Nahitaji kusafirisha gari kutoka Dar kwenda Mwanza kwa kulipia kwenye magari makubwa

Ndiyo, nilitamani hivyo kabisa kama unavyosema wewe hapa, kwamba kama train ya SGR inatoka hapa Dar saa 12 asubuhi, halafu saa 7 iko Mwanza, mimi naondoka nayo na gari langu likiwa limepakiwa nyuma ya train hiyo. Nikifika Mwanza nashushiwa gari langu huyo nasepa kwenda kijijini kula samaki na kunywa maziwa.

Unajua watu tuliozakiwa kijijini ni walafi sana kwenye samaki na maziwa. Maziwa tunayokunywa si haya ya kwenye pakiti, na samaki tunaokula si hawa waliokaa kwenye freezer. Tunakula samaki aliyetoka majini, si zaidi ya masaa mawili yaliyopita, na maziwa ambayo hayajawahi kupitia kiwandani. Tuna shida sana!
 
Kabla ya 2022!
Unaota. [emoji1787][emoji1787][emoji1787] Dodoma yenyewe kwa mbinde. Kufika Mwanza labda phase ya 5
Huo mradi unahitaji pesa mingi sana. Na serikali iko na mambo mengi.

Anyway lets seee

Au mnasemaje mods
 
Unaota. [emoji1787][emoji1787][emoji1787] Dodoma yenyewe kwa mbinde. Kufika Mwanza labda phase ya 5
Huo mradi unahitaji pesa mingi sana. Na serikali iko na mambo mengi.

Anyway lets seee

Au mnasemaje mods
Ikishindikana kuisha hadi kufikia kipindi hicho, mimi nitajua ni kutokana na interception ya ugonjwa huu wa Corona
 
Kalisafirishe kwa treni very cheap nenda TRL watakupa utaratibu
 
We jamaa umekomaa na hilo gari kama jeneza? [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Au umebeba uchawi humo?

Kama bovu tengeneza Dar. Likipona test yake ni kutembea hadi mwanza

Au mnasemaje mods
Akishalitengeneza akienda pale rombo anakula vichwa vyake vitatu burudani kabisa mpaka Mwanza
 
Nahitaji kulipakia na si kuendesha. Soma maelekezo vizur, na sio kwamba option ya kuendesha siijui.
Kuna kampuni inaitwa kung fu,wanafanya hizo kazi za kusafirisha magari kwa kuyapakia kwenye magari yao,wapo very professional ila ni gharama sana
 
Hata ikiwa laki 3 unalipa tu, ni risk sana kuendesha gari toka dar to Mwanza
 
Hata ikiwa laki 3 unalipa tu, ni risk sana kuendesha gari toka dar to Mwanza
Ni kweli kabisa, achilia mbali gharama. Ila hii Serikali ina jicho kubwa sana la kuona opportunities, pamoja na kwamba Serikali huwa hazifanyi biashara. Hii kitu wanaweza wakaifanyia kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…