Nahitaji mawazo yenu kwenye hili suala

Bavaria

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2011
Posts
53,092
Reaction score
53,496
Kuna gari imepaki nyumbani muda mrefu hivi kama miezi miwili bila kuguswa likiwa na mafuta kidogo sana.

Leo nikasema ngoja nijaribu kuliwasha nikapige nalo misele. Nikazungusha funguo mpaka pale kwenye on bila kupiga starter halafu nikawasha na AC.

Baada ya kama dk 10 hivi nikaona dashboard inafifia kama battery inaisha na AC ikazima.

Nikajaribu kupiga starter halikuwaka tena.

Hapo kunaweza kukawa na shida gani?
 
Hiyo betri kama nayo imelala kwenye gari miezi 2, itakuwa imeshaisha chaji au imekufa kabisa..

Jaribu kuwasha kwa kutumia betri nyingine ambayo una uhakika inawasha magari mengine..

Hii ikigoma, mwite fundi Maiko afanye yake..[emoji41][emoji41][emoji41]
 
Nimehisi kitu kama hiki, kwamba battery imekufa, nikasema niulize nipate uhakika.

Shukrani mdau.
 
Gari aina gani mkuu,ilitakiwa upiga starter kwanza ndipo uwashe ac,umelitesa battery bure,
Fungua bonet angalia terminal kama zimekaza na carbon kama ipo itoe kwa coka au peps
 
Gari aina gani mkuu,ilitakiwa upiga starter kwanza ndipo uwashe ac,umelitesa battery bure,
Fungua bonet angalia terminal kama zimekaza na carbon kama ipo itoe kwa coka au peps
Toyota Harrier.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…