Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Fuatilia yanayojiri kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha Wanasheria Tanganyika 2024 - Dodoma.
Naibu Waziri Mkuu, Dkt. Dotto Biteko akijibu hoja ya Mawakili kukamatwa wanapotekeleza majukumu yao amesema kuwa Serikali imelichukua hili. Amesema kuwa nchi hii inaendeshwa kwa misingi ya sheria hivyo itahikikisha TLS wanapokutana mwakani basi hili lisiwe changamoto ya kusemwa sana. Ameongeza kuwa Mawakili hawa wanakuja kuwatetea watu na kama wanavyoitwa maafisa wa mahakama ni muhimu wakapata heshima yao mahala pa kazi ili waweze kutekeleza majukumu yao kama inavyopaswa.
Naibu Waziri Biteko ameongeza kuwa TLS wanalo jukumu la kuchagua viongozi wataoendeleza mshikamano wa chama hicho, watakaokuwa na kiu na wakati mwingine kuikosoa Serikali, viongozi ambao watakuwa na matamko ya kitaaluma.
Ametoa wito wa TLS kuendelea kuwa na msisitizo wa kuendelea kukaa kwenye taaluma yao kama wanasheria na kuendelea kutekeleza majukumu kwa manufaa ya watanzania.
Dkt. Biteko amesema kuwa wanachama wa TLS wana tofauti mbalimbali kuanzia dini, makabila, ushabiki wa mpira nk lakini wanaunganishwa na kitu kimoja ambacho ni taaluma yao ya Uanasheria
Naibu Waziri Mkuu, Dkt. Dotto Biteko akijibu hoja ya Mawakili kukamatwa wanapotekeleza majukumu yao amesema kuwa Serikali imelichukua hili. Amesema kuwa nchi hii inaendeshwa kwa misingi ya sheria hivyo itahikikisha TLS wanapokutana mwakani basi hili lisiwe changamoto ya kusemwa sana. Ameongeza kuwa Mawakili hawa wanakuja kuwatetea watu na kama wanavyoitwa maafisa wa mahakama ni muhimu wakapata heshima yao mahala pa kazi ili waweze kutekeleza majukumu yao kama inavyopaswa.
Naibu Waziri Biteko ameongeza kuwa TLS wanalo jukumu la kuchagua viongozi wataoendeleza mshikamano wa chama hicho, watakaokuwa na kiu na wakati mwingine kuikosoa Serikali, viongozi ambao watakuwa na matamko ya kitaaluma.
Ametoa wito wa TLS kuendelea kuwa na msisitizo wa kuendelea kukaa kwenye taaluma yao kama wanasheria na kuendelea kutekeleza majukumu kwa manufaa ya watanzania.
Dkt. Biteko amesema kuwa wanachama wa TLS wana tofauti mbalimbali kuanzia dini, makabila, ushabiki wa mpira nk lakini wanaunganishwa na kitu kimoja ambacho ni taaluma yao ya Uanasheria