Najua Huwezi Sahau Lakini Je Can You Really Forgive Someone Who Cheated on You

Najua Huwezi Sahau Lakini Je Can You Really Forgive Someone Who Cheated on You

nikisamehe tu ujue na mimi nilisha fanya.............kama sivyo basi i promise my heart kufanya na mimi

Thats my point mkuu wangu.... hata mtu akikusamehe kwa maneno tu ila atakuwa anakukumbushia kila unampomkwaza.... inakuwa ni kama tool anayotumia.....

ila to give credit where credits due... Kuna mama mmoja ninamfahamu bwana yake alimtelekeza akamfukuza akachukua kimada mwingine..... unfortunately huyo bwana akapooza na kutoweza kufanya chochote.... Guess who anayemuhudumia... yuleyule mama aliyemtelekeza yaani amemsamehe na bado anasacrifice muda wake kumuhudumia.....

Kweli kuna some Angels around... lakini siku hizi ni wachache wa moyo huo, wenye upendo wa kweli.
 
it is very hard to dress a white dress with dirty spots and still cheat urself that u look smart!! bora usijue tu coz hata ukisamehe memory huwa zinarudi tu..u better stay away.
 
I can 4give bt siwezi sahau na i can't trust tena so its better tukitengana!
 
I can 4give bt siwezi sahau na i can't trust tena so its better tukitengana!
hii ni very theoretical... kama uko ndani ya ndoa ndio utajua hali ilivyo... we forgive but we dont forget, we hope but we dont give 100% trust... one thing for sure, if you aim at revenging, then you are not in this world, coz you are bound to suffer for the rest of your life
 
Kusamahe ni kugumu sana kumbuka umemwumiza mwenzio na umemvunja imani na wewe. Hata kama atakusamehe itachukua muda mrefu hadi kurudi hali ya kuridhika. Ninaiita hali ya kuridhika kwa sababu trust nikama sahani ya udongo ikivunjika tu vipande hata ukiigundisha na superglue haitawezekana kurudi ktk hali ya mwanzo.
Hali ya kuridhisha ni pale mtu anapoangalia mambo mengi na kujipa moyo yataisha. Shida ni pale huyo mtenda kosa asijutie kosa na akichukulia msamaha aliopewa ni haki yake. Hii ndio huleta matatizo mengi katika ndoa. Wanawake wengi huumia sana hasa mwanaume akaendelea kujitutumua kana kwamba nothing happened na kwa kuwa kasamehewa basi everything is back to normal. Nothing is normal na inabidi mwanaume utafute namna ya kumjenga imani mwenzio and it is time consuming.
Wanawake mara nyingi unakuta wazee waliotutangulia wanasema kuvunja familia ni uamuzi wa mwanaume na siyo mwanamke na hili huwapa jinamizi wanawake wengi wanaendelea kuishi ktk loveless marriages.
Cheating mara nyingi ni mwanzo wa mwisho wa ndoa. Do not try it if you can fight it as much as you can si kwa mwanamke na si kwa mwananume. Ndoa ni kazi ngumu sana.
Kusamehe kuna kuwa kurahisi pale mnaposhirikiana kujenga imani kwenye ndoa.
 
wanawake wengi wanasamehe na kusahau....pia, ndoa nyingi ambazo baba ni kinara wa kutoka nje ya ndoa, mkewe akitoka ni rahisi kusamehe kwasababu anaona kama sawa tu kwasababu yeye pia hutoka nje ya ndoa...ila kuna aina hii ya ndoa ambayo baba hajawahi kutoka nje ya ndoa, na hategemei kutoka nje ya ndoa...au mama hajawahi kutoka nje ya ndoa na hategemei kutoka nje ya ndoa..mmojawapo akitoka nje ya ndoa, kidonda chake huwa ni kukubwa sana, na kama anatoka kabila fulani hivi, unaweza kumkuta ananing'inia au kama sivyo makabila mengine, atakucharanga mapanga au atakuwa chizi...cha muhimu kuelewa ni kwamba, kutoka nje ya ndoa ni dhambi kubwa ambao Mungu huwa anaadhibu, dhambi zote ni sawa lakini Mungu anasisisita uzinzi akisema kuwa, ni dhambi tofauti na zingine kwasababu inafanyika ndani ya mwili pale mnapoingiliana, mnajiunganisha na ni dhambi ambayo huwa haiendi bila mapigo mbele za Mungu kama mtu hatatubu kwa kumaanish akuiacha. pili, kwa wale waliotendwa awe mwanaume au mwanamke, jua kuwa, kusamehe ni lazima, na usiposamehe, Mungu pia hatakusamehe.

kama vile unavyoona inauma sana unapotendwa na mkeo au mmeo, hivyohivyo inamuuma sana Mungu pale unapomsaliti kwa kukubali mambo ya kishetani badala ya kumwamini na kumsubiri yeye...imagine mtu anaenda kwa mganga wa kienyeji akiona kuwa ndo suluhisho badala ya kwneda kwa Mungu, that means, mganga ni muhimu kwake na ana nguvu kwake kuliko Mungu..tusi gani hilo? ni mambo gani tumefanya kwa kumsaliti Mungu, na ni madhambi mengi sana watu tunafanya waziwazi na Mungu anatuona hata akiwa ameshatuonya...lakini Mungu anatuvumilia kwa neema yake, anatusamehe....Mungu akihesabu maovu ni nani atakayesimama? USIPOWASAMEHE WATU MAKOSA YAO YA MUNGU WETU WA MBINGUNI HATATUSAMEHE SISI MAKOSA YETU...kusamehe hakuna option...
 
Mungu tusaidie. Najua hatuwezi pasipo msaada na nguvu zako. Ushukuriwe Mungu kwa sababu umesema hutatuacha tujaribiwe kupita tuwezavyo na pamoja na hilo jaribu utafanya na mlango wa kutokea.

Lakini pia Mungu Tuepushie majaribu yatokayo kwa yule mwovu Ibilisi maana hayo yanauma zaidi na yanatutenga na wewe Kabisa.

Mungu wabariki wadada na wa kaka wa JF, bariki ndoa zao, ziponye, zifanye kuwa mpya kila siku. Wabariki na wale ambao hawajapata wenza wao, wasiumizwe tena bali uwape wale walio wa kwao kweli kweli.

Happy new year all.
 
Mungu wabariki wadada na wa kaka wa JF, bariki ndoa zao, ziponye, zifanye kuwa mpya kila siku. Wabariki na wale ambao hawajapata wenza wao, wasiumizwe tena bali uwape wale walio wa kwao kweli kweli.

Happy new year all.
Amina;
Ameen;
Amen;
Hallelujah
Jah Bless....
 
Back
Top Bottom