Jana ya siku ninayotaka kuielezea alikuja ndugu yangu kwa lengo la kushauriana afanye nini kujikwamua kiuchumi.Hapo ni baada ya kuachwa na mwanaume aliyekua akimtegemea kwa kila kitu.
Wakati tunapiga piga story uwani geti likagongwa,mlinzi na dada hawakuwepo so nikamuomba akachungulie ni nani.Akaenda na alivyorudi akasema kuna chizi anaomba machupa.Nikamwbia ngoja nikamkusanyie nimletee ila akasema nimemfukuza hawa mara nyingi ni wezi.
Nikatoka fasta kumstopisha asubiri machupa manake yalikuwepo mengi plus ndoo zilizopasuka.Cha ajabu natoka getini namkuta kakaa nje ya geti.Nikamwambia subiri nakuletea machupa.Nikamletea then nikaingia ndani nikamuacha akiweka machupa kwenye roba lake mimi nikaingia zangu ndani.
Baada ya kama dk 40 geti likagongwa.Akaenda tena ndugu yangu kufungua ila nikamsikia anaongea kwa kufoka kisha akarudi huku anafyonza.Namuuliza vipi anasema si yule chizi wa machupa eti anaomba aingie ndani apumzike.Nikashangaa kwanin hajaondoka muda wote huo ila nikakumbuka alivyokaa pale chini ya geti niliona kama anaumwa vile.Kahuruma kakaniingia,nikahisi ana njaa au mgonjwa.Nikachukua 5k ila wkt nataka kwenda kumpa ndugu yangu akasema "nimemtimua na nimemwambia nisimuone tena hapa".Nikarudi kukaa tukaendelea na story zetu ila baada ya muda geti likagongwa then nikajikuta nacheka jinsi ndugu yangu alivyokunja sura kwa hasira huku akisema"Kama ni yule chizi tena sijui ntamfanyaje".Nikamwambia ngojea niende mimi nina sura ngumu labda ataniogopa😀.
Kufika nje namkuta ni yeye,nikaweka sura ya sitaki masihara kisha nikampa ile elfu tano nikamwambia nenda kale. Akaipokea fasta kisha akanionesha panadol akanambia "Kichwa kinaniuma sana dada naomba nipumzike kivulini japo dk 5 tu hlf naondoka."
Nikamuangalia huku nikiwaza vitu vingi kichwani,vipi akinifia humu ndani,vipi kama ni style ya kuibiwa,n.k.
Kwa kumtizama alionekana mgonjwa kweli so nikamwambia ingia pumzika dk tano tu hlf uende hospital.Ndugu yangu akapinga sana hlf akasema mbele yake kuwa hawa sio wakuwaingiza ndani ni wezi ila nikamuingiza nikamtandikia mkeka nikampa na glasi ya juice then ili kuhakikisha hafanyi ujanja wowote nikaleta kiti nikakaa karibu yake.
Akajilaza pale mkekani kama dk 2 hivi kisha akaamka akakaa akaegemea ukuta halafu akaanza kumponda ndugu yangu nikamwambia achana nae msamehe bure.Basi akawa anaanzisha story za hapa na pale namjibu tu ili asihisi niko pale kumlinda ila baada ya kuongea nae kwa muda nilianza kumchukulia serious.
The guy was so smart na mwenye uelewa mkubwa wa mambo ila kwa muonekano ni chizi kabisaa ananuka ni mchafu kuanzia minywele,kucha mavazi ndio balaa ila ndani ya nusu saa nilijikuta nimejifunza vitu vipya kutoka kwake na nilitaman tuendelee kupiga story hivyo alivyoaga nikamwambia subiri ule ndio uondoke.Akasema si ushanipa hela ya kula nikamwambia hiyo fanya nauli ya hospital.Nikamuomba ndugu yangu ampikie.Akakubali ila kishingo upande.
Basi jamaa akafurahi sana kisha akaanza kunimwagia sifa za uongo.Mara " ooh unajua sista leo ndio nimejua kwanin wenzetu Mungu kawafungulia milango.Huwezi kuwa na roho nzuri kama hivi hlf Mungu asikupe utajiri!".
