Elections 2010 Najua baadhi inawauma lakini huyu ataendelea kuwepo

Elections 2010 Najua baadhi inawauma lakini huyu ataendelea kuwepo

Jembejipya

Member
Joined
Sep 23, 2010
Posts
8
Reaction score
0
JAKAYA MRISHO KIKWETE
1.Mtanzania pekee aliyewafanya wapinzani uchwara walie kuomba uongozi.
2.Mtu pekee ambaye mafanikio yake kimaendeleo yanapingwa kwa porojo.(bila takwimu)
3.Mtu pekee katika Tanzania ya leo aliyekubali kuacha sheria iwashughulike wanadhirifu wa mali za umma.
4.Rais wa Tanzania 2005 - 2015.
5.Aliyegeuza ilani ya CCM na mafanikio yake kuwa kama moto ambao kila mpinzani anaogopa kuukaribia.
 
Of course, as long as vipofu kama wewe wenye kutafsiri ufisadi kuwa ni mafanikio mkiendelea kuwepo kwanini mlezi wa mafisadi asiwepo?

Halafu upofu wa aina hii sio wa bahati mbaya bali wa kuitakia,aidha kutokana na njaa, kujikomba au ubabaishaji tu. Hivi ni kwa ujira gani unaweza kuwasaliti ndugu zako kule kijijini wanaoishi katika hali mbaya zaidi ya ilivyokuwa zama za ukoloni?

Kweli njaa yako ni muhimu zaidi ya rafiki zako wanaobambikiziwa kesi na polisi kwa vile tu hawana uwezo wa kuhonga wanausalama hao?Unawaambia nini akinamama wanaoahidiwa bajaji na Kikwete ilhali yeye na vigogo wenzie wanatanua kwa mashangingi ya mamilioni ya shilingi?

Ni dhahiri umejiunga leo na JF sio kwa vile ulikuwa huifahamu au huipendi bali ni hayo maagizo kutoka kwa Usalama wa Mafisadi.

Just be careful, usitukane mamba kabla hujavuka mto.
 
Hapa kama unampigia mbuzi gitaa!! wanachadema watakaaa kwasababu ya ma highway wanayoyaona kule walipo!! basi wanadhani slaa na yeye atayaleta!

... asante kwa ujumbe!! wameusoma huo
 
Tumgeukie huyo Kikwete wako

JAKAYA MRISHO KIKWETE

1.Mtanzania pekee aliyewafanya wapinzani uchwara walie kuomba uongozi.

Kama unaongelea wapinzani uchwara, basi wewe una uongozi uchwara.Tafadhali tuambie kafanya nini kwa wapinzani ukweli, na sio wapinzani uchwara. You do not judge a leader's ability by how he works with his easiest challenges, but how does he work with his hardest ones.

2.Mtu pekee ambaye mafanikio yake kimaendeleo yanapingwa kwa porojo.(bila takwimu)

Mafanikio gani ? Takwimu zina tabia ya kuweza kudanganya vizuri tu.Ninaweza kuwaita watu wa Kikwete 100 na kuwauliza maswali ambayo yako favorable kwa Kikwete, wakatoa majibu ya kumpendelea Kikwete na kutoa headline kwamba katika survey fulani Kikwete amekubalika 100%. Mafanikio ya Kikwete zaidi ya mafanikio yakutegemewa kwa wastani wa kawaida yako wapi? Hizo shule zisizo na walimu wala majengo ? Hizo ahadi zisizotimilika ? Hebu tupe hayo mafanikio ya Kikwete tuweze kuyajadili. Inaonekana katika kuwashutumu watu kumpinga Kikwete bila takwimu, wewe ndiye unasema Kikwete ana mafanikio bila takwimu.

3.Mtu pekee katika Tanzania ya leo aliyekubali kuacha sheria iwashughulike wanadhirifu wa mali za umma.

