Nahitaji kwenda Zanzibar kupiga mishe za vibarua

Shukrani sana mkuu, kwa hiyo hapo Mwemberadu ama Kariakoo ndio kuna njia kuelekea huko kwenye mishe za vibarua? Vipi nauli kutoka Dsm mpaka zenji, vipi una ufahamu kuhusu hicho kisiwa? Kuna mambo ya msingi nahitaji kuuliza
Ipo hivi, ukitoka huko kijijini kwenu hadi Dar, panda basi la usiku ili ufike Dasalamu pale Magufuri Bus Terminal asubuhi, kisha panda mabasi hapa Dar tunaita (mwendokasi) japo siku hizi siyo mwendokasi tena, hadi kituo cha (nadhani Azania au posta, nauli ya hilo basi ni 750/-.

Ukishuka hapo muulize muhudumu wa kituoni ukiwa unatoka akuonyeshe ofisi za Kilimanjaro Fast Ferries au Zan Fast Feries -Mwendokasi ya majini.

Pale unakata tiketi kwa kitambulisho ndg Mtanganyika, kisha utafuata utaratibu hadi unaingia chomboni.

Ukifika nchini Zanzibar au kisiwa cha Unguja, utashuka na kukaguliwa utambulisho wako kisha utaibukia barabarani kukutana na boda, tax, bike na waongozaji local kwa wageni kukupeleka unapotaka.

Kule mtu anakupeleka hadi unapotaka hata usipomlipa but kwa utu mpe hata 2000/-.

Sehemu za kulala Unguja; hapa usije dhania ni sawa na hapa Tanganyika asee kule guest ni za kutafuta sana na room ya bei ya chini kabisa ni 25,000 ambapo ukiona hicho chumba ni sawa na room ya elf8 au 10 hapa T/nyika.

Usafiri na Chakula: Usafiri nauli madhani kwa sasa zimepanda but route fupi ni 500 na route ndefu kama kutoka mjini kwenda shamba huko ni 1,400/- hiyo ndo nauli kubwa.

Chakula; asee jiandae kula chips kuku paja nono, supu kwa boflo, juice kwa andazi au ukikosa sana ulojo hivi ndiyo vyakula common sana kule.

Ukitaka sembe au walikwa muda wa mchana inabidi uulize kwenye vijiwe (siyo maskani) kwa eneo utakalokuwepo sababu mama lishe siyo wengi ni wa kutafuta sana, labda jioni pale darajani.

Ila kwa eneo unalotaka kwenda huko site ni full ugali, wali kwa samaki au nyama ng'ombe, sababu wamama kutoka bara wanapiga kazi hasa kupika.

Swali ...
 
Mkuu unamaanisha umbali mrefu zaidi toka unguja center mpaka huko pemben kabisa ni 1400? Basi zenji ni kaeneo kadogo sana
 
Mkuu unamaanisha umbali mrefu zaidi toka unguja center mpaka huko pemben kabisa ni 1400? Basi zenji ni kaeneo kadogo sana
Sio 1400,mfano kutoka stone town mpaka kizimkazi shamba huko ni tsh 3000 kwa coaster au zile canter(mbavu za mbwa?,mjini mpaka paje na michamvi bei ni hiyohiyo.
 
Zanzibar kazi za ujenzi zipo nyingi sana kwasababu uwekezaji mkubwa ni hoteli za kitalii,ila ukibahatika kupata vibarua ktk kampuni za wazungu angalau huwa wanawalipa tsh 15000 na fundi tsh elfu 20 hadi 25,ila ukiangukia ktk kampuni za wahindi hao pesa zao ndogo vibarua wanawalipa elfu 12 kwa siku,Sasa kwa maisha ya Zanzibar hiyo pesa usipoangalia kila wiki utakuwa una save elfu 30 au 40 kama hauna familia.
 
Sio 1400,mfano kutoka stone town mpaka kizimkazi shamba huko ni tsh 3000 kwa coaster au zile canter(mbavu za mbwa?,mjini mpaka paje na michamvi bei ni hiyohiyo.

Sio 1400,mfano kutoka stone town mpaka kizimkazi shamba huko ni tsh 3000 kwa coaster au zile canter(mbavu za mbwa?,mjini mpaka paje na michamvi bei ni hiyohiyo.
Basi hapo unguja ni padogo sana ila wamejitahidi sana kutangaza utalii,hongera zao.
 
Shukrani kwa maelezo mazuri, huko Jambiani, Paje na Michamvi vibarua ni uhakika?
 
Mkuu we upo zenji? Kuna mdau kaniambia kule kuhusu kula na kulala ni hapo hapo kambini, yaani mwenye kazi anatoa hizo huduma.
 
Mkuu we upo zenji? Kuna mdau kaniambia kule kuhusu kula na kulala ni hapo hapo kambini, yaani mwenye kazi anatoa hizo huduma.
Kulala camp huwa zipo ila kuhusu kula hakuna kampuni itakulisha hiyo ni gharama zako
 
Nenda site Moja IPO michamvi kabla hujafika michamvi mwisho Kuna site Moja Inaitwa Kwa Mama Samia inajengwa kampuni ni Mohamed builders pale 12,000 Kwa siku Kama ni kibarua pesa wanatoa Kwa wiki Mara Moja ila uwe mtu wa kazi kweli maana hawataki wazanzibar au watu wa pwani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…