Naingia kwenye kufuga kuku chotara (Saso)

Naingia kwenye kufuga kuku chotara (Saso)

Niliwanunua wakiwa wameshapata chanjo zote. Kwa Sasa ni marudio tu ya chanjo ya kideri.

Kuhusu dawa nilipata changamoto ya mafua nikawapa mchanganyiko wa tangawizi, vitunguu swaumu na pilipili. Wakakaa sawa. Baada ya muda ikajirudia Tena nikaamua kutengeza mazingira wawe wanalala juu ya wavu. Huenda nikapunguza maradhi kwa % kadhaa
Vp kuhusu chanjo na madawa ya kuku?..halafu kuhusu chakula hiyo debe moja na nusu ni makadirio ya chini mno. Mimi binafs ni mfugaji wa kuku.

IMG_20220218_191140_160.jpg
 
Baada ya mvua za msimu huu kuwa za kusita na kupoteza mbegu kwa kupanda zaidi ya Mara mbili na kuungua na jua, huku nyanya nazo zikiwa zinachechemea, nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara Aina ya sasso wakati tunaendelea kusubiri neema ya mvua Kama itatuwezesha kuvuna.

Mpango ni kufikisha kuku 1000 na zaidi mpaka mwisho wa mwaka huu 2022.

Kwa Sasa nimeanza na kuku 25 (mitetea 20 na majogoo 5) ambao nimewanunua December 26 wakiwa na miezi miwili.

Malengo makuu ni kusubiri kuku wafike umri wa kutaga kuanzia march 2022 (wakiwa wamefikisha miezi 5) ili nitotoleshe mayai.

Kuku wakianza kutaga nategemea kupata wastani wa mayai 10 kwa siku (kwa uchache) sawa na mayai 100 Kila baada ya siku 10. Hii inamaana Kila baada ya siku 10 nitapeleka mayai 100 kutotolesha.

Baada ya siku 120 ambayo ni wastani wa miezi 4 kuanzia mwezi March sawa na mwezi July 22 nitakuwa nimetotolesha mayai 1200 ambayo kwa wastani nitapata vifaranga 1000 na kidogo (hayo mayai 200) naasume baadhi yatakuwa hayajatotoleshwa au vifaranga watakaoshindwa kuvuka nursery stage.

Kwahiyo mpaka inafika December 2022(insha_Allah) nitakuwa na kuku 1000 ambao ukiachana na parent 25 nilionza nao kutakua na wakubwa wenye miezi 6,5,4(watakua wameanza kutaga) size ya Kati na wadogo kabisa batch ya mwisho miezi miwili.

Baada ya kufikisha idadi hiyo nitaanza kuuza mayai au kutotolesha vifaranga kwa ajili kuuza au kwa ajili kufuga wa nyama.

KUHUSU GHARAMA
Kuku nimenunu 8000 Kila mmoja sawa na 200,000 kwa kuku wote.

Banda lilikuwepo linalowatosha kuku hao 25.

Kwa kuku watarajiwa Banda lao natarajia kuanza kuhangaika nalo baada ya kuku kuanza kutaga. Ambalo nitalijenga kwa awamu nne ( Kila awamu nitakamilisha sehemu ya kuku 300) makisio ya gharama za ufundi kwa Banda la kisasala kuku 1000 na zaidi ambalo nimeandaa eneo la (20x10)m nimepata ni shilling 3.5M kwa materia ya eneo nililokuwepo.

KUHUSU CHAKULA
Kutokana nimewanunua wakiwa wakubwa nimetengeneza mchanganyiko wangu wa chakula ili kupunguza gharama.
Ambapo gharama za debe moja(baada ya kuchanganya) ni chini ya 3000 na kuku wote 25 wanakula debe 1 na nusu kwa mwezi. Na nimeanza mchakato wa kutengeneza funza na hydroponic folders na baadae nitaandaa bwawa la azola.

Baada ya kufikisha kuku 1000 makadirio ya chakula kwa siku ni kilo 130 ambazo ni sawa kwa mchanganyo wangu wa chakula + hydroponic ni 500 kwa kilo.
Sawa na sh 65,000 kwa siku

KUHUSU MATARAJIO YA FAIDA
kwa mwaka huu wote wa 2022 silengi kupata faida, nahitaji mradi ujisogeze na uwe stable. Kwa maana mpaka inafika December 2022 mradi uwe umerudisha gharama zangu japo kwa uchache na uwe inaweza kujiendesha kwa kuuza mayai au kuku.

