Naifatilia hii realmotors naona wana Magari mazuri, kuna mtu yoyote alishawahi agiza gari na hii kampuni?

Naifatilia hii realmotors naona wana Magari mazuri, kuna mtu yoyote alishawahi agiza gari na hii kampuni?

Mkuu hongera kwa mchakato huo na hitaji lako la ushauri. Mimi nina uzoefu wa kutosha kuagiza magari kwa kampuni kadhaa.

Ngoja nikupe maoni yangu kuhusu kampuni za magari.

Miongoni mwa kampuni bora ambazo ukiagiza gari una uhakika wa kupata gari nzuri sana ni:

1. Autorec - hawa wana magari mazuri sana ila bei yao ni shida. Sababu ni kuwa kabla hujauziwa gari inafanyiwa reconditioning, nakuhakikishia gari zao ni used ila ni top. Shida ni hapo ktk bei.

2. Trust - Hawa pia wana magari top quality, ni kama autorec na bei zimechangamka kdg.

3. Real Motors - Hawa wanauza gari nzuri sana, kwa maoni yangu, tofauti na autorec na trust wao hawafanyi reconditioning ila wana point gari nzuri tuu. Hivyo bei zao ni cheaper na quality ni nzuri. Kwa kawaida hawapendi kuwa na gari zaidi ya km 100,000.

Shida yao ni moja tu, customer service sio nzuri yaani hawabembelezi mteja kamwe. Nadhani wanauza magari kwa passion na sio kutafuta pesa.

Ushauri: Kati ya kampuni zote hizo kwa kuangalia bajeti ya mtanzania wa kawaida, Real Motors is the best kwa sababu utapata gari nzuri na bei nzuri, hilo la customer care mtavumiliana.
Hii ni SURE THING....!!!! Mimi nimenunua gari kwao mara tatu na sijuti hadi kesho.
 
Back
Top Bottom