Najuta nimezaa nje ya ndoa, ushauri wako muhimu sana

Najuta nimezaa nje ya ndoa, ushauri wako muhimu sana

kaka hapo kweli tatizo, labda utuambie, huyo bi mdogo anajua kama umeoa maana asije akawa anajua utamuoa. ila la muhimu meleze mkeo, naamini atakuelewa tu.
 
Umesema vyema kabisa The Boss

Fanya hivyo paulss ili ukweli ukuweke Huru

Itakuwa tabu sana ikijulikana wakati watoto wameshakua wakubwa

Tubu kwa kosa la kutoka nje, Ila iwe Toba ya kweli kwa mkeo na kwa Mungu

Kisha toa taarifa kwa hatua
 
Last edited by a moderator:
iyo ya hawana pa kwenda imepitwa na wakati sana, especially unapoleta madharau kama hayo. Kuna wanawake wengi tu wanaweza kujitegemea, na wengine ndio bread winners, unasemaje hapo.

Unaweza kuwa na hela zote duniani bado utahitaji mwenza,ndo mana mnanunua viserengeti boys/marioo etc.
 
'Mtoto wa nje' ndo kitu gani? I hate this neno,kwangu mtoto ni mtoto na ninao kibao na nawapenda wanangu wote na kuwatunza.
Mtoa mada sikiliza bana,huyo mkeo asikutishe na wala huna sababu y a kuogopa kihivyo. Ulichokifanya ni jambo la kawaida sana na asilimia kubwa ya wanaume tumepitia huko.La kufanya:
A) Face the girls parents. Mchukue nduguyo unayemwamini mwende kwa wazazi wake, weza kwenda na baba,mama,kaka,mjomba does'nt matter,nyie nendeni,mtalipishwa faini itakuwa imetoka hiyo.
B) Tafuta ndugu upande wa mke ambaye mkeo anamweshimu sana,mpasulie ukweli kuwa umezaa na huyo mdada,mwombe akuite wewe na mkeo na kwenye kikao yeye ndo atamke yeye na sio wewe kisha mama watoto akikuhoji jibu 'ndiyo' halafu usiongee sana,be cool,akipandisha just stay quite ila akijitia kurusha ngumi mtandike maana si ruksa akunyanyulie mkono hata kama una kosa.
Katika hili aki pack na kuondoka kamwe usimfuate,its up to her kuamua kurudi au kuacha,nakuhakikishia atarudi,hujaua mtu aslan.
Always remember waume wa kwelituko wachache sana hapa mjini na hakuna mwanamme anaachwa siku hizi.
Najua it sounds arrogant ila ukweli i am advising by drawing on my deep experience ya ku deal na mama zetu hawa.

Nilitaka kupingana na wewe lakini kwa hiyo bold and blue SINA UBISHI HUO NDO USHAURI WA MAANA
 
Bishanga nimekupata sawia..............

Yangu ni haya..............

Wanawake siku hizi hatutishwi na wanaume hata kidogo...iwe kifedha or kimwili aka mapenzi, sijui ngono vyovyote utakavyoiita but let me tell you mleta mada..............UMEKWISHA TENDA hakuna jinsi ya kuzuia...........na nikwambie huyo mkeo utakapomwambia lazima roho itamuuma sana tena mno na kama hana stamina kidogo anaweza zimia............lakini je najiuliza akiondoka itakuwa imeondoa ukweli kwamba huna watoto?? Haiwezekani mwambie na tunza watoto wako reaction yake na impact za kutetereka kwa ndoa ni 100% hilo jiandae. Najiuliza mara mbili mbili ikiwa ungecheat na condom na asingejua ungekuwa hujacheat?? WANAUME WA KWELI SIKU HIZI HAKUNA JAMANI...........Ningekuwa mimi tena ningekwambia walete tukae nao usipate sababu ya kuwasiliana na mama yao.........tushawazoea wanaume nyie tunajua sana mnacheat lakini cheat salama wajameni hali mbaya mweehhhh Bishanga anajua namaanisha nini
 
i love sukuma men, they stand for their kids no matter what.

