Naichukia Siku ya Jumatatu

Indoraptor

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2019
Posts
249
Reaction score
506
Niseme tu tangu nikiwa nasoma siku hii haijawahi kuwa pendwa kwangu. Nilidhani nikimalizana na mambo ya shule nitaanza kuifurahia siku hii ya 'jumatatu' lakini mambo yamekuwa ndivyo sivyo.

Ni siku ambayo kila ikifika jumapili jioni naiwaza itaenda kuanzaje.

Ni siku ambayo nawaza naenda kukutana tena na watu wenye maudhi mengi baada ya kuachana nao kwa siku mbili nyuma

Yote haya nadhani yanatokana na kazi za kuajiriwa. Nimepanga kujipa mwaka mmoja wa kukaa kwenye ajira baada ya hapo nijiajiri labda naweza nikaifurahia sikuu hii
 
Wewe endelea kuichukia na sisi tunatumia hiyo chiki yako kama fursa ya kitengeneza pesa mkuu
 
Tatizo umeajiriwa.. Mimi ndio nimeamka sahivi, nataka niende kuwatembelea wafanyakazi wangu, kwenye projects zangu.
 
Hahaha,mabosi wanakuwa na nguvu na ufuatiliaji wa hali ya juu.Wajibika ipasavyo utaipenda bila shida
 
Naipenda Sana jumatatu
 
Uvivu ni adui mkubwa sana kwa maendeleo ya taifa na vijana wenye nguvu kama wewe ambao husingizia majuto uzeeni ambapo hugeuka kuwa mjukuu
 
Kujiajiri ni zaidi ya kuajiriwa kama huipendi now na yenyewe haitokupenda mkuu
 
Hahaha, mwenzio huyu.
Your browser is not able to display this video.
 
Halaf jpli huwahi kuisha balaaa jtatu huwa nzito
 
Mkuu nahisi wewe unaweza kuwa unaipenda kidgo. Kwangu mimi huwa natamani hii siku isingekuwepo kwenye week, Jumatatu ni siku ambayo huwa inaanza mapema sana na inakawia kuisha. Nadhani Jumatatu inakuwaga na masaa mengi zaidi ya siku nyingine zote, na Jumapili huwa na masaa machache kuliko siku nyingine yoyote. I hate Mondays
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…