Nahitaji kuwekeza Tsh. Milioni 170

Nahitaji kuwekeza Tsh. Milioni 170

Za jioni wadau,

Naomba mchango wa mawazo yenu, nikiwa na milioni 170 za kitanzania naweza wekeza wapi pesa hii nikapata rejesho lenye tija?

Kwangu mimi rejesho lenye tija ni angalau milioni 2 kwa mwezi.

Natanguliza shukrani.

Njoo PM
 
Njoo Arusha, ufuge kukuku wa mayai
Kipindi hiki cha baridi mayai hadimu sana

Mimi next year Nina mpango wa kukopa million 400 CRDB niwekeze kwenye kuku wa mayai

Tatizo watu hawana mitaji tu
Nikipata kampuni za kichina nitajenga poultry farm ya kisasa kabisa
Jichanganye tu ila take it from mfugaji mkubwa wa kuku wa layers, hakuna investment pasua kichwa kama hio. Utakuja kutusimulia tu.
 
Za jioni wadau,

Naomba mchango wa mawazo yenu, nikiwa na milioni 170 za kitanzania naweza wekeza wapi pesa hii nikapata rejesho lenye tija?

Kwangu mimi rejesho lenye tija ni angalau milioni 2 kwa mwezi.

Natanguliza shukrani.

Duuuh uweke 170m faida 2m kwa mwezi? Inatakiwa upate atleast 5m net profit.
 
Njoo nikupe ramani ukafungue kituo cha radio ndani ya miezi mine hiyo pesa inarudi na faida na kituo tunakiuza tunapiga tena pesa tunaangalia ustarabu mpya
Àsije akafuata huu ushauri wako. Kituo cha redio ni biashara ngumu sana kwa sasa. Vituo vingi hata mishahara wanalipa kwa mbinde. Huu ushauri wako haufai kwa sasa
 
Za jioni wadau,

Naomba mchango wa mawazo yenu, nikiwa na milioni 170 za kitanzania naweza wekeza wapi pesa hii nikapata rejesho lenye tija?

Kwangu mimi rejesho lenye tija ni angalau milioni 2 kwa mwezi.

Natanguliza shukrani.

Kama uko interested nipigie 0714 122 011
Nikupe mpango wa Jenga uza,
Utapiga mchele wa kutosha,
Biashara ambayo haina hasara kabisa,
Kama faida inaweza kuwa milioni 3 mpaka 4 kwa mwezi kuanzia tunaanza kujenga mpaka tunaiuza,
Piga simu
 
Kwahyo kwa pesa yako hiyo tunaweza kujenga nyumba mbili kali sana tukauza na kuziuza ndani ya miezi minne tushajenga nyumba mbili na kuziuza tayari(miezi miwili na nusu ujenzi mwezi mmoja na nusu kuuza)
Nyumba moja labda tunajenga kwa milioni 80 yaani kununua kiwanja na kujenga kilakitu tunakuja kuuza milioni 100 kwahyo unafaida ya milioni 20 kwa nyumba moja,
Kwa nyumba mbili unafaida ya milioni 40 kwa mtaji wa milioni 160,
Kumbuka nyumba hizi tumejenga zote na kuuza ndani ya miezi minne tuu,
Kwahyo ndani ya miezi minne tayari unafaida ya milioni 40 inamaana kwa mwezi unakuwa umetengeneza kama milioni 10 kwa mtaji wa milioni 160,
Kwa mwaka kutengeneza faida ya milioni 100 ni kawaida tuu,
Kumbuka mtaji wako unakua kwahyo kwa mwaka unaofata utatengeneza faida ya zaidi ya milioni 200 mwaka unaofata tena ni milioni 400 na kuendelea,
Aliekuwa serious apige simu tufanye kazi
Njoo tufanye kazi Boss [emoji3513] +255 714 122 011
 
Kwahyo kwa pesa yako hiyo tunaweza kujenga nyumba mbili kali sana tukauza na kuziuza ndani ya miezi minne tushajenga nyumba mbili na kuziuza tayari(miezi miwili na nusu ujenzi mwezi mmoja na nusu kuuza)
Nyumba moja labda tunajenga kwa milioni 80 yaani kununua kiwanja na kujenga kilakitu tunakuja kuuza milioni 100 kwahyo unafaida ya milioni 20 kwa nyumba moja,
Kwa nyumba mbili unafaida ya milioni 40 kwa mtaji wa milioni 160,
Kumbuka nyumba hizi tumejenga zote na kuuza ndani ya miezi minne tuu,
Kwahyo ndani ya miezi minne tayari unafaida ya milioni 40 inamaana kwa mwezi unakuwa umetengeneza kama milioni 10 kwa mtaji wa milioni 160,
Kwa mwaka kutengeneza faida ya milioni 100 ni kawaida tuu,
Kumbuka mtaji wako unakua kwahyo kwa mwaka unaofata utatengeneza faida ya zaidi ya milioni 200 mwaka unaofata tena ni milioni 400 na kuendelea,
Aliekuwa serious apige simu tufanye kazi
Njoo tufanye kazi Boss [emoji3513] +255 714 122 011
Kwanini usimwache afanye mwenyewe na watu wake? Wewe endelea kujenga hizo zako. Tunashukuru kwa wazo
 