Kikwete majuzi kawapigia kampeni Mramba na Lowassa, watu ambao uchafu wao unajulikana na umeelezwa vya kutosha.Kasema Lowassa hakufanya makosa anachafuliwa tu. Kwa kuwapigia kampeni na kutoa kauli kama hizo kuhusu watu hawa, wengine ambao kesi zao bado ziko mahakamani, Kikwete kashaingilia uhuru wa mahakama . Unawezaje kusema kwamba Kikwete kaachia mahakama imshughulike mtu kama Mramba ? Hivi Kikwete kama ana interest ya kumuona Mramba anashinda ubunge ili CCM ichukue kiti, kweli Kikwete anaweza kuwa serious kwa vita dhidi ya rushwa? Kama alikuwa serious kwa nini alimfanmyia kampeni Mramba ambaye kesi yake iko mahakamani na Lowassa ambaye kajiuzulu katika wingu la rushwa ?

4.Rais wa Tanzania 2005 - 2015.

We have lowered the bar so low now to the extent that almost anybody can be president, and this presidential clout business, to seriously thinking people at least, will not be a distinction by itself. What did he do as president ? Watanzania tuna tatizo la kutoa ofisi ambazo mtu kazishika kama distinction. Ofisi ambazo mtu kazishika si distinction. Ukitaka kutuonyesha distinction tuonyeshe huyo mtu kafanya nini katika ofisi hizo.

5. Aliyegeuza ilani ya CCM na mafanikio yake kuwa kama moto ambao kila mpinzani anaogopa kuukaribia.

CCM haina hata itikadi, much less ilani. Ilani gani ? Mafanikio gani ? Sio wewe uliyelaumu watu kumpinga Kikwete bila takwimu, sasa mbona unataka kumtetea bila takwimu na kuvunja sheria yako mwenyewe ?
 
Kumbe anaekurupukaga CCM sio Mwalimu wa UPE peke yake. Wako wengi.
 
JAKAYA MRISHO KIKWETE a.k.a Msanii,alipokuwa Ludewa ndo katia fora katoka na staili ya kupokea simu kabla ya kupanda jukwaani halafu anawambia wananchi alikuwa anazungumza na balozi wa Marekani, eti Obama kaahidi kuendelea kutoa misaada..tehtehteh ....kumbe alikuwa anaongea peke yake,jamaa msanii yule.. ehe....
 
Tuache ushabiki "maandazi" maendeleo ni pamoja na kubadili uongozi..
Kula TANO Mkuu Kiranga...
 
Kama aliyofanya yanakubalika kwa nini anahangaika kiasi hicho kubandikwa kila kona ya nchi kama vile ni mgeni kwa wananchi. hadi kinana anasema inabidi siku za mapumziko zipunguzwe na kufanya kampeni nyingi zaidi kwa maana hali ni mbaya? CHEMA CHAJIUZA KIBOVU CHAJITEMBEZA. kama anakubalika mbona hata mikutano haina watu inabidi muwzombe kwa malori kutoka sehemu moja hadi nyingine?

Hivi bado hujakubali kua JK amedorora tofauti na ilivyokua 2005. kwa taarifa yako watanzania 2010 Hawadanganyiki!
 
Wageni wengine mashaka matupu

Jembejipya

  • profile.png
    View Profile
  • forum.png
    View Forum Posts
  • message.png
    Private Message
  • article.png
    View Articles
  • add.png
    Add as Contact

user-offline.png
Junior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
Join DateThu Sep 2010Posts1Thanks0Thanked 0 Times in 0 Posts Rep Power0

Nakubaliana na wewe Wageni wapya wanakuja na moto lakini Moto wao huwa wa kuni tu haukawi kuisha mwache aje na kasi yake kwa kuwa anaonyesha ni CCM Damu unakaribishwa lakini usilete Matusi hapa. njoo na heshima yako Mkuu Jembejipya. Tunataka utupe ushahidi wako sio kuleta upinzani waTimu ya Simba na Yanga asante karibu tena.
 
