Nakinzana na wanaotaka tuite Amirati Jeshi Mkuu badala ya Amiri Jeshi Mkuu

Nakinzana na wanaotaka tuite Amirati Jeshi Mkuu badala ya Amiri Jeshi Mkuu

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2016
Posts
520
Reaction score
2,930
Nimeona Mjadala sehemu kwamba tubadili tuite Amirat badala ya Amir, sababu amir ni kwa mwanaume na Amirat ni kwa mwanamke. Kwamba Mh. Rais, Samia Suluhu Hassan tumuite Amirati Jeshi Mkuu.

Nina kinzana na wanaotoa hoja ya kuita Amirati badala ya Amiri, mbali na hoja ya kikatiba ibara ya 33 (2) inayo mtambua Rais Kama kiongozi wa nchi, kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu, naomba nijadili suala hili kwa minajili ya kilugha tuu Kama linavyohojiwa na kujadiliwa kwa minajili ya kilugha.

Amir / Ameer ni neno la kiaribu kweli likiwa limelenga mwanaume kiongozi “leader”, Kamanda “commander”, Mtawala “ruler”, au chifu “chief”,.

Neno hili limetokana na neno la kiarabu A-M-R.(Kuamrisha au to command).

Neno hili ni la Kiarabu, ila katika lugha yetu ya kiswahili tumelitohoa na kulitumia yaani tumelikopa na kuwa "Amiri" .Yaani ni neno mkopo.

Neno mkopo ni kipengele cha kileksika kutoka lugha chagizi kinachoingizwa katika lugha pokezi ili kiweze kutumika kama neno rasmi la lugha pokezi, mara nyingi huweza kufanyiwa marekebisho au mabadiliko maalumu ya kifonolojia/kimofolojia aidha upande wa sauti,Silabi au irabu ili kukidhi mahitaji au maana ya msingi inayokuzudiwa katika lugha pokezi.

Katika dhana ya neno Ameer ,Amir lugha changizi ni kiarabu ,Lugha pokezi ni Kiswahili.

Tulivyochukua neno Ameer ,Amir kutoka lugha chagizi ya kiarabu tuliongeza irabu ktk lugha yetu Amir, tukaongeza i (Amiri) .

Pia tulibeba maana ya msingi "Kamanda" na bila kujali kamanda huyo awe wa kike au wakiume, sisi tuliangalia maana zaidi bila kuangalia linatumika kwa Jinsia gani. Na sisi tukalitumia kama Amiri Jeshi Mkuu tukiwa na maana Commander in Chief (C in C).

Tukisema tuangalie kubadili kuita Amirat ,kwa kubadili maana kwamba Sasa hivi aliyeshika madaraka ni mwanamke,tutaleta mchanganyiko sana ,Amirat hiyo ina maana nyingi sana Amirat ina maana ya kiongozi ,wengine Amirat hujulikana Kama First lady (Yaani Mke wa Rais ) , Princess (Binti Mfalme.

Sasa ili tumuite Amirat itatupaswa kutohoa neno hilo kutoka ktk kiarabu na kulipa maana mahususi kulingana na muktadha wa sasa ,sababu neno hilo lina maana nyingi ,hivyo maana rasmi itafanya watumiaji wajue kwanini tunatumia Amirat ,sawa na sasa hakuna maana zaidi ya kutumia Amiri zaidi ya neno "Kamanda " bila kujali jinsia aidha wa kike au kiume.

IMG_20210324_161001_925.jpg
 
Sasa u apinga wenye lugha Yao?

Imeandikwa vizuri,amir ni kuongozi wa kiume kwa kiarabu amirat ni wa kike, tatizo liko wapi.

Kumuita amir au vinginevyo ni maamuzi yetu

Tunaweza acha Hilo memo tukaita tu, mkuu majeshi yote y ulinzi na usalama Tanzania.
 
Jamani mbona ni rahisi tu AMIRI KIONGOZI wa kiumbe na KIONGOZI wa kike anaitwa. AMIRA JESHI MKUU .AMIRAT HERUFI YA MWISHO HAISOMEKAGI T.HIVYO HaItakuwa vibaya kuita AMIRA.
 
Sasa u apinga wenye lugha Yao?

Imeandikwa vizuri,amir ni kuongozi wa kiume kwa kiarabu amirat ni wa kike, tatizo liko wapi.

Kumuita amir au vinginevyo ni maamuzi yetu

Tunaweza acha Hilo memo tukaita tu, mkuu majeshi yote y ulinzi na usalama Tanzania.
Mwalimu (mualim - mwalimu wa kiumbe) nalo linatokana na kiarabu, mualimatu (mwalimu wa kike).