Nikamwambia mbona yule ndugu yangu unasema ana roho mbaya ila ndo tajiri sasa?Akasema kama kweli tajiri basi Mungu kamnyima neema ya kufurahia huo utajiri mana anaonekana ana stress sana.
Nikamchokoza nikamwambia kwa hiyo wewe una roho mbaya ndo maana leo unaokota machupa.?Akainama chini kwa muda kisha akanambia,sina roho mbaya ila nimefanya vitu vingi vibaya vya kutosha kulaaniwa na Mungu ila ndugu zangu wana mchango mkubwa wa mimi kuwa hivi nilivyo leo ila najipanga nitasimama tena.
Nilimuangalia kwa muda nikijiuliza mengi kuhusu mtu yule kisha akakatisha ukimya kwa kusema "ujue nini sista!?Nimetokea kukupenda sana hivyo nitakupa zawadi ukiipenda haya usipoipenda ipuuze."
Kwa alivyo nikajiuliza mtu huyu ana nin cha kunipa ila nikajifanya niko excited but the smart guy alishasoma body language yangu akasema"najua sina cha maana cha kukupa ila akasema afya yangu ikitengamaa kuna ishu nataka kufanya initoe kwenye haya maisha ila kuna saa najihisi nitakufa hivyo natamani nikifa hiyo ishu imuinue mtu mwingine ila kabla ya kukutana na wewe leo hakuna ndugu wala mtu yeyote moyo wangu umempenda kiasi cha kumpa hiyo ishu.
Nikasema nashukuru kwa upendo huo kaka.Akaniambia hivi shilingi 300 mara 60 zikiongezeka kwenye kipato chako kila siku utahisi chochote au ni sawa na punje ya chumvi baharini.Honestly alivyotamka 300 nilidharau moyonj ila nikapiga hesabu nikaona hiyo ni sawa na 540K kwa mwezi nikamwambia ni hela nyingi itanifaa kwa mengi.
Akakaa vizuri then akanieleza jinsi hizo mia tatu mia tatu zinavyopatikana.Nilichoka.
Yule bwana alikula akaondoka tukiagana kuwa baada ya siku nne atapita tena.Alivyoondoka nikawa nalitafakari lile jambo,nikapiga simu kadhaa kudhibitisha baadhi ya vitu.Nikaamua nitaifanya ila kuna vitu nilitaka anieleweshe ili nisikosee.Siku ya nne,ambapo alisema ni kila Alhamis anapita mtaani kwetu sikwenda kazini kwa lengo la kumsubiri rafiki yangu muokota machupa ila hakutokea,kesho na keshokutwa yake pia hakutokea.Nikamtuma dada aulize kwa majirani kama wanamuonaga wakasema hawajamuona.
Siku miezi ikapita ila mpaka ninaandika hapa sijamuona tena kaka yangu kipenzi ila baada ya muda nikajiongeza nikajaribu na leo naongelea 300 mara mia kadhaa kwa siku.
Natamani sana kujua kuwa yule malaika wangu na yeye anafanya ndo mana hapiti kuokota chupa na sio ugonjwa ulimzidi akafariki 😭😭.
Yule ndugu yangu sikumwambia biashara aliyonifundisha yule bwana,inshort ni zaidi ya mwaka sasa ninafanya hiyo kitu na sijamwambia mtu yeyote na sina mpango wa kumwambia mtu yeyote labda nikijua ninakufa leo ndio na mimi nitatafuta nimpendae nimwambie na kama huyo bwana alikufa basi dunia nzima anayefanya hicho kitu ni mimi peke yangu.
Lengo la kuandika huu uzi ni
1)Nko bored na nikiwa bored napenda kuandika.
2)Naamini hiki kisa kitakufunza vitu.
3)Nataka kukuambia kuwa Mungu yupo.
