Najuta nimezaa nje ya ndoa, ushauri wako muhimu sana

Najuta nimezaa nje ya ndoa, ushauri wako muhimu sana

Its so touching mkuu, ulivyoitoa hata me naweza kufeel ni kwa kiasi gani unasumbuka. Nadhani ingekuwa vizuri utafute namna ya kumweleza mkeo wa ndoa hata kama utatumia muda mrefu SANA kufikisha ujumbe. Akikuelewa basi mshukuru Mungu na baada ya hapo nenda kule kijijini ucheki namna ya kuwaingia wakwe wako wa kufikia. But ni ngumu sana mkuu kulimaliza hilo, nionavyo mie, ukweli utakuweka huru, na ukificha maradhi, kifo kitakuumbua. Kumbuka, maisha ya toba yatakufanya uwe huru na ile kama ni damu yako usiiache! Truth will set you free!!!!!
 
mara nyingi sana
binadamu tunakuwa na kawaida ya kuona 'matatizo' yetu kama makuubwa sana

kumbe wapi....


ni madogo mno.......ukiyakubali na kuyachukulia kuwa ni madogo

Ongea na mkeo taratiibu
nenda nae kwa step......

1. hatua ya kwanza mwambie kuwa ulitoka nje.....na uombe msamaha

2.hatua ya pili jifanye huna uhakika kuwa huyo binti alizaa watoto wako au la
unataka ku find out

3.hatua ya tatu....unamwambia intention yako ya 'kulea watoto kama ukithiitisha ni wako'

Kaka, hili tatizo siyo rahisi kihivyo. Hapa nikijivisha viatu vya mkuu paulss....nahisi kutetemeka (na umri wangu huu), kwani sijui huyu bibi angelipukaje....

Hata hivyo, nakubaliana na wewe + wadau wengine kwamba hawezi kuendelea kuficha kwani ni hatari sana...Hivi yakimfika makubwa kama kifo leo hii, hao watoto atawaacha katika mazingira gani??

Hapa akubali kuwa...LIWALO NA LIWE!!!

Babu DC!!
 
Nafikiri ni vyema kumueleza huyo binti uliyezaa naye nje UKWELI kuwa wewe ni mume wa mtu na unafamilia na ulifanya hako kamchezo na haukutegemea kama ungeweza kuzaa naye. Lakini hata hivyo, upo tayari kutunza watoto wako na huna mpango wa kuishi naye yeye (huyo binti) na hivyo awe huru kuolewe na yeyote. Na ni vizuri hata hao ndugu wa huyo binti wafahamu hivyo mapema ili wasiendelee kuwa na ndoto za binti yao kuolewa nawe. Si haki mkeo na familia yako ije iteseke kwa uzembe wako mwenyewe!

Kwa upande wa mkeo mwambie ukweli kuwa ulizaa nje bahati mbaya. Unaweza kutafuta wasaa mzuri na kumwambie kwa busara ili kupunga madhara yanayoweza kujitokeza baada ya mkeo kupata hizo taarifa. Kwa kuwa tatizo limetokea naamini anaweza kukusamehe na mkaendelea na maisha.

Zingatia pia aliyoyanena The Boss ni muhimu pia.
Pole mkuu
 
Kongosho, mateka akikimbia usinililie, manake una jibu maswali ya mtego.
umejuaje details za huyu accidental father of twins?
 
Last edited by a moderator:
oops, hivi kumbe nimejua details zake? Ulikuwa mfano tu.


Akikimbia ujue sio mateka tena bali ni mfungwa huria 🙂

Kongosho, mateka akikimbia usinililie, manake una jibu maswali ya mtego.
umejuaje details za huyu accidental father of twins?
 
Last edited by a moderator:
mpaka dakika hii natafuta kinachokuchanganya sikioni kwa kweli.

Sioni kwa nini hujasema kwa mkeo, kwani akikasirika kwa mwezi atakufa?? Au ana magonjwa ya moyo??

Je ungerudi na VVU usingesema ili mnywe dawa wote???