Meza ni Kireno ikiwa na maana hiyo kwa umoja, wingi wake kwa Kireno ni MEZAS je nasi tuseme hivyo?

Na mifano mingi tu....
 
Kwa mkutadha huo, nashauri tuite tu Mkuuu wa Majeshi.
Nimeona Mjadala sehemu kwamba tubadili tuite Amirat badala ya Amir ,sababu amir ni kwa mwanaume na Amirat ni kwa mwanamke. Kwamba Mh.Rais,Samia Suluhu Hassan tumuite Amirati Jeshi Mkuu.

Nina kinzana na wanaotoa hoja ya kuita Amirati badala ya Amiri ,mbali na hoja ya kikatiba ibara ya 33 (2) inayo mtambua Rais Kama kiongozi wa nchi , kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu ,naomba nijadili suala hili kwa minajili ya kilugha tuu Kama linavyohojiwa na kujadiliwa kwa minajili ya kilugha.

Amir / Ameer ni neno la kiaribu kweli likiwa limelenga mwanaume kiongozi “leader”,Kamanda “commander”, Mtawala “ruler”, au chifu “chief”,.

Neno hili limetokana na neno la kiarabu A-M-R.(Kuamrisha au to command).

Neno hili ni la kiarabu, ila katika lugha yetu ya kiswahili tumelitohoa na kulitumia yaani tumelikopa na kuwa "Amiri" .Yaani ni neno mkopo .

Neno mkopo ni kipengele cha kileksika kutoka lugha chagizi kinachoingizwa katika lugha pokezi ili kiweze kutumika kama neno rasmi la lugha pokezi ,mara nyingi huweza kufanyiwa marekebisho au mabadiliko maalumu ya kifonolojia/kimofolojia aidha upande wa sauti,Silabi au irabu ili kukidhi mahitaji au maana ya msingi inayokuzudiwa katika lugha pokezi.

Katika dhana ya neno Ameer ,Amir lugha changizi ni kiarabu ,Lugha pokezi ni Kiswahili.

Tulivyochukua neno Ameer ,Amir kutoka lugha chagizi ya kiarabu tuliongeza irabu ktk lugha yetu Amir ,tukaongeza i (Amiri) .

Pia tulibeba maana ya msingi "Kamanda " na bila kujali kamanda huyo awe wa kike au wakiume ,sisi tuliangalia maana zaidi bila kuangalia linatumika kwa Jinsia gani. Na sisi tukalitumia kama Amiri Jeshi Mkuu tukiwa na maana Commander in Chief (C in C).

Tukisema tuangalie kubadili kuita Amirat ,kwa kubadili maana kwamba Sasa hivi aliyeshika madaraka ni mwanamke,tutaleta mchanganyiko sana ,Amirat hiyo ina maana nyingi sana Amirat ina maana ya kiongozi ,wengine Amirat hujulikana Kama First lady (Yaani Mke wa Rais ) , Princess (Binti Mfalme.

Sasa ili tumuite Amirat itatupaswa kutohoa neno hilo kutoka ktk kiarabu na kulipa maana mahususi kulingana na muktadha wa sasa ,sababu neno hilo lina maana nyingi ,hivyo maana rasmi itafanya watumiaji wajue kwanini tunatumia Amirat ,sawa na sasa hakuna maana zaidi ya kutumia Amiri zaidi ya neno "Kamanda " bila kujali jinsia aidha wa kike au kiume.View attachment 1733410
 
Mwalimu (mualim - mwalimu wa kiumbe)....nalo linatokana na kiarabu, mualimatu (mwalimu wa kike).
Meza ni Kireno ikiwa na maana hiyo kwa umoja, wingi wake kwa Kireno ni MEZAS je nasi tuseme hivyo?
Na mifano mingi tu ....
Chairman/ chairperson kwenye dulu za sheria ikoje Kuhusu matumizi za jinsia?
 
Pia kiswahili hakina structure ya feminine na masculine forms. Isipokua kwenye maeneo mahususi kama mama na baba.

She/He - yeye
Waitress/Waiter - Mhudumu
Lion/Lioness - Simba

Kwahiyo rais awe wa kike au kiume atabaki kuwa Amiri jeshi tu.

Ngurumo huyo na mauongo yake ndio kaleta hizo story, na watu wameziparamia kichwa kichwa.
 