4)Nataka kukuambia dharau haijawahi kuwa na faida.Kuna saa nahisi yule mtu alitumwa kuleta hizi mia tatu mia tatu kwa huyu ndugu yangu ila dharau zake zikamkosesha neema.
Wakati tunapiga piga story uwani geti likagongwa,mlinzi na dada hawakuwepo so nikamuomba akachungulie ni nani.Akaenda na alivyorudi akasema kuna chizi anaomba machupa.Nikamwbia ngoja nikamkusanyie nimletee ila akasema nimemfukuza hawa mara nyingi ni wezi.
Nikatoka fasta kumstopisha asubiri machupa manake yalikuwepo mengi plus ndoo zilizopasuka.Cha ajabu natoka getini namkuta kakaa nje ya geti.Nikamwambia subiri nakuletea machupa.Nikamletea then nikaingia ndani nikamuacha akiweka machupa kwenye roba lake mimi nikaingia zangu ndani.
Baada ya kama dk 40 geti likagongwa.Akaenda tena ndugu yangu kufungua ila nikamsikia anaongea kwa kufoka kisha akarudi huku anafyonza.Namuuliza vipi anasema si yule chizi wa machupa eti anaomba aingie ndani apumzike.Nikashangaa kwanin hajaondoka muda wote huo ila nikakumbuka alivyokaa pale chini ya geti niliona kama anaumwa vile.Kahuruma kakaniingia,nikahisi ana njaa au mgonjwa.Nikachukua 5k ila wkt nataka kwenda kumpa ndugu yangu akasema "nimemtimua na nimemwambia nisimuone tena hapa".Nikarudi kukaa tukaendelea na story zetu ila baada ya muda geti likagongwa then nikajikuta nacheka jinsi ndugu yangu alivyokunja sura kwa hasira huku akisema"Kama ni yule chizi tena sijui ntamfanyaje".Nikamwambia ngojea niende mimi nina sura ngumu labda ataniogopa😀.
Kufika nje namkuta ni yeye,nikaweka sura ya sitaki masihara kisha nikampa ile elfu tano nikamwambia nenda kale. Akaipokea fasta kisha akanionesha panadol akanambia "Kichwa kinaniuma sana dada naomba nipumzike kivulini japo dk 5 tu hlf naondoka."
Nikamuangalia huku nikiwaza vitu vingi kichwani,vipi akinifia humu ndani,vipi kama ni style ya kuibiwa,n.k.
Kwa kumtizama alionekana mgonjwa kweli so nikamwambia ingia pumzika dk tano tu hlf uende hospital.Ndugu yangu akapinga sana hlf akasema mbele yake kuwa hawa sio wakuwaingiza ndani ni wezi ila nikamuingiza nikamtandikia mkeka nikampa na glasi ya juice then ili kuhakikisha hafanyi ujanja wowote nikaleta kiti nikakaa karibu yake.
Akajilaza pale mkekani kama dk 2 hivi kisha akaamka akakaa akaegemea ukuta halafu akaanza kumponda ndugu yangu nikamwambia achana nae msamehe bure.Basi akawa anaanzisha story za hapa na pale namjibu tu ili asihisi niko pale kumlinda ila baada ya kuongea nae kwa muda nilianza kumchukulia serious.
The guy was so smart na mwenye uelewa mkubwa wa mambo ila kwa muonekano ni chizi kabisaa ananuka ni mchafu kuanzia minywele,kucha mavazi ndio balaa ila ndani ya nusu saa nilijikuta nimejifunza vitu vipya kutoka kwake na nilitaman tuendelee kupiga story hivyo alivyoaga nikamwambia subiri ule ndio uondoke.Akasema si ushanipa hela ya kula nikamwambia hiyo fanya nauli ya hospital.Nikamuomba ndugu yangu ampikie.Akakubali ila kishingo upande.
Basi jamaa akafurahi sana kisha akaanza kunimwagia sifa za uongo.Mara " ooh unajua sista leo ndio nimejua kwanin wenzetu Mungu kawafungulia milango.Huwezi kuwa na roho nzuri kama hivi hlf Mungu asikupe utajiri!".