Mpe mchina akupe yutong moja Kwa mkopo utammlazia kisha uwe konda utalaza kila siku laki 7 faida
 
Za jioni wadau,

Naomba mchango wa mawazo yenu, nikiwa na milioni 170 za kitanzania naweza wekeza wapi pesa hii nikapata rejesho lenye tija?

Kwangu mimi rejesho lenye tija ni angalau milioni 2 kwa mwezi.

Natanguliza shukrani.
Yaani 170m unataka rejesho la 2m/month? Hauko serious
 
hivi kwanini sasa hivi kila mtu anawaza kuwekeza UTT na BOT , ina maana mazingira ya kufanya biashara Tanzania yamekuwa magumu sana au purchasing power ya raia imepungua sana? Yani hakuna anayewaza ata kuhusu fursa za export
Mutual funds na hizi Bonds za serikali sio biashara ni investment. Zipo miaka na miaka nashangaa unasema eti Sasa hivi watu wanakimbilia huko kuwekeza wakati watu wanaweka huko billions and billions miaka na miaka.

Sema Sasa hivi Kwa sababu ya internet taarifa zinatembea inaonekana watu wanakimbilia which is wrong!

Uingereza wana Hadi bonds za miaka 100. Wakati Tanzania Government Bond ya miaka mingi ni ya miaka 25 Tena imeanza majuzi.

Biashara ni taaluma kama zilivyo taaluma zingine. Si Kila mtu anaweza biashara.

Mtu kama samata anastaafu Soka na bilion kadhaa halafu Hela yake aje kufanya biashara za nguo si ataishia kufilisika asipokuwa na taarifa nzuri. Best way ni kuweka Hela zake sehemu salama.

Unazungumzia kuhusu export. Ni kweli ila unajua compliance za bara la ulaya unapotaka kumpeleka hata asali. Kuanzia aina ya asali na packaging yake? Fuatilia uone.
 
Njoo nikupe ramani ukafungue kituo cha radio ndani ya miezi mine hiyo pesa inarudi na faida na kituo tunakiuza tunapiga tena pesa tunaangalia ustarabu mpya
Frequency anapata wapi wakati zishajaa zote?
 
Sijajua upo wapi ila ingekuwa kwa upande wangu wazo la kwanza lingekua ni MICROFINANCE. Kwa mtaji huo ukiuwekeza kwene microfinance ukiwa na usimamizi mzuri, software ya uchakataji wa taarifa, ufuatiliaji mzuri kwa wateja kuanzia kabla ya kukopa na baada ya kukopa basi Una possible ya kudouble hio pesa mara mbili kwa mwaka maana ukiwekeza million 150 una uhakika wa profit ya 10 million kila mwezi kama faida baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji kama mishahara na kadharika.

Lakini wazo la pili ni ununuzi wa mazao hasa maharage, harage halijawahi kukata kama mimahindi, unaweza ukawa na vyumba vyako hapo hom au ukakodi sehemu, kipindi hiki ni cha mavuno ukachukua million 100 ukanunua maharage na million 50 ukanunua mpunga by mwezi wa 12 bei hupanda sana na utatengeneza faida kwa zaidi ya 35% ya pesa yako.

Wazo la tatu fedha hio fanya passive investment UTT japo return yake ni ndogo but atleast ni safe na security ya kutosha, utakua huna hofu na mtaji wako pamoja na faida.

Kama utashindwa sana basi fungua duka kubwa au kampuni itakayo deal sana na masuala ya angribusiness kama uuzaji wa mbolea, madawa ya kilimo, vifaa vya kilimo cha kisasa na makorokoro mengi yanayohusika na kilimo na mnyororo wa uongezaji thamani wa mazao ya shambani.
Upo vizuri sana! Je unaweza kuwa mtaalamu wa maswala ya kuandaa bussiness plan?
 
Back
Top Bottom