Nahisi kufa nahitaji msaada wa haraka

Ngoja nami nitie neno;
Pole sana mkuu
ila mimi huwa naamini katika mawazo chanya, unaweza kuhangaika weeh ukaja kugundua tatizo lipo kwenye mzunguko wako wa maisha ya kila siku na ukaja kupona kwa jambo dogo sana kwasababu hio nakushauri usikate tamaa japo ni ngumu kwa nyakati hizi ila kadri unavyoamka kila siku tambua una nafasi ingine...
maisha huwa ni mbele kwa mbele! ukishindwa huku jaribu kule ukikwama hapa jaribu pale, kama umehangaika sana hawaoni tatizo jaribu hata wewe kufikiri nje ya box jichunguze lifestyle yako, hata wanaposema kama maisha yanakukataa Dar hamia mbeya huwa wanamaana! kubadili hali ya hewa ukapata mzunguko mpya w amaisha huwa ni tiba... ukifungua mlango mmoja unafungua mingine zaidi..
- kwenye maisha anagalia mbelee usitake kujua umeteseka kiasi gani kwa miaka mingapi! usitake kujua mwisho wako ni upi wewe nenda mbele kwa mbele ukijaribu hili na lile mpaka tiba sahihi itapatikana
simaanishi uwe desperate na kupona! hangaika ila ishi usisahau kuishi haijalishi unapitia nini pengine katika kuishi kuna tiba yako.
- Muachie Mungu afanye kitu juu yako maisha ni fumbo kubwa sana...na Mungu huwa ana njia zake za kujibu maombi yako.
maisha ni kama bahari sisi wafa maji sikuzote hatutaisha kutapatapa wewe unatapatapa na spinal mimi natapatapa na ujane na yule anatapatapa na mtoto mshenzi
kwahiyo kaza moyo usikate tamaa dawa ipo na kesho yako ni njema
 
Ushauri mzuri
 
Ahsante sana mkuu kwa kujari na ushauri wako nimeupokea kwa mikono miwili, ubarikiwe sana mkuu
 
labda ni vidonda vya tumbo. nenda kajaribu kupima vidonda vya tumbo kwa kipimo kile kikubwa kabisa.
 
Hiyo nazami ni ni UTI type II, niliumwa mgongo na kiuno kidogo, muda mrefu ila mkojo haumi, nikatumia vidonge Azuma kutwa mara 1 x 7 days, imeondoka. Nimeambiwa Azuma pia inatibu typhoid ,mimi sio daktari, ils mimi nilikuwa nahisi pia kams kuna kitu nimebeba eneo hilo kusabisha kuchoka sana hsda kams natembea na inabidi nipande mlima au mwinuko. Huenda wewe una tatizo tofauti ila hata mimi lilidumu muda mrefu.
Kwa hiyo nimepona hata mi sielewe ni kisukari type 2 au uti ila vidonge nilivyotumia ni hivyo,Sikwenda hospitali ila tatizo limeisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…