Najibu maswali yenu hapa...Uliza chochote

Najibu maswali yenu hapa...Uliza chochote

Da'Vinci

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2016
Posts
35,812
Reaction score
107,628
Habarii
Jana niliulizwa maswali kwenye uzi flani as HardTalk Bahati mbaya sikuweza kuyamaliza yote kutokana na simu kuisha chaji. Hivyo basi Ningependa kujibu maswali yote yaliyobaki na kama kuna swali lolote uliza.. about Psychology, Theology, Philosophy, Science and technology, Politics, Entertainment, Cosmology, Economy etc etc...

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk
 
1.Unaonekana unafuatiliaga sana movie jee ni ipi latest uliyoona ni kali?
2.Tukikukabidhi leo hii JF uwe mmiliki wake jee ni kitu gani ungeongeza na kipi ungeondoa na kwa nini uongeze hicho ama upunguze kile?
3.Kwa siku minimumu na maximumu unalala masaa mangapi?
4.Jee katika jamii inayokuzunga ni jambo gani hukukela zaidi pale unapoliona/kukumbana nalo?
5.Idea yako ya kutafri vitabu kuja lugha adhimu ya kiswali imefikia wapi?

End Justify Mean
Mkuu MwiH
●Napenda muvi sana kuliko hata chakula muvi kali Latest niliyoipenda ni Glass iliyotoka wiki iliyopita.
●Kama nikipewa JF nisimamie >>ningeongeza wigo wa memba kua na uwezo wa kujieleza Openly. Hakuna kujieleza kwa uwazi Jf, tupo limited kwa baadhi ya mambo labda kutokana na mfumo wa serikali kuikaba koo JF nao wanafanya ivo kulinda ugali
>> Ningepunguza Multiple Ids.. kuna utitiri wa ma id meengii hadi tunaonekana tuko memba wengii humu
●Mkuu mm ni Sleepless elite yaani kundi la watu wanaolala muda umeenda na kuamka mapema!mara nyingi nalala saa 8 Usiku naamka saa 12. Ratiba yangu ya siku inaanza saa 6 mchana.
●Hakuna kitu sipend kama kuona mtu akionewa au kudhurumiwa naumia na ninakereka sana.. ajili yaa hii yashanikuta mambo sana.
●Mkuu idea ya kutafsiri vitabu kiukweli nimeiweka pending coz niliona kuna mzunguko mkubwa kufanikisha hilo naweza pelekwa segerea bure. Pia sikupata mtu aliyevutiwa na wazo langu but bado ipo kichwani labda ipo siku nitaandika kitabu changu.
Nimekujibu?????

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk
 
1. Ni swali gani gumu kwako? Na ni kitu gani hupendi watu wakijue kukuhsu?
2. Ni kitu gani kimewahi kukufurahisha kwenye maisha yako ambacho huwezi kukisahau?
3. Kipi/ nini kinatukwamisha kwenye uchumi wa kati? Viongozi, mfumo am sisi wenyewe? Kipi kifanyike?
4. Upi mtizamo wako wa kuongozwa na chama kimoja muda mrefu? Imetusaidia ama imeongeza mgawanyiko/matabaka?
5. Tumeshuhudia kundelea kufanya vibaya kwa shule za serikali. Je, wapi tunakosea? Wazazi na muamko duni wa elimu au incentive za serikali hazikidhi mahitaji? Elimu bure?

Utaniwia radhi kama kuna replication. Kama ipo nilink na majibu husika tafadhali. Obrigado[emoji1488]

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu
4G LTE
●Swali langu gumu ni Je Mungu anajua destination yetu?? I mean anajua kama nitaingia motoni au peponi. Mkuu hiko kitu nisichopenda wajue nikikitaja hapa watu watakua wamejua.
●Kinachotukwamisha uchumi wa kati ni watu wenyewe na mfumo wa serikali. pia watu hawazitambui fursa japo wengine wanazitambua ila hawawezi tekeleza kutokana na kutokua na Mitaji ya pesa na akili. Cha kufanyika ni kua watu wawe na mapenzi ya dhati na nchi yao waijenge nchi yao wenyewe, pia serekali iwe mfumo ambao utaweza kusaidia watu kuwavutia kuja kuwekeza nchini
●Daah mkuu issue hii ngumu kidogo! Mm sidhani kama kuongozwa na chama kimoja kuna shida. Mm sihitaji niongozwe na vyama vingi vilivyokaa madarakani nataka niongozwe na chama kitakacho simamia maslahi ya wananchi wengi wa Tanzania sio ya watu wachache shida ni kua Chama hiki kiukweli kishapitwa wakati sera zake na watu wamekichoka kutokana na kutotimiza yale wanayoahidi. Ccm ina mazuri mengii na mabaya mengi tuu
●mkuu kwanza mfumo wetu pia uko ovyoo kiukweli haumjengi mwanafunzi kua Competent wazazi pia kiasi flani wana mwamko duni hasa vijijini
Swala la elimu bure ndo shida kabisa!
Sijui wakati serikali ina tekeleza hii sera iliwaza nini, labda walitaka sifa kwa wananchi wao!! Imagine unatoa elimu bure hafu shule hakuna madarasa wala dawati, walimu wala vifa vya kufundishia. Watoto wanajazana tuuu mwisho wa siku shule hawasomi wanakua wanaenda kucheza tu huko.
Nadhani sweikali ingajipanga kwanza kuitekeleza hii sera ya elimu bure maana haina tija kama watu wanaenda kusoma bure hafu hakuna vifaa wala darasa!!SERIKALI HAPA ILIKURUPUKA.
●Tanzania itajengwa pindi watu watakapo jitoa kuijenga kwa akili na nguvu zoote...
Nimekujibu? ???

