Najibu maswali yote kuhusu Afya ya kinywa na meno

load

Member
Joined
Mar 19, 2017
Posts
83
Reaction score
47
Habari wakuu

Niulize swali lolote kuhusu kinywa na meno, ntakujibu.

Karibuni.
 
meno yangu hupatwa na ganzi pindi nikila chakula chenye uchachu pia nikinywa soda aina ya pepsi. nini chanzo cha tatizo na tiba yake ni nini?
 
Je kuna madhara ya kutumia tooth picks?

Vipi kuhusu dental floss?
 
Je kuna madhara ya kutumia tooth picks?

Vipi kuhusu dental floss?
Kuna madhara. Baada ya matumizi ya muda mrefu ya tooth pick fizi huwa zinapata damage na kuanza kutoka damu.
Dental floss ndio njia sahihi ya kusafisha meno na fizi baada ya kupiga mswaki.
Njia sahihi ya kupiga ni kutopiga straight bali kwa nusu mviringo.
Na pia kuanza kupiga mswaki sehemu tofauti tofauti .
Faida yake ni sehemu zote kupata attention sawa kwenye upigaji wako wa mswaki.
Pia usisahau ulimi.
 
Sante Dkt.Mfawidhi.
Ni kweli hayo ma-tooth pic yananiachiaga majeraha mpaka napata root abscess.
Nitazingatia miongozo yako.✔
 
Reactions: Tui
Habari wakuu

Niulize swali lolote kuhusu kinywa na meno, ntakujibu.

Karibuni.

magego yangu yote yana mashimo,alafu fizi zinatoka damu mara kwa mara haswa kipindi cha asubui nikitoka kuamka


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nauliza kijana wangu kapa ajali Meno mawili ya juu yametoja je kunawezekano wa kuota tena ?
Umri miaka 9

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Layer ya nje ya jino (enamel) inalika/inasagika, hasa maeneo ya jirani na fizi. Kuna tiba ya tatizo hili?
 
Meno kuwa na ganzi unapokula vitu vichachu au baridi tiba yake nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna dawa za meno na dawa za kusukutua Lakini hazimalizi tatizo kabisa. Nenda kwa daktari wa meno kwa uchunguzi kwani kuna uwezekano meno yako yameanza kulika na kuwa na matundu.
 
mkuu nina ndugu yangu mmoja ..kila asubuhi akiamka upande mmoja wa shavu la kushoto unavimba kidogo utafikiri anaumwa na jino ,na watu wengi humwambia jambo hilo .lakini baada ya masaa mawili matatu uvimbe hupote..je unahisi jambo gani hilo shukuran

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Layer ya nje ya jino (enamel) inalika/inasagika, hasa maeneo ya jirani na fizi. Kuna tiba ya tatizo hili?
Jaribu kuacha kutumia vitu vichachu,sukari,soda.
Usipige mswaki na dawa yenye fluor nyingi. Enamel ni ngumu sana. Mpaka iwe damaged hujatake care nzuri ya meno yako.
Kabla tatizo halijawa kubwa zaidi muone daktari wa meno kwa uchunguzi.
 
Sina jawabu la uhakika kwa kweli. Amuone daktari wa meno kwa uchunguzi wa awali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…