Baadaya ya mwaka huu nategemea kupata faida Kama ifuatavyo.

1. Kwa kuwa natarajia kwenye kuku 1000 kuwe na mitetea isiyopungua 800 hivyo nategemea kukusanya mayai yasiopungua 510 kwa siku(kwa makadirio ya chini. Sawa na tray 17 kwa siku .

Tray 1ni sawa na tsh10,000 kwa mayai ya chotara (Bei za nilipo) sawa na tsh 170,000 kwa siku

NB: Mradi huu nitausimamia mwenyewe kwa asilimia 100 hivyo hakuta kuwa na gharama za ziada za mfanyakazi.

Hivyo ndivyo nitavyoiishi 2022.
Nakaribisha maoni.
Mkuu hongera kwa uthubutu na kila la kheri katika ufugaji, mrejesho wako kwa kila hatua utakua mchango mzuri kwetu.

Mimi na bro tuliwahi kujaribu kuwafuga 12 tu kama majaribio ilienda poa mayai tuliyala kiasi na wawili wa mwisho walikua wakubwa kiasi kwamba kwenda kumchinja unaogopa atakugeukia[emoji16]...
 
Ndugu yangu samahani naomba unisaidie namba yakoo nahitaji nikuulize kitu kuhusu hii kitu uliyoandika hapa. Ubarikiwe🙏.
Baada ya mvua za msimu huu kuwa za kusita na kupoteza mbegu kwa kupanda zaidi ya Mara mbili na kuungua na jua, huku nyanya nazo zikiwa zinachechemea, nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara Aina ya sasso wakati tunaendelea kusubiri neema ya mvua Kama itatuwezesha kuvuna.

Mpango ni kufikisha kuku 1000 na zaidi mpaka mwisho wa mwaka huu 2022.

Kwa Sasa nimeanza na kuku 25 (mitetea 20 na majogoo 5) ambao nimewanunua December 26 wakiwa na miezi miwili.

Malengo makuu ni kusubiri kuku wafike umri wa kutaga kuanzia march 2022 (wakiwa wamefikisha miezi 5) ili nitotoleshe mayai.

Kuku wakianza kutaga nategemea kupata wastani wa mayai 10 kwa siku (kwa uchache) sawa na mayai 100 Kila baada ya siku 10. Hii inamaana Kila baada ya siku 10 nitapeleka mayai 100 kutotolesha.

Baada ya siku 120 ambayo ni wastani wa miezi 4 kuanzia mwezi March sawa na mwezi July 22 nitakuwa nimetotolesha mayai 1200 ambayo kwa wastani nitapata vifaranga 1000 na kidogo (hayo mayai 200) naasume baadhi yatakuwa hayajatotoleshwa au vifaranga watakaoshindwa kuvuka nursery stage.

Kwahiyo mpaka inafika December 2022(insha_Allah) nitakuwa na kuku 1000 ambao ukiachana na parent 25 nilionza nao kutakua na wakubwa wenye miezi 6,5,4(watakua wameanza kutaga) size ya Kati na wadogo kabisa batch ya mwisho miezi miwili.

Baada ya kufikisha idadi hiyo nitaanza kuuza mayai au kutotolesha vifaranga kwa ajili kuuza au kwa ajili kufuga wa nyama.

KUHUSU GHARAMA
Kuku nimenunu 8000 Kila mmoja sawa na 200,000 kwa kuku wote.

Banda lilikuwepo linalowatosha kuku hao 25.

Kwa kuku watarajiwa Banda lao natarajia kuanza kuhangaika nalo baada ya kuku kuanza kutaga. Ambalo nitalijenga kwa awamu nne ( Kila awamu nitakamilisha sehemu ya kuku 300) makisio ya gharama za ufundi kwa Banda la kisasala kuku 1000 na zaidi ambalo nimeandaa eneo la (20x10)m nimepata ni shilling 3.5M kwa materia ya eneo nililokuwepo.

KUHUSU CHAKULA
Kutokana nimewanunua wakiwa wakubwa nimetengeneza mchanganyiko wangu wa chakula ili kupunguza gharama.
Ambapo gharama za debe moja(baada ya kuchanganya) ni chini ya 3000 na kuku wote 25 wanakula debe 1 na nusu kwa mwezi. Na nimeanza mchakato wa kutengeneza funza na hydroponic folders na baadae nitaandaa bwawa la azola.