Ukisikia "mfumo dume", hii ndo maana yake! Kila kitu tunakitizama kimrengo wa kiume. Mathalani, mmoja akisema "mtu mrefu amepita nje", moja kwa moja mpokeaji wa taarifa hiyo atawaza huyo "mtu mrefu" ni mwanamume na si vinginevyo.

Kwa mantiki hiyo katiba yetu haitambui rais anaweza kuwa mwanamke ndio maana limetumika neno "amiri" na kusahau "amira".
 
kiufupi zipo lugha zinazotambua utofauti wa jinsia katika maneno ila kiswahili ni miongoni mwa lugha zisizotofautisha jinsia. Hivyo huyo ni Amiri Jeshi Mkuu
 
Sasa u apinga wenye lugha Yao?
Imeandikwa vizuri,amir ni kuongozi wa kiume kwa kiarabu amirat ni wa kike,tatizo liko wapi.
Kumuita amir au vinginevyo ni maamuzi yetu
Tunaweza acha Hilo memo tukaita tu,mkuu majeshi yote y ulinzi na usalama Tanzania.
Sisi sio waarab japo lugha ya kiswahili ina mchanganyiko wa lugha mbalimbali..ni bora akapewa heshima yake kwa jinsi Jeshi litakavyobainisha baada ya kufanya taratibu zao kubainisha atambulishwe kwa jina gani..Nyie waarab acheni kutusumbua.. Endapo akiitwa MKUU WA NCHI NA MAJESHI MAMA SAMIA SULUHU HASSAN sidhani kama kuna shida na itafaaa zaidi kuliko kukumbatia mabeberu wa Ulaya na Asia.
 
Nimeona Mjadala sehemu kwamba tubadili tuite Amirat badala ya Amir ,sababu amir ni kwa mwanaume na Amirat ni kwa mwanamke. Kwamba Mh.Rais,Samia Suluhu Hassan tumuite Amirati Jeshi Mkuu.

Nina kinzana na wanaotoa hoja ya kuita Amirati badala ya Amiri ,mbali na hoja ya kikatiba ibara ya 33 (2) inayo mtambua Rais Kama kiongozi wa nchi , kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu ,naomba nijadili suala hili kwa minajili ya kilugha tuu Kama linavyohojiwa na kujadiliwa kwa minajili ya kilugha.

Amir / Ameer ni neno la kiaribu kweli likiwa limelenga mwanaume kiongozi “leader”,Kamanda “commander”, Mtawala “ruler”, au chifu “chief”,.

Neno hili limetokana na neno la kiarabu A-M-R.(Kuamrisha au to command).

Neno hili ni la kiarabu, ila katika lugha yetu ya kiswahili tumelitohoa na kulitumia yaani tumelikopa na kuwa "Amiri" .Yaani ni neno mkopo .

Neno mkopo ni kipengele cha kileksika kutoka lugha chagizi kinachoingizwa katika lugha pokezi ili kiweze kutumika kama neno rasmi la lugha pokezi ,mara nyingi huweza kufanyiwa marekebisho au mabadiliko maalumu ya kifonolojia/kimofolojia aidha upande wa sauti,Silabi au irabu ili kukidhi mahitaji au maana ya msingi inayokuzudiwa katika lugha pokezi.

Katika dhana ya neno Ameer ,Amir lugha changizi ni kiarabu ,Lugha pokezi ni Kiswahili.

Tulivyochukua neno Ameer ,Amir kutoka lugha chagizi ya kiarabu tuliongeza irabu ktk lugha yetu Amir ,tukaongeza i (Amiri) .

Pia tulibeba maana ya msingi "Kamanda " na bila kujali kamanda huyo awe wa kike au wakiume ,sisi tuliangalia maana zaidi bila kuangalia linatumika kwa Jinsia gani. Na sisi tukalitumia kama Amiri Jeshi Mkuu tukiwa na maana Commander in Chief (C in C).

Tukisema tuangalie kubadili kuita Amirat ,kwa kubadili maana kwamba Sasa hivi aliyeshika madaraka ni mwanamke,tutaleta mchanganyiko sana ,Amirat hiyo ina maana nyingi sana Amirat ina maana ya kiongozi ,wengine Amirat hujulikana Kama First lady (Yaani Mke wa Rais ) , Princess (Binti Mfalme.