Ndoa ya kusambaratishwa kwa sababu ya watoto jua haikuwepo toka mwanzo.

Kongosho una hatari wewe...mambo mengine sio rahisi kuyatamka kama hivyo bila ya the lager
 
Dawa yao hawa ni hiyo tu,hata ukiharibu mtoto wa kiume gangamara,hawana pakwenda hawa,kwanza waoaji wako wapi in the first place,halafu watoto amwachie nani?

Hapa umekata stimu yangu ya Heineken kabisa hatuna pa kwenda tulitolewa porini kuwa na heshina na adabu kwa mama zako alah
 
paulss, pole sana na hongera kwa kukubali ukweli kwamba hao ni watoto wako. Jipange kuujulisha ulimwengu nini kilichojiri. Kutakuwa na madhara ila hakuna namna lazima maisha uyape mwelekeo unaostahili kwa kuwaingiza ndani na hao mapacha wako
 
Last edited by a moderator:
Vip lakini mkuu mechi ya ugenini taaaaamuuuu eeeh ila matunda yake ni kupachikwa mabao na wenyeji eeeeh bhana eeeh............
 
Eiyer nafurah sana kuona na wewe unajandaa kumshauri huyu mwenzetu.
kuna jambo ambalo limenikumbusha mbali sana kwa huyu mkaka in such a way natamani nimpe ushuhuda kidogo ambao i went through hose days.

niliwah kuwaambia kwamba mr alikuwa na mtoto wa mashtuzi, tofauti ni kwamba huyu nilimkuta na hakunikuta mimi. napenda nimshuhudie jinsi ambavyo mimi nililazimika kuiumba amani ya familia yangu kwa ishara ambayo niliiona nilipoambiwa.

kwakujua kwamba yule mtoto amani yake iko established kwa wazazi wake, na wazazi wake ndo hivo tena nilijipa nafasi ya mimi kuwa ni mwanangu na nkaasume yale ambayo ningependa ayapate hata kama mimi siishi na huyu baba mzazi wa huyu mtoto.

nilimwomba mume wangu amchukue aje alelewe hapa, kwani nilijua kwamba no matter what watahitaj kuhudumiwa na baba yao na ni bora nimlee mimi kuliko na mtu baki ili akue na wadogo zake. sikuishia hapo nilifikiria upande wa pili wa shilingi. huyu mama aliyezalishwa akiwa form two inamaana maisha kwake ndo yako hapo,atapika pombe za kienyeji hadi lini? na je kwanini baba aliyehusika hakurudi kupika pombe yeye aliendelea na shule? nikagundua kwamba kosa ni maumbile tu kwamba kwakua baba habebi mimba basi yeye yuko salama no mata kazini na wanawake wangapi.

hapa napo nikazidi kuwasha ari ili mtoto akakombolewe kutoka kwa mama yake, aletwe niishi nae mimi ili mama sasa aweze kujipanga afanye kazi akomboke kwenye maisha ya dhiki. nilifanikiwa katika hili na alipokuja mama alikuwa huru kuendeleza maisha. Miaka 2 baadae mambo yangu yalipokuwa afadhali nilimpa mama wa huyu mtoto mtaji afanyebiashara na namshukuru sana Mungu hadi leo hii huyu dada ni rafiki yangu wa dhati na huwa ni msaada sana kwangu hata kifedha.

so kama mke wa huyu kaka atawaza kwa undaani zaid pasi kuangalia yale ambayo wengi wetu tumezoea kuyasikia hakika hili tatizo laweza kuwa dogo sana na likatumika kama njia ya kumletea baraka. si lazimishi afanye kama mimi ila natoa ushuhuda wa maisha ya tofauti ambayo niliyapitia na ambayo wengi walyawazia kinyume.

ila pia lazima binti aliyezalishwa aelezwe ukweli kwamba kuna mke halali wa ndoa na yeye ni mzazi tu hawez kuwa mke. na mkimsaidia ajitegemee kamwe hatakuwa burden kwenu ila mkimtenga atawapa shida sana.