Baada ya kufikisha kuku 1000 makadirio ya chakula kwa siku ni kilo 130 ambazo ni sawa kwa mchanganyo wangu wa chakula + hydroponic ni 500 kwa kilo.
Sawa na sh 65,000 kwa siku

KUHUSU MATARAJIO YA FAIDA
kwa mwaka huu wote wa 2022 silengi kupata faida, nahitaji mradi ujisogeze na uwe stable. Kwa maana mpaka inafika December 2022 mradi uwe umerudisha gharama zangu japo kwa uchache na uwe inaweza kujiendesha kwa kuuza mayai au kuku.

Baadaya ya mwaka huu nategemea kupata faida Kama ifuatavyo.

1. Kwa kuwa natarajia kwenye kuku 1000 kuwe na mitetea isiyopungua 800 hivyo nategemea kukusanya mayai yasiopungua 510 kwa siku(kwa makadirio ya chini. Sawa na tray 17 kwa siku .

Tray 1ni sawa na tsh10,000 kwa mayai ya chotara (Bei za nilipo) sawa na tsh 170,000 kwa siku

NB: Mradi huu nitausimamia mwenyewe kwa asilimia 100 hivyo hakuta kuwa na gharama za ziada za mfanyakazi.

Hivyo ndivyo nitavyoiishi 2022.
Nakaribisha maoni.
 
Hili nitalizingatia. Majogoo yatayoonekana afya yake hainishawishi nitayafanya kitowewo
[emoji23][emoji23][emoji23]acha kuyafanya kitoweo mkuu bora ubadilishane na mtu anayeuza kuliko kula sababu kila dhaifu utakua unakula

Ni mawazo yangu tu
 
ufugaji wa kuku naupenda ila shida ilikuw inakuja siku ya jmoc na jpili nikimaliza kuwafanyia usafi na kuwapa chakula akili inaniambia chomoa mmoja ujipongeze.

nikaona isiwe tabu nikaweka mfanyakaz hapo ndo nikaharibu mradi kabsaaaa,dogo anaenda kuuza kuku anapata hela yuleee kwa mademu badae analeta story mara kuku amekufa nimemtupa.

safari hii nimendaa 1m naingia mazima sitaki masiara tena.
 
ufugaji wa kuku naupenda ila shida ilikuw inakuja siku ya jmoc na jpili nikimaliza kuwafanyia usafi na kuwapa chakula akili inaniambia chomoa mmoja ujipongeze.

nikaona isiwe tabu nikaweka mfanyakaz hapo ndo nikaharibu mradi kabsaaaa,dogo anaenda kuuza kuku anapata hela yuleee kwa mademu badae analeta story mara kuku amekufa nimemtupa.

safari hii nimendaa 1m naingia mazima sitaki masiara tena.
Hongera Sana kingkongtz Nami ntakutengenezea sehemu ya kuzalisha hydroponic fodder. Zinapungiza mno gharama ya ulishaji. Kuku (na ndege wengine) na wanyama kama mbuzi, ng'ombe, nguruwe, sungura wanafurahia kula chakula hiki.
PhotoGrid_1645787977321.jpg
 
Hongera sana mkuu. Ni mawazo mazuri sana. Kwa kusimamia mwenyewe hakika utafanikisha malengo yako na Mungu wetu wa mbinguni akutangulie. Ulishawahi kufuga before? Mimi pia hadi sasa nafanya kama unachofanya, nimeanza mwaka jana September na maendeleo siyo haba. Mimi ninafuga almost ndege (Wafugwao) wote wanaopatikana mazingira ya Tz.

Sasa nina haya machache nadhani yanaweza kukufaa;
1. Kwa idadi ya hao matetea unaweza kukomaa ukatotolesha kwa kutumia kuku wenyewe (sina hakika kama sasso wanaatamia). Kwa maoni yangu ni bora kuliko mashine. Ndicho nachofanya. Nilishawauzia watu mashin sana kabla sijaamua kuanza kufiga. Mashine zina changamoto sana ya efficiency. Unaweza peleka mayai 100 ukaambiwa yametotolewa 15. Unaweza zimia au ukahisi umeibiwa. Kuku ukimwekea mayai 13 atakupa walau vifaranga 10. Kuna maelezo mengi sana hapa ya kuelezea. Tuishie hapa kwa sasa.

