Kaudunde Kautwange
JF-Expert Member
- Nov 15, 2011
- 1,644
- 1,648
Mkuu kwanza hongera sana kwa hii idea, ni bonge la idea.Kama kichwa cha habari kinavyojielezea nipo njiani kufungua NGO yangu ambayo itakuwa ina deal na maswala ya ELIMU YA TANZANIA
Kazi tutakazokuwa tunafanya ni kama ifuatavyo:
1. Kufundisha mashuleni kwa mfumo wa club
2. Kuandaa matamasha mbali mbali ya kielimu mashuleni
3. Kutoa mafunzo kwa walimu
4. Kupima IQ test completion kwa wanafunzi
5. Kutoa consultant kwa maswala ya kielimu kwa wamiliki wa shule na wakuuu wa shuleni
Karibuni sana hata kama wewe sio mwalimu; karibu tupige kazi kidogo kinachopatikana tutakuwa tunalipana
Pili, kwa wilaya za mjini, waalimu ni wengi kiasi, hivyo suala la ukosefu wa waalimu bado haujawa changamoto sana, ukizingatia na uwepo wa tuition centers.
Ushauri:
Fungua NGO wewe kama wewe, fuata zile taratibu zote za kuwa na waanzishiri, board member n.k
Ukishafungua, mobilize hata waalimu 10 tu wa kada za Sayansi, kisha chagueni wilaya za mikoani ambazo zina uhaba wa waalimu.
Nendeni kwa DED au Mkuu wa wilaya au Mkuu wa Mkoa, mwelezeni hiyo idea, na mumpe strategies za ku boost matokea kwenye shule ambazo zina matokeo mabovu kwenye kada ya sayansi.
Mwambieni, mtakuwa mnajitolea, lakini kuwe na uhakika wa kuwa na mfuko wa maendeleo ya elimu ambao wazazi watashirikishwa in a positive way
Baada ya hapo, anzeni kutafuta sponsor kwa kile ambacho mnakifanya.. chagueni zile shule ambazo waalimu wengine wanaziona kama ni changamoto
Hakikisheni mnakuwa na clear visibility plan, hii itasaidia sana hata wadau wa elimu waliopo nchi zingine wanaweza kuwasaidia
Naomba niishie hapo!!!