Mamii ilikuwa rahisi kwa kuwa huyo mtoto ulimkuta to be frank nizungumze nikiwa ni mwanamke ni ngumu sana kukubali kulea mtoto aliyekukuta.maana kupitia kwake unauona uovu wa mumeo,kupitia kwake unjiona labda pengine kuna sehemu hukukamilika,kupitia kwake unazidi kujihisi una mapungufu si unajua siye wanawake tunavokimbilia kujilaumu katika kila makosa ya waume zetu,so please tusilinganishe mtoto wa nje ya ndoa na mtoto wa kabla ya ndoa hawa ni watoto tofaut KABISA,na justification zake pia ni tofauti,mimi mume wangu aniletee hata watoto kumi ambao aliwapata kabla ya kunijua mimi nitawalea maana inawezekana mimi ndiye sababu ya mama yao kuachwa,lakini walio chini ya umri wa ndoa yangu please!mwanaume anapaswa kuwa na busara sana tena sana PLUS MAOMBI!vinginevyo akiendekeza zile za kidume dume za "HAYAISHI,YANI BADO UMEKASIRIKA TU,MKE WANGU SI UNISAMEHE,MBONA HATA KAKA NAE ANA MTTOT MWINGINE NA HAJAMWAMBIA MKEWE SI BORA MI NIMESEMA,!''mambo yanaweza kuwa mabaya sana.nimejaribu kuvaa viatu vya huyo mke though najua siwezi kuimagine atareact vipi!
 
Nafikiri kama dhambi ya uzinzi ingekuwa na namba, wanaume wangekosa namba ya kupewamaana maana wangescore zaidi ya namba zilizopo kwenye hesabu. Kaka, Biblia inatufundisha kuwa utaijua kweli, na hiyo kweli itakuweka huru. Kweli ni neno la Mungu. tunafundiswa kusema kweli kila mtu na mwenzake, mwambie mkeo ukweli, cha muhimi, ujue kuwa atakasirika, hata kufikiri kuondoka, jipange tu kumuelewesha, kumbembeleza na kuomba msamaha. baada ya muda atakusamehe, ila ujue KUWA HATAKAA AKUAMINI TENA! Usiogope, kutokuaminiwa na mkeo sio kosa kubwa ukilinganisha na kutelekeza watoto wako wa nje, yaweza kuwaletea mikosi watoto wako wa ndani, na hayo mapenzi unayohangaikia yakaingia mkenge.
 
Bishanga nimekupata sawia..............

Yangu ni haya..............

Wanawake siku hizi hatutishwi na wanaume hata kidogo...iwe kifedha or kimwili aka mapenzi, sijui ngono vyovyote utakavyoiita but let me tell you mleta mada..............UMEKWISHA TENDA hakuna jinsi ya kuzuia...........na nikwambie huyo mkeo utakapomwambia lazima roho itamuuma sana tena mno na kama hana stamina kidogo anaweza zimia............lakini je najiuliza akiondoka itakuwa imeondoa ukweli kwamba huna watoto?? Haiwezekani mwambie na tunza watoto wako reaction yake na impact za kutetereka kwa ndoa ni 100% hilo jiandae. Najiuliza mara mbili mbili ikiwa ungecheat na condom na asingejua ungekuwa hujacheat?? WANAUME WA KWELI SIKU HIZI HAKUNA JAMANI...........Ningekuwa mimi tena ningekwambia walete tukae nao usipate sababu ya kuwasiliana na mama yao.........tushawazoea wanaume nyie tunajua sana mnacheat lakini cheat salama wajameni hali mbaya mweehhhh Bishanga anajua namaanisha nini

Unacheza karate nini? Nikikuona nitimue mbio
 
Vip lakini mkuu mechi ya ugenini taaaaamuuuu eeeh ila matunda yake ni kupachikwa mabao na wenyeji eeeeh bhana eeeh............

Kimbweka mtu haachi asili....umetokaje kule kwenye jukwaa letu leo?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom