Nahisi sina bahati na biashara

Nahisi sina bahati na biashara

Uganga ni maarifa yaliyoumbwa na mungu waliyonayo wanadamu .kinachoponya TV ni ufundi wa kutengeneza TV sasa ww TV imeharibika Anza kusema maarifa yote ya mungu uanze kuomba mungu .acha ujinga nenda kwa fundi TV dakika tano TV inapona.
Ndio nimekwambia hata huyo fundi TV anamuomba Mungu TV ipone Mungu akitia lock hata fundi aweje TV haiponi
 
Biashara yoyote unayoanza na kuanza kukupa faida papo kwa papo, haiwezi kukutajirisha, utaishia kupata vichenji vya kula tu, huwezi piga hatua zaidi..! Biashara za kukupa utajiri huwa ni ngumu sana unaweza fanya mwaka mzima huoni faida zaidi ya kutumia tu, ila siku ikianza kukulipa utajiri huo hapo. Watu wengi huwa wanachemka kwa kukosa focus and Consistency, wewe mara umeenda chunya ukakimbia, mara tunduma ukakimbia tena....! Utajikuta miaka inaenda hakuna cha maana umefanya, utatafuta mchawi wako ingali mchawi ni we mwenyewe....! Kuna siri kubwa kwenye kufanya kitu kimoja kwa muda mrefu mpaka upate matokeo chanya acha kuruka ruka, tafuta kitu kimoja pambana nacho mpaka kieleweke....! Sasa mwezi mmoja tu unataka biashara ianze kukulipa kweli, bado una vingi vya kujifunza kwenye hiyo biashara tofauti na kuwaza faida kwanza
 
Biashara yoyote unayoanza na kuanza kukupa faida papo kwa papo, haiwezi kukutajirisha, utaishia kupata vichenji vya kula tu, huwezi piga hatua zaidi..! Biashara za kukupa utajiri huwa ni ngumu sana unaweza fanya mwaka mzima huoni faida zaidi ya kutumia tu, ila siku ikianza kukulipa utajiri huo hapo. Watu wengi huwa wanachemka kwa kukosa focus and Consistency, wewe mara umeenda chunya ukakimbia, mara tunduma ukakimbia tena....! Utajikuta miaka inaenda hakuna cha maana umefanya, utatafuta mchawi wako ingali mchawi ni we mwenyewe....! Kuna siri kubwa kwenye kufanya kitu kimoja kwa muda mrefu mpaka upate matokeo chanya acha kuruka ruka, tafuta kitu kimoja pambana nacho mpaka kieleweke....! Sasa mwezi mmoja tu unataka biashara ianze kukulipa kweli, bado una vingi vya kujifunza kwenye hiyo biashara tofauti na kuwaza faida kwanza
Mkuu nimekuelewa mpaka nimepitiliza, barikiwa sana.
 
Nenda lindi au mtwara chukua ekari 5 anza ufugaji wa mbuzi na kuku wa kienyeji. Hakikisha unalima miti ya kukusaidia kulisha mbuzi wakati wa kiangazi. Weka makazi yako hapo usitake kufanya kilimo cha m Pesa na simu, kaa hapo mwenyewe hata mwaka mzima.

Kama unatumia kitimoto nenda sehemu yoyote wanapolima mahindi kwa wingi fuga kitimoto jike 8 dume wawili baada ya mwaka mmoja utanishukuru

Wakati unaendelea na ufugaji lima pia mahindi na maharage

Samaki mimi huwa sizielewi kabisa
Siku ya kwanza kujifunza self defence nikaelewa why Kuna master wa kungfu
 
Habari wakuu, nipo kwenye kisiwa cha maisome kilichopo Sengerema, nina mwezi sasa nafanya biashara ya uchuuzi wa samaki aina ya sato natoa huku napeleka Mwanza ila faida sipati kwasababu nilikuwa nachukua kwa walanguzi sio direct kutoka kwa wavuvi so faida ilikuwa inaishia kwenye malazi na usafiri, ndio nikashauriwa nitafute wavuvi niwadhamini nyavu, pumba na kuwakodishia mitumbwi ili waniuzie samaki kwa bei rahisi kidogo.

