anapata heat stroke.

Nahisi Jamaa yangu anapata heat stroke.

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Huyu Jamaa yangu kutoka Arusha yupo Dar kwa wiki kadhaa sasa. Siku kadhaa zilizopita akiwa anaangalia mpira kwenye kibanda umiza ile mechi ya Yanga na Kengold, kipindi cha pili mwishoni alianza kujisikia kizunguzungu kikali,anasema macho yake yakawa yanashindwa kuangalia screen, kichefuchefu na jasho linamtoka sana, akaomba asaidiwe atoke nje, akaenda akajilaza barazani kwa muda mpaka alipojisikia vizuri, akaondoka kwenda kwake.

Siku kadhaa tena baadae akiwa kwake usiku hali ile ilimrudia tena, akahangaika mpaka akalala asubuhi hali ikawa mbaya zaidi akakimbizwa Zahanati ya jirani. Akachukuliwa vipimo ikaonekana presha ,sukari, maleria, wingi wa damu vyote vipo sawa, ila bado Mgonjwa yupo hoi.

Akawa refered Kimara Health center, Kimara wakarudia vipimo vilevile nao hakuna walichogundua. Kuna dawa wakamchoma na kumtaka arudi nyumbani ingawa bado hali yake ilikuwa haijatengemaa na walikuwa wanasisitiza kuwa hawaoni tatizo hivyo hana sababu ya kuendelea kuwa pale,jambo lililomshangaza sana Mgonjwa.

Swali ni je huyu hakuhitaji tiba ya heat stroke kwa dalili zile badala ya Watabibu kuridhika tu kuwa hawaoni tatizo kwenye vipimo vyao? Nini tiba ya heat stroke na je haiwezi kumshambulia tena.
 
Huyu Jamaa yangu kutoka Arusha yupo Dar kwa wiki kadhaa sasa.Siku kadhaa zilizopita akiwa anaangalia mpira kwenye kibanda umiza ile mechi ya Yanga na Kengold,kipindi cha pili mwishoni alianza kujisikia kizunguzungu kikali,anasema macho yake yakawa yanashindwa kuangalia screen,kichefuchefu na jasho linamtoka sana,akaomba asaidiwe atoke nje,akaenda akajilaza barazani kwa muda mpaka alipojisikia vizuri,akaondoka kwenda kwake.Siku kadhaa tena baadae akiwa kwake usiku hali ile ilimrudia tena,akahangaika mpaka akalala asubuhi hali ikawa mbaya zaidi akakimbizwa Zahanati ya jirani.Akachukuliwa vipimo ikaonekana presha ,sukari,maleria,wingi wa damu vyote vipo sawa,ila bado Mgonjwa yupo hoi.Akawa refered Kimara Health center,Kimara wakarudia vipimo vilevile nao hakuna walichogundua.Kuna dawa wakamchoma na kumtaka arudi nyumbani ingawa bado hali yake ilikuwa haijatengemaa na walikuwa wanasisitiza kuwa hawaoni tatizo hivyo hana sababu ya kuendelea kuwa pale,jambo lililomshangaza sana Mgonjwa.Swali ni je huyu hakuhitaji tiba ya heat stroke kwa dalili zile badala ya Watabibu kuridhika tu kuwa hawaoni tatizo kwenye vipimo vyao?.Nini tiba ya heat stroke na je haiwezi kumshambulia tena.
Hosp zoore hizi jamanìiii.....aende hata Amana au Mnyamala....kama anajiweza au bima aende Botch hapo.....unahangaila Disp wanakupima kwa mkono ebooo
 
Mpelele hospitali kubwa.

Juzi jamaa yetu mmoja alikua anajisikia hovyo, kwenda hospitali wakamwambia mshipa wa moyo umeziba. Ni kama bahati aliwahi mwenyewe kwenda, angechelewa asingefika kesho yake.

Aende hospitali kubwa haraka sana.
Sio kwamba nao wanawajibika kutoa referral kwenda mbele badala ya hicho walichofanya?Ingawa tayari tunaelekea kutafuta huduma zaidi kwingine ila hatukuridhika kabisa na walivyochukulia tatizo serious kama hilo.Nimeleta huku jf kwa faida ya wengine pia.
 
Yaani unapata heat stroke usiku?

Hebu nenda kafanye vipimo vya uhakika hospitali kubwa
Sasa kama una ufahamu wa ziada toa elimu tujue kuhusu heat stroke.Mwanzo aliipata jioni na baadae ndio ikamtokea usiku,au hizo dalili zaweza kuwa tatizo gani maana presha,sukari zipo sawa.
 
Sio kwamba nao wanawajibika kutoa referral kwenda mbele badala ya hicho walichofanya?Ingawa tayari tunaelekea kutafuta huduma zaidi kwingine ila hatukuridhika kabisa na walivyochukulia tatizo serious kama hilo.Nimeleta huku jf kwa faida ya wengine pia.
Hospitali zote hata Muhimbili ama jakaya Kikwete unaenda hata kama hujawahi kutibiwa pale hawakukatai, wanakupokea wanakuandikishia jalada unaanza vipimo. Sio lazima uwe na rufaa.
 
Sasa kama una ufahamu wa ziada toa elimu tujue kuhusu heat stroke.Mwanzo aliipata jioni na baadae ndio ikamtokea usiku,au hizo dalili zaweza kuwa tatizo gani maana presha,sukari zipo sawa.

Hiyo sio heat stroke kwa sababu mazingira uliyotaja hayashawishi hivyo...

Dalili ulizotaja ni za kiujumla sana si lazima iwe ana shida ulizotaja, mathalani hata mtu mwenye uvimbe kwenye ubongo huwa anakuwa na dalili hizo, upungufu wa maji mwilini, wingi wa sumu mwilini TSS n.k

Ndio maana watu wote hapa wanasema nenda hospitali kubwa kwa vipimo zaidi...
 
Back
Top Bottom