Nakasirishwa na unafiki wa viongozi wetu

Nakasirishwa na unafiki wa viongozi wetu

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Wananchi tunafanya kazi kwa bidii na tunapenda haki lakini viongozi wetu hawaonyeshi kuwa na nia ya kututetea wametuacha katika mazingira duni hawatusaidii kuboresha hali zetu na ndio sababu miaka ya nyuma watu walikuwa wanajiunga na migomo.

Viongozi wetu (wa kisiasa na dini) wanaishi maisha ya anasa lakini bado wanatuomba chakula na pesa ilihali sisi nako tunapambana tupate mahitaji yetu ya kila siku.

Mambo ni mengi na ya ajabu yanashangaza sana. Mtu ana uwezo lakini bado anaongezewa anasa. Sio haki hata kidogo. Ni bora kama mtu ana mshahara na maisha mazuri basi hizo pesa ikafanyie Jambo lingine kusaidia masikini.

Pima mara mbili kata mara moja ili kuhakikisha lililo jema na lenye hekima kati ya Benz moja la rais mstaafu au kujenga masoko ya kisasa katika tarafa 5.
 
Yaan raia mstaafu kupewa gari ya 450 m ilioni imekuwa nongwa?

Mbona hiyo zawadi ndogo kwa mtu wa cheo hicho?
 
Nyumba tayari
Gari tayari..ila nashauri
Aongezewe jingine la kwendea
Shamba,hawa viongozi wametutumikia
Sana

Ova
 
Nchi hii hakuna mwanasiasa mwenye nia ya dhati ya kusaidia watanzania. Kila mtu mpigaji, hata na wale waliojifanya kuwa wasaidizi wa mwendazake wanafiki watupu. Mungu yupo nasi, hakika tutafika salama.
 
Yaan raia mstaafu kupewa gari ya 450 m ilioni imekuwa nongwa?

Mbona hiyo zawadi ndogo kwa mtu wa cheo hicho?
Kila mwezi anapata 80% ya mshahara wa Rais aliyemadarakai pamoja na marupurupu kibao. Wangekuwa wanaguswa kwa haraka hivyo kwenye maisha yetu huku mtaani, basi naamini katika miaka 60 ya Uhuru kimoja kati ya Maji, Elimu, Afya kingekuwa bora na mfano Afrika yote.
 
Nchi hii hakuna mwanasiasa mwenye nia ya dhati ya kusaidia watanzania. Kila mtu mpigaji, hata na wale waliojifanya kuwa wasaidizi wa mwendazake wanafiki watupu. Mungu yupo nasi, hakika tutafika salama.
Ni kweli.
 
Ndio ccm unayotawala tangu Uhuru. Sisi tukisema mnasema Bavicha hawa! Ongeeni nyie basi.

Huu moto utamuunguza kila mtu.

Mtu kama Mwinyi alikuwa waziri, akawa Rais, mwanae ni Rais na kama ilivyo kwa maraia wa Afrika Hawana cha kuwatumikia Raia wao bali Raia huwatumikia Ma Rais. Kuendelea kumpa mali za serikali za umma eti unamjengea nyumba na magali wakati anayo mengi na anaweza kununua na mengine inafikirisha sana.

Kumbe hawa viongozi wanaongea tu. Lao ni moja.
 
Yaan raia mstaafu kupewa gari ya 450 m ilioni imekuwa nongwa?

Mbona hiyo zawadi ndogo kwa mtu wa cheo hicho?
Kwani wealth aliyonayo we unaona anahitaji hiyo 450M. Huku unasema tudunge mkanda wakati Baba unalala Bar?
 
Back
Top Bottom