2. Vifaranga wakitotolewa hakikisha wanakaa juu na poop inadondoka chini. Yaani jenga kitu kama chanja hivi ili huduma zao zote wapate wakiwa juu. Ukifuga hii staili ya siku zote vifaranga wakakaa chini/kwenye maranda utaumia sana. Utachukia ufugaji. Ukifanya hii staili nakuhakikishia hatakufa kofaranga yeyote kwa ugonjwa.

3. Hakikisha unajipanga kwa chanjo zote za muhimu za kuku. Japo kwa hiyo staili ya ukaaji hapo juu (2) niliyosema hata ukiamua usichanje watakua vizuri tu. But no need to risk kwa project kubwa. Wapige chanjo zote muhimu.

4. Hakikisha maji na chakula wanapata ipasavyo na kwa wakati. Bila kusahau usafi wa vyombo. Usicheze na usafi kabisa.

5. Jipe muda wa kukaa na kuku bandani na kiwaangalia, wasome tabia zao. Hii itakusaidia kujua kama kuku anaumwa au la. Kuna muda ugonjwa unaweza ingia usifahamu ukachelewa kuwapa dawa halafu ukakuumiza.

6. Vifaranga hakikisha wanakula super starter (pellet) kwa wiki 2 za mwanzo. Pia katika wiki hizi mbili za mwanzo ukiweza wanyweshe maji yenye multvitamin, OTC 20, Trimazine, Amplorium.

7. Hakikisha hizo dawa hapo juu plus fluban muda wote uko nazo ndani.

8. USAFI wa banda ni muhimu muda wote kama kuku wenyewe walivyo muhimu!

Anyway, yapo mengi ya kuelezea. Muhimu FOCUS.

Kila la heri mkuu!

Dongbei.


*
[emoji120]
 
Mkuu hongera kwa uthubutu na kila la kheri katika ufugaji, mrejesho wako kwa kila hatua utakua mchango mzuri kwetu.

Mimi na bro tuliwahi kujaribu kuwafuga 12 tu kama majaribio ilienda poa mayai tuliyala kiasi na wawili wa mwisho walikua wakubwa kiasi kwamba kwenda kumchinja unaogopa atakugeukia[emoji16]...
Asante Sana.
 
MREJESHO BAADA YA MIEZI MITATU.

Leo tarehe 1 April ni miezi mitatu imepita tangu nimeanza mradi huu. Na huu ni mrejesho kwa vijana wenzangu ili watakapoanza wajue muongozo sahihi.

Nilifanikiwa kununua kuku wengine wakafika jumla 60. Lakini wakapungua
Mpaka Sasa wamebaki 50. Mpaka Sasa nimezika kuku watano wawili kwa ajili ya ugonjwa na watatu walikua wadhaifu wameuliwa na majogoo wakati wanawapanda Mara kwa Mara.

Kuachana na vifo mradi unaenda vizuri, japo mafua na kuharisha ilikua ndio changamoto kubwa lakini kwa Sasa nimeweza kuidhibiti.

Kuku wamekua wakubwa, Ila changamoto hawana uwiano sawa wa ukuaji, hii ni kutokana na wakati nna wanunua walikua hawana ukubwa sawa japo walikua Wana umri sawa.

Mpaka Sasa hawajaanza kutaga japo wanatetea Sana. Nimeambiwa changamoto inaweza ikawa lishe ya awali(yaani wakati wakiwa vifaranga au lishe ya Sasa). Yaani wanasema kuku anaetakiwa kutaga baadae analishwa tofauti na kuku anaetakiwa nyama kipindi Cha kifaranga(bado nafanya utafiti nitaleta mrejesho)

Lakini pia wanasema kuku ukimlisha chakula chenye mashudu mengi, mwili unatengeza mafuta Sana na kuharibu mfumo wa mayai(bado nafanya utafiti nitaleta mrejesho)

Nimefanikiwa kuuza kuku mmoja kwa sh 18,000 na nimepanga kupunguza majogoo kwa sh 20,000 pasaka hii. Na Kama utafiti juu ya chakula kipindi Cha kifaranga kinaweza kuwa sababu ya kushindwa kutaga vizuri au kutaga kabisa basi nitawauza wote nianze upya

Nimefanikiwa pia kutengeneza mashine ya kutotolesha mayai (incubator) ambayo Jana tarehe 31 March imefanikiwa kutotolesha mayai 42 Kati ya 53 ya kanga na mayai 60 Kati ya 60 ya kuku.
Mashine hii Ina uwezo wa kutotolesha mayai tray 6 sawa na mayai 180 mpaka 200.

