Nahitaji mkopo wa biashara au mzigo wa nafaka

Nahitaji mkopo wa biashara au mzigo wa nafaka

Mimi ni kijana wa kitanzania, umri miaka 28... nina duka la kuuza nafaka kwa reja reja hapa manzese karibu kabisa na kituo cha mwendokasi njia ya kwenda mburahati. Ni eneo zuri kibiashara, lina watu wengi hususani mama ntilie.

Duka lina document zote muhimu kama TIN,LESENI YA BIASHARA na risiti za ushuru mwingine kama service levy n.k.

Lengo ni kuomba mkopo wa kukuza biashara yangu ili kuendana na kasi ya ukuaji na uhitaji wa huduma. Mkopo wangu naomba katika mifumo ifuatayo

1. Pesa taslimu... hii itaniwezesha kununua nafaka kulingana na uhitaji

2. Mzigo /nafaka... hii ni kupewa nafaka kama mchele, mahindi,maharagwe n.k. Kwa wenye mizigo stoo wanaweza kunikopesha/ kuleta nikauza kwa makubaliano tutakayoafikiana.

Ndoto ni kubwa sana ila mtaji ni changamoto, naombeni msaada.

NB: kama una mzigo au biashara ya nafaka tunaweza kuongea ukatumia fremu yangu kwa makubaliano maalumu pia.
mm na mchele ila nipo morogoro embu nicheki tuone tunafanyaje 0622567625
 
Back
Top Bottom