Nakubaliana na wewe Wageni wapya wanakuja na moto lakini Moto wao huwa wa kuni tu haukawi kuisha mwache aje na kasi yake kwa kuwa anaonyesha ni CCM Damu unakaribishwa lakini usilete Matusi hapa. njoo na heshima yako Mkuu Jembejipya. Tunataka utupe ushahidi wako sio kuleta upinzani waTimu ya Simba na Yanga asante karibu tena.

Msemo wa Iza kwamba tuache ushabiki "MAANDAZI"
 
Timkalibishe atoe maoni yake na atoe Evidence tatizo ni kwamba hawa wageni hawajui kuwa unapoingia humu njoo na evidence kuhakiki unachokisema hii si kwajili ya Chadema au ccm ni yawatanzania. Toa evidence tumpe kura jk bwana Jembe jipya.
 
Wewe kweli Jembejipya. Hata kunolewa halijanolewa. Post yako ya kwanza hata mashiko haina!!!! Kwani hizo ni sifa?

Toa mifano ya mafanikio siyo pambo za jumla jumla.
 
Kwanza bisha hodi. Halafu karibu. Naamini hapa tongotongo litakutoka tu.

Tutakuelimisha hata kama uliishia la saba, hata kama ni M-CCM ambaye husikii wala huambiliki. Hata kama umetumwa kubandika vipost uchwara hapa.

Mwisho wa siku RAIS WAKO NI DOCTOR SLAA.
 
Tumgeukie huyo Kikwete wako

JAKAYA MRISHO KIKWETE

1.Mtanzania pekee aliyewafanya wapinzani uchwara walie kuomba uongozi.

Kama unaongelea wapinzani uchwara, basi wewe una uongozi uchwara.Tafadhali tuambie kafanya nini kwa wapinzani ukweli, na sio wapinzani uchwara. You do not judge a leader's ability by how he works with his easiest challenges, but how does he work with his hardest ones.

2.Mtu pekee ambaye mafanikio yake kimaendeleo yanapingwa kwa porojo.(bila takwimu)

Mafanikio gani ? Takwimu zina tabia ya kuweza kudanganya vizuri tu.Ninaweza kuwaita watu wa Kikwete 100 na kuwauliza maswali ambayo yako favorable kwa Kikwete, wakatoa majibu ya kumpendelea Kikwete na kutoa headline kwamba katika survey fulani Kikwete amekubalika 100%. Mafanikio ya Kikwete zaidi ya mafanikio yakutegemewa kwa wastani wa kawaida yako wapi? Hizo shule zisizo na walimu wala majengo ? Hizo ahadi zisizotimilika ? Hebu tupe hayo mafanikio ya Kikwete tuweze kuyajadili. Inaonekana katika kuwashutumu watu kumpinga Kikwete bila takwimu, wewe ndiye unasema Kikwete ana mafanikio bila takwimu.

3.Mtu pekee katika Tanzania ya leo aliyekubali kuacha sheria iwashughulike wanadhirifu wa mali za umma.

Kikwete majuzi kawapigia kampeni Mramba na Lowassa, watu ambao uchafu wao unajulikana na umeelezwa vya kutosha.Kasema Lowassa hakufanya makosa anachafuliwa tu. Kwa kuwapigia kampeni na kutoa kauli kama hizo kuhusu watu hawa, wengine ambao kesi zao bado ziko mahakamani, Kikwete kashaingilia uhuru wa mahakama . Unawezaje kusema kwamba Kikwete kaachia mahakama imshughulike mtu kama Mramba ? Hivi Kikwete kama ana interest ya kumuona Mramba anashinda ubunge ili CCM ichukue kiti, kweli Kikwete anaweza kuwa serious kwa vita dhidi ya rushwa? Kama alikuwa serious kwa nini alimfanmyia kampeni Mramba ambaye kesi yake iko mahakamani na Lowassa ambaye kajiuzulu katika wingu la rushwa ?

4.Rais wa Tanzania 2005 - 2015.

