Hello
Mimi natuma bidhaa kwa bei ya jumla kutoka China. Huku ninasoma!
1. Guangzhou ndio mji unaopatikana kila kitu!!!
ILA kama unahitaji large quantities fuatilia viwanda vinavyojihusisha na bidhaa unayohitaji!
SHENZHEN pia ni mji ambao upo Guangdong, mkoa (province) moja na Guangzhou! Huu mji una electronics za kila aina kwa bei ya jumla!
FOSHAN utapata furniture aina zote unazotaka!!! Mashuka, mapazia!
2. Maradhi, unawaza kuumwa mkuu?? Sasa issue ya hospitals huku ni bei ghali, kwangu lakini! ILA sio kizuizi kikubwa! Labda kama unakuja kwa ajili ya matibabu.
Au unamaanisha MALAZI???
Hotels ni kwanzia 100-200RMB INATEGEMEA NA MSIMU! Msimu wa CANTON FAIR HUWA ZINAPANDA HASWA!
3. USAFIRISHWAJI WA BIDHAA
HUWA NINATUMIA SHIPPING LOGISITICS ZA WACHINA! Sio wazinguaji kama wabongo!
Silent Ocean mzigo ukipotea wananata sana! Na hukaa mpaka Miezi minne bandarini!!!
Mohka ndio wamekuwa wadananda, issues za usafiri ni kuwa makini sana!