Mpango ni kutengeneza nyingine ya mayai 720 mapema mwezi huu baada ya kupata matokeo mazuri ya mashine ya awali.

Nitaendelea kutoa mrejesho kwa maendeleo zaidi. Asante
 
MREJESHO BAADA YA MIEZI MITATU.

Leo tarehe 1 April ni miezi mitatu imepita tangu nimeanza mradi huu. Na huu ni mrejesho kwa vijana wenzangu ili watakapoanza wajue muongozo sahihi.

Nilifanikiwa kununua kuku wengine wakafika jumla 60. Lakini wakapungua
Mpaka Sasa wamebaki 50. Mpaka Sasa nimezika kuku watano wawili kwa ajili ya ugonjwa na watatu walikua wadhaifu wameuliwa na majogoo wakati wanawapanda Mara kwa Mara.

Kuachana na vifo mradi unaenda vizuri, japo mafua na kuharisha ilikua ndio changamoto kubwa lakini kwa Sasa nimeweza kuidhibiti.

Kuku wamekua wakubwa, Ila changamoto hawana uwiano sawa wa ukuaji, hii ni kutokana na wakati nna wanunua walikua hawana ukubwa sawa japo walikua Wana umri sawa.

Mpaka Sasa hawajaanza kutaga japo wanatetea Sana. Nimeambiwa changamoto inaweza ikawa lishe ya awali(yaani wakati wakiwa vifaranga au lishe ya Sasa). Yaani wanasema kuku anaetakiwa kutaga baadae analishwa tofauti na kuku anaetakiwa nyama kipindi Cha kifaranga(bado nafanya utafiti nitaleta mrejesho)

Lakini pia wanasema kuku ukimlisha chakula chenye mashudu mengi, mwili unatengeza mafuta Sana na kuharibu mfumo wa mayai(bado nafanya utafiti nitaleta mrejesho)

Nimefanikiwa kuuza kuku mmoja kwa sh 18,000 na nimepanga kupunguza majogoo kwa sh 20,000 pasaka hii. Na Kama utafiti juu ya chakula kipindi Cha kifaranga kinaweza kuwa sababu ya kushindwa kutaga vizuri au kutaga kabisa basi nitawauza wote nianze upya

Nimefanikiwa pia kutengeneza mashine ya kutotolesha mayai (incubator) ambayo Jana tarehe 31 March imefanikiwa kutotolesha mayai 42 Kati ya 53 ya kanga na mayai 60 Kati ya 60 ya kuku.
Mashine hii Ina uwezo wa kutotolesha mayai tray 6 sawa na mayai 180 mpaka 200.

Mpango ni kutengeneza nyingine ya mayai 720 mapema mwezi huu baada ya kupata matokeo mazuri ya mashine ya awali.

Nitaendelea kutoa mrejesho kwa maendeleo zaidi. Asante
Unatengeneza incubator mwenyewe?
 
Baada ya mvua za msimu huu kuwa za kusita na kupoteza mbegu kwa kupanda zaidi ya Mara mbili na kuungua na jua, huku nyanya nazo zikiwa zinachechemea, nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara Aina ya sasso wakati tunaendelea kusubiri neema ya mvua Kama itatuwezesha kuvuna.

Mpango ni kufikisha kuku 1000 na zaidi mpaka mwisho wa mwaka huu 2022.

Kwa Sasa nimeanza na kuku 25 (mitetea 20 na majogoo 5) ambao nimewanunua December 26 wakiwa na miezi miwili.

Malengo makuu ni kusubiri kuku wafike umri wa kutaga kuanzia march 2022 (wakiwa wamefikisha miezi 5) ili nitotoleshe mayai.

Kuku wakianza kutaga nategemea kupata wastani wa mayai 10 kwa siku (kwa uchache) sawa na mayai 100 Kila baada ya siku 10. Hii inamaana Kila baada ya siku 10 nitapeleka mayai 100 kutotolesha.