Kwa nini mnapenda kuwafanya watoto victims wa mambo yenu?? Na ungejua mapema si ajabu ungesema atoe mimba???

nimegundua wanamme wanzidi kupotea katika kizazi hiki.

Mkuu huoni tatizo kweli? Nadhani hapa kinachonitatizo ni kuheshimu hisia za mwenzako pia
Hebu pata picha mkeo anakwambia mtoto wa pili wa ndoa yenu ni wa rafiki yako, unaweza kuichukulia rahisi kama unavyosema watoto wamekuwa victim?

Hata hivyo nimependa ushauri mkuu ingawa namjua mke wangu vizuri na ugumu wa kulipoke hili
Bado nasoma ushauri wa wadau
Thanx
 
mara nyingi sana
binadamu tunakuwa na kawaida ya kuona 'matatizo' yetu kama makuubwa sana

kumbe wapi....


ni madogo mno.......ukiyakubali na kuyachukulia kuwa ni madogo

Ongea na mkeo taratiibu
nenda nae kwa step......

1. hatua ya kwanza mwambie kuwa ulitoka nje.....na uombe msamaha

2.hatua ya pili jifanye huna uhakika kuwa huyo binti alizaa watoto wako au la
unataka ku find out

3.hatua ya tatu....unamwambia intention yako ya 'kulea watoto kama ukithiitisha ni wako'

Big up kamanda. Ushauri huu ndo wa kufanyia kazi
 
Nimeishiwa na maneno,ila ukiwaacha hao watoto wakateseka hao watoto wako wawili wandoa hawatafanikiwa,potelea mbali wamjue baba wasimjue ila hakikisha wanapata matunzo mazuri kabisa,na sidhani kama mkeo atakuwa tayari kuwalea ukilazimishwa kuwachukua wapeleke kwa bibi yao,nirahisi kuwatunza hata kama huna kitu ila hapo kwa wazazi wa binti watakufanya chumaulete othewise kama wana kipato kidogo,huuni ku alizia tu pakuanzia wadau washasema.ila pole sana
 
Paulss, unajali hisia za mke wako, ni kweli ni vizuri kujali hisia za mke.

Je hisia za watoto? Achia mbali haki yao ya kumwona baba??

Je huyo mwanamke mwingine, ana jiwe kifuani?? Unadhani hana hisia kabisa sababu tu si mke?? Zingatia kuwa watoto wanafanya mahusiano yasipotee.

Hapa suala la hisia sioni kama ni priority tena maana mambo yashaharibika.

Hapa ni kufanya 'the right thing kwa kutumia right ways'

kumwambia mkeo haiepukiki, ya nini watoto wakutane siku ya msiba wa mzazi wawe rivals kwenye mali??

Siombei hili, imagine linatokea balaa kwa watoto wako utalia kimya kimya? Utaenda waliko kuonesha msibani??
Na ukienda msibani what for?? Unamkubali akiwa si hai wakati ulimkataa akiwa hai??

Sema mapema, tena sana na ikibidi baada ya muda mrefu watoto hao wawe wanakuja kwako ili wasionane kama maadui bali watu wa familia moja.
 
Wala usiumie sana baba sio mtu muhimu sana kwenye malezi ya watoto wengi tunaojua ni bb zetu sio wenyewe
 
chukua jukumu kamili mdau!
mwambie mkeo, mtoto wa nje si dhambi, dhambi ni kumTOA au kumKATAA.
Sio tu kulea mwanao. Kajitambulishe kwa mwanao na wazazi wa binti wakujue.
Kisha weka msimamo wako kwa binti, kila mtu achukue njia yake, si una mke bana??
 
Mume wangu kwanini umenisaliti,Ni kipi ulichokosa kwangu?roho inaniuma sana,nimeishi na wewe kwa upendo wangu wote,Nimejiheshimu na kuutunza mwili wangu kwa ajili yako,Sikutegemea kuwa kuna siku ungenisaliti,Nashukuru sana kwa uliyonitendea.
 
