Nahreel,, kama huwezi sema bhana..Unashindwa kuwasimamia wasanii wako

Nahreel,, kama huwezi sema bhana..Unashindwa kuwasimamia wasanii wako

Antennah

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2015
Posts
6,754
Reaction score
8,750
Leo ngoja niwe muwazi kabisaaa..
Nahreel wewe ni moja ya maproducer classic na wenye vipaji vikubwa sana hapa bongo.
Tangu nilipoanza kuskia midundo yako kipindi unampigia joh makin miaka hiyo nilitambua wazi kwamba we ni kichwaaa........,,,

Sasa leo naomba nitoe dukuduku langu la moyoni kwako......ni ukweli lakini nimchungu pia. Biashara ya kuendesha au kumanage lebel ya The industry INAKUSHINDA kama siyo tayar IMEKUSHINDA.

get-it-on-640x640.jpeg


Unakila kitu cha kufanya msanii akiwa hapo ajihisi yupo kwenye mikono salama kwa kuendeleza talent yake,,,(studio, brain, and exposure). na nikili wazi hata ngoma zinazotoka hapo hasa za wasanii wako kama rosa lee, wew mwenyewe as navy kenzo na wildad ni kubwa sana kwenye maskio yetu.

Ila kusema ukweli kaka kuwamanage wasanii wako umeshindwa au niseme unashindwa kabisa yani......rosa lee ni female rapper mkubwa sana africa lakini juhudi yako as a manager ni ndogo sana kwa huyu dada...mpka inafkia time inaonesha anatumia nguvu ya ziada yeye kama yeye kuandika na kuflow in amayzing way ili tu atleast ajibrand yeye kama yeye......!!!

Kwenye swala la kupromote wasanii wako nakupa sufuri.
Kwenye swala la kucheza na interval ya mda wa kutoa ngoma kwa wasanii wako nakupa (-1) Kwenye swala la kujua kumanage na kucontrol lebel kunahitaji basics zipi..nakupa 1% out of 100%

huyo wildad ni msanii mzuri sana lkn umemchomesha mahindi weeee mpka ameanza kusaulika.....sijui upo bize na show za nje!!!???
Rosa lee nae unamtolea magoma lkn poor poor poor promotion kabisa wakati dada watu ni mkali na ngoma zake ni kali kinomaa...!!!!

Kuna hako kadada kengine kanaitwa "ibe ibe" naskia soon utakasainisha mkataba....kanaimba vizur yan very talented lakn ndo hivo tena. Na nakuhakikishia.....ukitaka kuona rosa lee na wildad sio wasanii wakawaida......hebu wakabizishe kwa manager mwenye utashi ndo utaelewa nini namaanisha.

ILA WEWE HIYO KAZI IMEKUSHINDA......SIONI EFFECT YOYOTE KUBWA YA LEBEL YAKO KWENYE GAME.....REGARDLESS OF ALL THINGS THAT YOU HAVE.

Ushauri wangu.
Just be there as an artist wa navy kenzo na pia kama producer wa kazi zote za hapo "the industry"

Then tafuta watu special wenye utashi na maarifa na ujuzi wa hali ya juu waweze kumanage hao artist wako, Including promotets.
Huwezi kufanya vitu vitatu kwa wakat mmoja.
 
Uyu She ni mkali ila apunge zile "Muzfuc*¥ker" zake atafika mbali.....!

Nkirudi kwenya Mada jamaa anajitaidi sana kufanya kazi yake nafikiri pia haikua kazi ndogo kwa mimi na wewe kuwafahamu Wildad na Rosalee.....

Jamaa naona anatarget zaidi soko la Afrika, classic music wanaoufanya kibongo bongo wengi awauelewi ata hivyo bado naina Theindustry kuja kua lebel kubwa Africa.......!
 
Hata hao navy kenzo wenyewe wanapumulia mashine,
tangu Kamatia chini itoke, sijaona usiriasi wa kazi zilizofuata...
Nah real abadilishe maproducer huenda akafika mbali
 
Huwez kua promoter and producer at same time,..
.naheel ajitafakari

Kweli kabisa,anatakiwa atengeneze timu itakayomsaidia kubrand wasanii wake na kubrand studio yake.
Kazi zote hizo hawezi kuzifanya mwenyewe bila ya team hasa wataalam wa soko ka music.
 
Back
Top Bottom