Baada ya siku 120 ambayo ni wastani wa miezi 4 kuanzia mwezi March sawa na mwezi July 22 nitakuwa nimetotolesha mayai 1200 ambayo kwa wastani nitapata vifaranga 1000 na kidogo (hayo mayai 200) naasume baadhi yatakuwa hayajatotoleshwa au vifaranga watakaoshindwa kuvuka nursery stage.

Kwahiyo mpaka inafika December 2022(insha_Allah) nitakuwa na kuku 1000 ambao ukiachana na parent 25 nilionza nao kutakua na wakubwa wenye miezi 6,5,4(watakua wameanza kutaga) size ya Kati na wadogo kabisa batch ya mwisho miezi miwili.

Baada ya kufikisha idadi hiyo nitaanza kuuza mayai au kutotolesha vifaranga kwa ajili kuuza au kwa ajili kufuga wa nyama.

KUHUSU GHARAMA
Kuku nimenunu 8000 Kila mmoja sawa na 200,000 kwa kuku wote.

Banda lilikuwepo linalowatosha kuku hao 25.

Kwa kuku watarajiwa Banda lao natarajia kuanza kuhangaika nalo baada ya kuku kuanza kutaga. Ambalo nitalijenga kwa awamu nne ( Kila awamu nitakamilisha sehemu ya kuku 300) makisio ya gharama za ufundi kwa Banda la kisasala kuku 1000 na zaidi ambalo nimeandaa eneo la (20x10)m nimepata ni shilling 3.5M kwa materia ya eneo nililokuwepo.

KUHUSU CHAKULA
Kutokana nimewanunua wakiwa wakubwa nimetengeneza mchanganyiko wangu wa chakula ili kupunguza gharama.
Ambapo gharama za debe moja(baada ya kuchanganya) ni chini ya 3000 na kuku wote 25 wanakula debe 1 na nusu kwa mwezi. Na nimeanza mchakato wa kutengeneza funza na hydroponic folders na baadae nitaandaa bwawa la azola.

Baada ya kufikisha kuku 1000 makadirio ya chakula kwa siku ni kilo 130 ambazo ni sawa kwa mchanganyo wangu wa chakula + hydroponic ni 500 kwa kilo.
Sawa na sh 65,000 kwa siku

KUHUSU MATARAJIO YA FAIDA
kwa mwaka huu wote wa 2022 silengi kupata faida, nahitaji mradi ujisogeze na uwe stable. Kwa maana mpaka inafika December 2022 mradi uwe umerudisha gharama zangu japo kwa uchache na uwe inaweza kujiendesha kwa kuuza mayai au kuku.

Baadaya ya mwaka huu nategemea kupata faida Kama ifuatavyo.

1. Kwa kuwa natarajia kwenye kuku 1000 kuwe na mitetea isiyopungua 800 hivyo nategemea kukusanya mayai yasiopungua 510 kwa siku(kwa makadirio ya chini. Sawa na tray 17 kwa siku .

Tray 1ni sawa na tsh10,000 kwa mayai ya chotara (Bei za nilipo) sawa na tsh 170,000 kwa siku

NB: Mradi huu nitausimamia mwenyewe kwa asilimia 100 hivyo hakuta kuwa na gharama za ziada za mfanyakazi.

Hivyo ndivyo nitavyoiishi 2022.
Nakaribisha maoni.
Hongera chief.....ila nikwambie kitu, hutapata mayai zaidi ya matano kwa siku.

Sasso sio a layering breed....ni kuku kwaajili ya nyama. Uwezo wao wa utagaji ni mdogo sana, na ni chini ya asilimia 30 kwa siku.

Tafuta breed nzuri kwaajili ya mayai. Nakuhakikishia hutapata mayai zaidi ya matano kwa siku. Nitafute kwa mwongozo zaidi.
 
Hongera chief.....ila nikwambie kitu, hutapata mayai zaidi ya matano kwa siku.

Sasso sio a layering breed....ni kuku kwaajili ya nyama. Uwezo wao wa utagaji ni mdogo sana, na ni chini ya asilimia 30 kwa siku.

Tafuta breed nzuri kwaajili ya mayai. Nakuhakikishia hutapata mayai zaidi ya matano kwa siku. Nitafute kwa mwongozo zaidi.
Hivi hakuna crossbreed ya kuku wa kienyeji na wa mayai, ambao wanatoa mayai kedekede?
 
Back
Top Bottom