Nahitaji kujua historia ya Bagamoyo

Abu_yazid

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2014
Posts
3,435
Reaction score
4,245
Wanajamvi nahitaji msaada wa kufahamu historia ya mji wa Bagamoyo kaburi la Sharifa, kaburi la wapendanao, kaburi la Ally bwana Juma, kisima cha ajabu, msikiti wa Bagamoyo, jengo la makumbusho na historia ya mamba wa Bagamoyo kiundani zaidi.

Nitashukuru mkinisaidia wanajamvi.
 
Kwani wewe uko wapi? Kama upo Dar ni lisaa limoja tu kwa daladala.
 
hapo Bagamoyo waliweza kuhifadhi historia ni kule kanisa katoliki msalabani wamepangilia mambo ambayo yanaakisi ulichojifunza kule kaole kuna wasanii tu wanaropoka ukiwauliza maswali ya msingi hawana majibu toshelezi
 
Nenda katembelee huko kaole utayapata yote hayo kwa undani.
 
Mbona kama ni kitu unachokifamu vilivyo?
Ooh nimeshapa jibu karibu sana jamvini
 

NITAKUSAIDIA.
Baada ya mimi na wanafunzi wangu kwenda Bagamoyo tar30Aug.2014 nilijifunza haya;
1.KABURI LA MAIFU
=>Ieleweke kuwa lile si kaburi la Shariff bali la Maiff(mwanamke mwenye karama kama Shariff)
*nisamehewe ikiwa nimekosea jina Maiff*

=>Mjini Kaole(1200s) maji yote yalikuwa ya chumvi.
Watu walisumbuka kuchimba visima na kote walipata maji chumvi.

Msichana huyo alifanya dua,
akapewa maono na kuwaambia watu,
"Kwa uwezo wa Allah chimbeni hapa na hakika yatatoka maji matamu"

Kweli yalitoka maji safi,
wakajenga msikiti kando yake na vyote vipo hata leo.

¡èMaji kisimani hayapungui hata mchoteje,
hayaongezeki hata mvua inyeshe vipi¡è

=>Inaaminiwa watu wakiingia mle kaburin wakaomba hufanikiwa
 

2.KABURI LA WAPENDANAO
Inasimuliwa hivi;
..Wapendanao fulani,mume na mke walipatwa na dhoruba baharini.
=>Walipojua hawatasalimika waliamua kujifunga kamba pamoja ili wakifa maji,mizoga yao iokotwe pamoja ufuoni.

=>Maskini! Kweli walipokufa kwa maji,
mizoga yao iliokotwa pwani ya jiji la kale la Kaole.

=>Majina yao yameandikwa kwenye bamba la kuta za kaburi lao kubwa hata leo.
 
Kaburi la Shariff-1200s
(karne ya 13) lililo katika masalia ya mji wa kale wa Kaole.

Mita chache kutoka lilipo kaburi hili kuna KISIMA CHA MAAJABU
(Chadaiwa ni cha Shariff-mke);
=>Kina maji matamu, yasiyo na chumvi licha ya kuwa kando ya bahari.
=>Maji hayapungui hata mchote vipi!
=>hayaongezeki hata mvua inyeshe vipi!
 
Sio kaburi LA maiff ni "sharifa"
 
HISTORIA YA MJI WA BAGAMOYO.

Bagamoyo ni jina kubwa sana hapa Tanzania kutokana na kujipatia umaarufu wake kufuatia vitu mbalimbali vilivyopo wilayani humo.

Mji huu wa bagamoyo upo mkoani pwani,iko kati miji ya kale na ya kihistoria kabisa ya waswahili katika nchi ya Tanzania,na ipo mwambao wa Bahari ya Hindi.

Katika mji huu kuna makumbusho mbalimbali ya kale kama maghofu,misikiti,minyororo ya kufungia watumwa,mbuyu mkubwa kuliko yote na kisima cha maji yanayotumika kunywa kuoga na kazi nyingine.

Wakazi wengi katika mji huo wa bagamoyo ni makabila mchanganyiko ya kibantu,kabila kubwa ni Wazaramo,lakini kuna makabila mengine kama wakwere,wazigua,na wadowe wote wakiishi katika mji huo ambao una vivutio vingi sana na vya kupendeza.

MAANA YA JINA BAGAMOYO.

Jina hili la bagamoyo lina maana kuwa hapo zamani lilikuwa linaitwa"Bwagamoyo" kutokana na hapo zamani kulikuwa na biashara ya utumwa kule Zanzibar ikifanywa na masultani kutoka Maskati Oman,ambapo watumwa walipokuwa wanaletwa bwagamoyo kwa ajili ya kusafirishwa kwenda zanzibar lazima wapumzike wakifika bwagamoyo,wanafurahi,wanacheza,wanakula na ndipo likaja jina la bwagamoyo wako na sio bagamoyo kama linavyoitwa sasa hivi.
 
NYIE ANDIKE KUHUSU HISTORI ZA MIJI YOOOOTE, SAWA. LAKINI UTATA UPO KTK JINA LA "DSM" LILIVYOPATIKANA. PATAMU HAPO
 
Kanungila...
Mimi nitagusa hapo kwenye "utumwa kule Zanzibar ikifanywa na masultani kutoka Maskati Oman."

Soma historia ya utumwa ndiyo utakuwa katika hali ya kuelewa somo hili vyema.

Nakushauri uanze na "Transatlantic Slave Trade."
 
Kanungila...
Mimi nitagusa hapo kwenye "utumwa kule Zanzibar ikifanywa na masultani kutoka Maskati Oman."

Soma historia ya utumwa ndiyo utakuwa katika hali ya kuelewa somo hili vyema.

Nakushauri uanze na "Transatlantic Slave Trade."
Naaaam
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…