Mungu aepushie mbali. Najaribu kupiga picha camera imegoma kabisa. Subiri wenye watoto wa nje wanaweza kuwa washauri wazuri. Maana kuijua ngoma mpaka uingie ucheze. Pole sana.

hahaha! nyumba kubwa .. lakini unakubali maneno ya hii picha ....



tumblr_lj0wwoXfoX1qes1ceo1_500.jpg



paulss kitanda umechonga .. godoro ukanunua na shuka ukatandika sasa waogopa kulala..?!
 
Mkuu pole sana lakini hongera kwa kuonyesha moyo wa kukubali jukumu lako kwa wengi hata wakijua wanaingia mitini, cha muhimu wewe ndiyo unamjua mkeo vizuri ukiona atashinwa kukubali basi wewe tafuta ndugu wa karibu yako mweleze yaliyokusibu ili mjue (wewe na huyo ndugu yako) jinsi ya kulitatua sababu hakuna linaloshindikani hapa duniani.
 
Paulss, unajali hisia za mke wako, ni kweli ni vizuri kujali hisia za mke.

Je hisia za watoto? Achia mbali haki yao ya kumwona baba??

Je huyo mwanamke mwingine, ana jiwe kifuani?? Unadhani hana hisia kabisa sababu tu si mke?? Zingatia kuwa watoto wanafanya mahusiano yasipotee.

Hapa suala la hisia sioni kama ni priority tena maana mambo yashaharibika.

Hapa ni kufanya 'the right thing kwa kutumia right ways'

kumwambia mkeo haiepukiki, ya nini watoto wakutane siku ya msiba wa mzazi wawe rivals kwenye mali??

Siombei hili, imagine linatokea balaa kwa watoto wako utalia kimya kimya? Utaenda waliko kuonesha msibani??
Na ukienda msibani what for?? Unamkubali akiwa si hai wakati ulimkataa akiwa hai??

Sema mapema, tena sana na ikibidi baada ya muda mrefu watoto hao wawe wanakuja kwako ili wasionane kama maadui bali watu wa familia moja.

Mkuu sasa tupo pamoja, hisia nilizokuwa nazungumzia ndio hizo hasa ulizozitaja, kuhofia kumuumiza mkewangu wakati nawaumiza watoto na wanaowalea
Nilifikiri kutuma matumizi tu ingetosha but I was wrong.

So I'm here trying to find the right way to handle this
 
Muambie mkeo huku ukionesha hali ya kujutia ili uwe huru kuwasaidia wanao kuficha siri ni kujipunguzia raha ya maisha.
Ila hongera kaka kwa kuwa na mkojo mkali khaa hadi wametoka Mapacha tena wanafanana na wewe.
 
Afu hao watoto wawe wa kiume na mkeo ana watoto wa kike tu mziki utazidi kuwa mkubwa. Kuna mama mmoja mmewe alizaa baby boy nje...yani nyumba iligeuka vurugu mechi mama anasema hawezi tena kufanya investments na mumewe kwa kuwa yeye ana watoto wa kike huyo wa nje atakuja kuwapora mali bintize wazazi wakifa. Patamu.

Na kweli kuna wanaume uandikia urithi watoto wao wa nje huku walichuma na wake zao.
 
Mkuu kwanza nikupongeze kwa kupata mapacha kwa mujibu wa story yako!I love twins!...
Cha kufanya umwambie mkeo ukweli ila huo ukweli unatakiwa kuchanganya na ka uwongo kidogo!mfano mwambie yf ulivo kwenda bush kuna siku ulikunywa pombe bahati mbaya ilikutuma ulio yafanya!ila wakati huo unatakiwa uwe una eleza kwa hisia kali huku neno am sorry halitoki!
Then nenda zako church ukatuwe zigo kwa kuungama baada ya hapo nenda bush mtafute yule binti mwambie ukweli kwamba huna time nae ila watoto na kama vipi mpatie kimtaji kama njia ya kumpoza,ila hapa usikubali atoke hadi akuelewe!Halafu nenda sasa katafute mzee/wazee wenye busara zao wakalishe.
Kila la kheri mkuu ila kabebe mapacha wangu tafadhali....
 
Back
Top Bottom