Aisee nina week zaidi ya mbili hapa wavuvi kuwapata imekuwa mziki, wote wako chini ya watu nazidi kula mtaji tuu nishaanza kukata na tamaa, kuna wavuvi nilifanyiwa connection kutoka kisiwa kingine nikaongea nao vizuri tuu waje nikawapa na offer nzuri but toka juzi wananiambia wameshakuja wapo ila nikiwaambia tuonane tuongee wananiambia wanakuja, muda unazidi kwenda hakuna ninachofanya yaani basi tuu haya maisha hayana maana, mtanisamehe kwa uandishi m'bovu, nipo confused.
Acha kujitetea mtaji umeshaubugia wewe.

pesa ya mtaji tamu sana ile chomoachomoa kidogo kidogo..ukija kushtuka dah kwisha..
 
Uza hata chai hapo fungua mgahawa wa kishkaji kupika vuta Dada mmmoja
Nenda na mda usisubiri mvuvi aje akupe dili la samaki
Na hao samaki na chapati na mimi ntakuja
 
Habari wakuu, nipo kwenye kisiwa cha maisome kilichopo Sengerema, nina mwezi sasa nafanya biashara ya uchuuzi wa samaki aina ya sato natoa huku napeleka Mwanza ila faida sipati kwasababu nilikuwa nachukua kwa walanguzi sio direct kutoka kwa wavuvi so faida ilikuwa inaishia kwenye malazi na usafiri, ndio nikashauriwa nitafute wavuvi niwadhamini nyavu, pumba na kuwakodishia mitumbwi ili waniuzie samaki kwa bei rahisi kidogo.

Aisee nina week zaidi ya mbili hapa wavuvi kuwapata imekuwa mziki, wote wako chini ya watu nazidi kula mtaji tuu nishaanza kukata na tamaa, kuna wavuvi nilifanyiwa connection kutoka kisiwa kingine nikaongea nao vizuri tuu waje nikawapa na offer nzuri but toka juzi wananiambia wameshakuja wapo ila nikiwaambia tuonane tuongee wananiambia wanakuja, muda unazidi kwenda hakuna ninachofanya yaani basi tuu haya maisha hayana maana, mtanisamehe kwa uandishi m'bovu, nipo confused.
Hebu nikwambie jambo ambalo huenda hakuna mtu atakayekuambia...

Uvuvi na madini ni kazi zinazohitaji uwe na uimara wa kiroho...

Ikiwa umetoa Hela na ahadi ya bei nzuri na bado huoni watu kukuchangamkia, ni ishara nyota Yako haiko sawa...

Kazi kama hizo unakuta kuna wafanyabiashara umewakuta, sio rahisi wakuache ufanikiwe kirahisi.

Ungejitahidi kuogea chumvi ingekusaidia.

Biashara yoyote bila Imani dhabiti kamwe hufanikiwi...
 
Hebu nikwambie jambo ambalo huenda hakuna mtu atakayekuambia...

Uvuvi na madini ni kazi zinazohitaji uwe na uimara wa kiroho...

Ikiwa umetoa Hela na ahadi ya bei nzuri na bado huoni watu kukuchangamkia, ni ishara nyota Yako haiko sawa...

Kazi kama hizo unakuta kuna wafanyabiashara umewakuta, sio rahisi wakuache ufanikiwe kirahisi.

Ungejitahidi kuogea chumvi ingekusaidia.

Biashara yoyote bila Imani dhabiti kamwe hufanikiwi...
Nakubaliana na wewe mkuu, vp chumvi ya mawe pekee itasaidia?
 
Back
Top Bottom