Nahitaji mkopo sh: 6m kwa ajili ya kufuga kuku wa kienyeji

mannu

Member
Joined
Jun 6, 2013
Posts
36
Reaction score
5
Habari zenu wanajmiiforum pole na pilika za maisha mimi niko Dar nina shamba la heka mbili chanika ninaomba mnishauri ni wapi naweza kupata mkopo wa sh 6m kwa ajili ya kufuga kuku wa kienyeji kwa kutumia hati yangu ya kiwanja ya kijiji nitaweza kulipa kwa muda wa miaka mitatu pamoja na riba.Naomba mwenye kunisaidia mawazo tutakuwa pamoja na yeye sitapuuza mawazo ya mtu,niwatakie afya njema katika maisha yenu karibu kwa mawazo yenu
 
mkuu hati ya kiwanja ya kijiji?! hapo naomba ufafanuz kidogo maana hiz hati zinaleta shida sana
 
hati ya kijiji yenye mhuri wa m/kiti wa kijiji na mtendaji wa kijiji na mashahidi naomba mkubwa unisaidie hata kama ni milion tatu ndani ya mwaka moja naweza kurudisha pamoja na riba
 
Hilo shamba ni kubwa sana kamanda kwani laweza kuwa na value C chini ya 100M kama liko mahala pazuri dar, jitahidi utumie hata TShs 500,000?= hupata hati ya shamba, then nenda benki yeyote hapa Tz hasa za wazawa uweke shamba lako kama collateral/ security (dhamana). Ila naomba usidanganyike kuuza shamba kwa sasa, acha ligain more value. Kuwa makini na matapeli ya humu jamiiforums na kwingine kote kuhusu msaada au kununua eneo lako kwani binadamu wasasa sijui ni kizazi gani hiki wajaameni!!! Bwana Yesu asifiwe.
 
Jaribu kutembelea bank yoyote uwape maelezo nao watakupa mwongozo kama inawezekana au haiwezekani na taratibu gani ufuate.
 
Tafuta mtu anaefuga kuku akupe uhalisia wa biashara kabla hujakopa,mkopo ucje ukukakupa dhiki zaidi badala ya nafuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…