Nikamwambia mbona yule ndugu yangu unasema ana roho mbaya ila ndo tajiri sasa?Akasema kama kweli tajiri basi Mungu kamnyima neema ya kufurahia huo utajiri mana anaonekana ana stress sana.
Nikamchokoza nikamwambia kwa hiyo wewe una roho mbaya ndo maana leo unaokota machupa.?Akainama chini kwa muda kisha akanambia,sina roho mbaya ila nimefanya vitu vingi vibaya vya kutosha kulaaniwa na Mungu ila ndugu zangu wana mchango mkubwa wa mimi kuwa hivi nilivyo leo ila najipanga nitasimama tena.
Nilimuangalia kwa muda nikijiuliza mengi kuhusu mtu yule kisha akakatisha ukimya kwa kusema "ujue nini sista!?Nimetokea kukupenda sana hivyo nitakupa zawadi ukiipenda haya usipoipenda ipuuze."
Kwa alivyo nikajiuliza mtu huyu ana nin cha kunipa ila nikajifanya niko excited but the smart guy alishasoma body language yangu akasema"najua sina cha maana cha kukupa ila akasema afya yangu ikitengamaa kuna ishu nataka kufanya initoe kwenye haya maisha ila kuna saa najihisi nitakufa hivyo natamani nikifa hiyo ishu imuinue mtu mwingine ila kabla ya kukutana na wewe leo hakuna ndugu wala mtu yeyote moyo wangu umempenda kiasi cha kumpa hiyo ishu.
Nikasema nashukuru kwa upendo huo kaka.Akaniambia hivi shilingi 300 mara 60 zikiongezeka kwenye kipato chako kila siku utahisi chochote au ni sawa na punje ya chumvi baharini.Honestly alivyotamka 300 nilidharau moyonj ila nikapiga hesabu nikaona hiyo ni sawa na 540K kwa mwezi nikamwambia ni hela nyingi itanifaa kwa mengi.
Akakaa vizuri then akanieleza jinsi hizo mia tatu mia tatu zinavyopatikana.Nilichoka.
Yule bwana alikula akaondoka tukiagana kuwa baada ya siku nne atapita tena.Alivyoondoka nikawa nalitafakari lile jambo,nikapiga simu kadhaa kudhibitisha baadhi ya vitu.Nikaamua nitaifanya ila kuna vitu nilitaka anieleweshe ili nisikosee.Siku ya nne,ambapo alisema ni kila Alhamis anapita mtaani kwetu sikwenda kazini kwa lengo la kumsubiri rafiki yangu muokota machupa ila hakutokea,kesho na keshokutwa yake pia hakutokea.Nikamtuma dada aulize kwa majirani kama wanamuonaga wakasema hawajamuona.
Siku miezi ikapita ila mpaka ninaandika hapa sijamuona tena kaka yangu kipenzi ila baada ya muda nikajiongeza nikajaribu na leo naongelea 300 mara mia kadhaa kwa siku.
Natamani sana kujua kuwa yule malaika wangu na yeye anafanya ndo mana hapiti kuokota chupa na sio ugonjwa ulimzidi akafariki 😭😭.
Yule ndugu yangu sikumwambia biashara aliyonifundisha yule bwana,inshort ni zaidi ya mwaka sasa ninafanya hiyo kitu na sijamwambia mtu yeyote na sina mpango wa kumwambia mtu yeyote labda nikijua ninakufa leo ndio na mimi nitatafuta nimpendae nimwambie na kama huyo bwana alikufa basi dunia nzima anayefanya hicho kitu ni mimi peke yangu.
Lengo la kuandika huu uzi ni
1)Nko bored na nikiwa bored napenda kuandika.
2)Naamini hiki kisa kitakufunza vitu.
3)Nataka kukuambia kuwa Mungu yupo.
4)Nataka kukuambia dharau haijawahi kuwa na faida.Kuna saa nahisi yule mtu alitumwa kuleta hizi mia tatu mia tatu kwa huyu ndugu yangu ila dharau zake zikamkosesha neema.