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk
 
~una ushauri gani kwa wana JF has a ukioanisha kati ya awamu ya NNE na awamu hii ya tano,ya hapa kazi tu...ktk ujenzi wa Taifa.??

~ungepewa nafasi ya kuzaliwa upya ungependelea uzaliwe nchi gani...na nani.!?

~kwa nini waliompiga Tundu Lissu risasi hawajulikani,ilhali CCTV camera zinasemekana zilishuhudia tukio.!?

~je unadhani watekaji wa MO walipewa ile bilioni ndio wakamwachia...au ilikuwaje? Nini Mirza no wako?

~'Kilimo ndio uti wa mgongo.' Je unadhani hii Sera bado inazingatiwa!?

~Una ushauri gani kwa Mh.Rais,hasa ukiwakilisha kundi LA vijana?

~Watanzania wengi hawana bima ya afya na hata iliyopo in gharama kubwa,nini kifanyike.!?



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu
Heller
●Aisee kwa awamu hii wajikaze tu kupambana ili kuendana na sera hio maana hakuna mwanya wa kuchota hela bila kufanya kazi. Fanyeni kazi kwani mwanaume hula kwa jasho.
●Napenda Japan coz wako very civilized na wako na Nidhamu ya hali ya juu. Ila napenda kuishi mji wa Canton Aasa ivi waitwa Guangzhou China
●What mkuu CCTV kamera zilisema zimeshuhudia tukio??? Aikuwahi sikia hiii. Lakini hio sio njia pekee ya kumfahamu muuaji
●Hapana sidhani kama walipewa au hawakupewa maana jibu sahihi analo mtekaji au Mo mwenyewe ukizingatia sikuwepo ila kwa mtazamo wangu sidhani kama walikua wanahitaji hio bilion japo wanaweza kua waliichukua ili kuziwia loop hole za kutokufahamika
●Kilimo ndio uti wa mgongo wa Dunia! Lakini kwa tanzania sera inazingatiwa ila haitekelezwi ipasavyo. Hakuna soko kwa mkulima, hakuna pembejeo toshelezi na zinazomudika (Affordable ) kwa mkulima wa hali ya chini. Bahati mbaya tunategemea mvua ili tulime. Serekali nadhani wanalijua hili na wanalifanyia kazi one day yes!!
●Aunde sera itakayoweza kuwafanya vijana kuweza kujiajiri hasa kupata mikopo ya mitajii sio kutegemea ajira.
●Rais aliangalie hili pia maana afya bora ndio maisha. Awaangalie watu wa chini jinsi ya kuwasaidia kumidu bima za afya kutokana na hali zao ukizingatia anasema ni raisi wa wanyonge.
Lakini mkuu Elfu hamsini ni kubwa sana???
Je nimekujibu?


Sent from my GT-I9300 using Tapatalk
 
Habarii
Jana niliulizwa maswali kwenye uzi flani as HardTalk Bahati mbaya sikuweza kuyamaliza yote kutokana na simu kuisha chaji. Hivyo basi Ningependa kujibu maswali yote yaliyobaki na kama kuna swali lolote uliza.. about Psychology, Theology, Philosophy, Science and technology, Politics, Entertainment, Cosmology, Economy etc etc...

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk
Kila siku nasikia wale Wakristo wa madhehebu ya Kipentekosti wakikemea kunywa pombe. Je Biblia yetu inasemaje kuhusu kunywa pombe na je unakubali je unakubali kunywa pombe si dhambi?
 
Conspiracy Theory ni nini?

Mtu mwenye personality disorder anakuwaje?
Habarii mkuu
Ledada
Conspiracy theory ni Nadharia inayoeleza tukio au mpango wa siri ambao umewekwa. Yaweza kua kweli au si kweli
●Mtu mwenye personality disorder hua fikra zake haziko vizuri pia hua anashindwa kuongoza hisia zake mara nyingi anakua na hofu ya kutengwa na wale anaowapenda (anayempenda)
Nimekujibu???

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk
 
Habarii mkuu
Ledada
Conspiracy theory ni Nadharia inayoeleza tukio au mpango wa siri ambao umewekwa. Yaweza kua kweli au si kweli
●Mtu mwenye personality disorder hua fikra zake haziko vizuri pia hua anashindwa kuongoza hisia zake mara nyingi anakua na hofu ya kutengwa na wale anaowapenda (anayempenda)
Nimekujibu???

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk
Salama Mkuu,
Umejibu mkuu Shukrani[emoji4]
 
Back
Top Bottom