We have lowered the bar so low now to the extent that almost anybody can be president, and this presidential clout business, to seriously thinking people at least, will not be a distinction by itself. What did he do as president ? Watanzania tuna tatizo la kutoa ofisi ambazo mtu kazishika kama distinction. Ofisi ambazo mtu kazishika si distinction. Ukitaka kutuonyesha distinction tuonyeshe huyo mtu kafanya nini katika ofisi hizo.

5. Aliyegeuza ilani ya CCM na mafanikio yake kuwa kama moto ambao kila mpinzani anaogopa kuukaribia.

CCM haina hata itikadi, much less ilani. Ilani gani ? Mafanikio gani ? Sio wewe uliyelaumu watu kumpinga Kikwete bila takwimu, sasa mbona unataka kumtetea bila takwimu na kuvunja sheria yako mwenyewe ?
'

Ila huyu jamaa akiamua kushuka, huwa anashuka kweli, namkubali sana.

Akipunguza ugomvi, na watu wakaacha kukaa wanamchokonoa chokonoa, JF ina hazina kubwa sana hapa. Principal ya kwenda vizuri na Kiranga, hata kama umegombana naye, msikilize vizuri hoja zake, na umjibu kwa hoja,..., basi!
 
Rais pekee aliyekimbia mdahalo!.

Kama kuna mambo ambayo jk kafanya ambayo ni yakujivunia. mwambie akubali mdahalo ili atupe hizo takwamu.
 
Ongeza na haya
-Kiongozi pekee aliyeimarisha utawala bora unaozingatia utawala wa sheria
-kiongozi pekee aliyeimarisha democrasia nchini
-kiongozi pekee aliyewachukulia hatua mafisadi bila kuangalia vyeo vyao
-kiongozi pekee aliyekubali kupitisha sheria ya gharama za uchaguzi
-kiongozi pekee aliyeboresha elimu chini (kafuta ada za mitihani, kajenga shule lukukii)
-kiongozii pekee aliyejenga chuo kikuu cha kimataifa cha Udom
-kiongozi pekee aliyeboresha soka nchini kwa kumleta kocha mbrazili (na kufuta usemi wa kichwa cha mwendawazimu)
-kiongozi pekee aliyekuja na kauli mbio kilimo kwanza
-kiongozi pekee anayechukia ufisadi
-kiongozi pekee aliyezuia viongozi kununua magari ya kifahari (mashangingi)
-kiongozi pekee anayeanguka majukwaani kwa dhiki kwa ajili ya wananchi wake

NB: Mambo ni mengi ALIYEFANYA BABA HUYU, KWA REJEA SOMA ILANI YA UCHAGUZI CCM
 
Ongeza na haya
-Kiongozi pekee aliyeimarisha utawala bora unaozingatia utawala wa sheria
-kiongozi pekee aliyeimarisha democrasia nchini
-kiongozi pekee aliyewachukulia hatua mafisadi bila kuangalia vyeo vyao
-kiongozi pekee aliyekubali kupitisha sheria ya gharama za uchaguzi
-kiongozi pekee aliyeboresha elimu chini (kafuta ada za mitihani, kajenga shule lukukii)
-kiongozii pekee aliyejenga chuo kikuu cha kimataifa cha Udom
-kiongozi pekee aliyeboresha soka nchini kwa kumleta kocha mbrazili (na kufuta usemi wa kichwa cha mwendawazimu)
-kiongozi pekee aliyekuja na kauli mbio kilimo kwanza
-kiongozi pekee anayechukia ufisadi
-kiongozi pekee aliyezuia viongozi kununua magari ya kifahari (mashangingi)
-kiongozi pekee anayeanguka majukwaani kwa dhiki kwa ajili ya wananchi wake

NB: Mambo ni mengi ALIYEFANYA BABA HUYU, KWA REJEA SOMA ILANI YA UCHAGUZI CCM

Yeah..ameyafanya hayo yote ktk DUNIA YA KUSADIKIKA au usingizini..walah mbavu zangu wajameni
 
Back
Top Bottom