Sasa ili tumuite Amirat itatupaswa kutohoa neno hilo kutoka ktk kiarabu na kulipa maana mahususi kulingana na muktadha wa sasa ,sababu neno hilo lina maana nyingi ,hivyo maana rasmi itafanya watumiaji wajue kwanini tunatumia Amirat ,sawa na sasa hakuna maana zaidi ya kutumia Amiri zaidi ya neno "Kamanda " bila kujali jinsia aidha wa kike au kiume.View attachment 1733410
Ebu na wewe kuwa mwelewa, huyu haitwi AMIR (kiarabu), anaitwa AMIRI (kiswahili) Sasa hayo uliyoandika kuwa ni Amir ambalo ni kiarabu uko sahihi sisi hatutumii kiarabu kwahiyo hakukuwa na haja ya kuandika hayo uliyoandika.
 
Ukisikia "mfumo dume", hii ndo maana yake! Kila kitu tunakitizama kimrengo wa kiume. Mathalani, mmoja akisema "mtu mrefu amepita nje", moja kwa moja mpokeaji wa taarifa hiyo atawaza huyo "mtu mrefu" ni mwanamume na si vinginevyo.

Kwa mantiki hiyo katiba yetu haitambui rais anaweza kuwa mwanamke ndio maana limetumika neno "amiri" na kusahau "am
Kama ungesoma lugha ya kiswahili ungeelewa kwamba lugha yetu haina maneno ya feminine na masculine, ipo neutral neno moja laweza kutumika kwa jinsia zote tofauti na lugha kama kifaransa au kimasai. Masai hata salamu ya mwanamke ni tofauti na salamu ya mwanaume na ya kijana kwa mzee kila kitu lugha yao imechambua na hii akisalimia hata kama humuoni unajua Nani anaongea na nani hii haihusiani na haya Mambo yenu ya mfumo jike au dume au sijui mfumo gani . Hii ni ukomavu wa lugha. Kifaransa ni lugha ya siku nyingi sana nadhani kiingeleza kimechukua maneno mengi kwenye kifaransa. So ni ukomavu wa lugha tu haihusiani na haya Mambo yenu ya mifumo.
 
Nimeona Mjadala sehemu kwamba tubadili tuite Amirat badala ya Amir ,sababu amir ni kwa mwanaume na Amirat ni kwa mwanamke. Kwamba Mh.Rais,Samia Suluhu Hassan tumuite Amirati Jeshi Mkuu.

Nina kinzana na wanaotoa hoja ya kuita Amirati badala ya Amiri ,mbali na hoja ya kikatiba ibara ya 33 (2) inayo mtambua Rais Kama kiongozi wa nchi , kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu ,naomba nijadili suala hili kwa minajili ya kilugha tuu Kama linavyohojiwa na kujadiliwa kwa minajili ya kilugha.

Amir / Ameer ni neno la kiaribu kweli likiwa limelenga mwanaume kiongozi “leader”,Kamanda “commander”, Mtawala “ruler”, au chifu “chief”,.

Neno hili limetokana na neno la kiarabu A-M-R.(Kuamrisha au to command).

Neno hili ni la kiarabu, ila katika lugha yetu ya kiswahili tumelitohoa na kulitumia yaani tumelikopa na kuwa "Amiri" .Yaani ni neno mkopo .

Neno mkopo ni kipengele cha kileksika kutoka lugha chagizi kinachoingizwa katika lugha pokezi ili kiweze kutumika kama neno rasmi la lugha pokezi ,mara nyingi huweza kufanyiwa marekebisho au mabadiliko maalumu ya kifonolojia/kimofolojia aidha upande wa sauti,Silabi au irabu ili kukidhi mahitaji au maana ya msingi inayokuzudiwa katika lugha pokezi.

Katika dhana ya neno Ameer ,Amir lugha changizi ni kiarabu ,Lugha pokezi ni Kiswahili.

Tulivyochukua neno Ameer ,Amir kutoka lugha chagizi ya kiarabu tuliongeza irabu ktk lugha yetu Amir ,tukaongeza i (Amiri) .

Pia tulibeba maana ya msingi "Kamanda " na bila kujali kamanda huyo awe wa kike au wakiume ,sisi tuliangalia maana zaidi bila kuangalia linatumika kwa Jinsia gani. Na sisi tukalitumia kama Amiri Jeshi Mkuu tukiwa na maana Commander in Chief (C in C).

Tukisema tuangalie kubadili kuita Amirat ,kwa kubadili maana kwamba Sasa hivi aliyeshika madaraka ni mwanamke,tutaleta mchanganyiko sana ,Amirat hiyo ina maana nyingi sana Amirat ina maana ya kiongozi ,wengine Amirat hujulikana Kama First lady (Yaani Mke wa Rais ) , Princess (Binti Mfalme.

Sasa ili tumuite Amirat itatupaswa kutohoa neno hilo kutoka ktk kiarabu na kulipa maana mahususi kulingana na muktadha wa sasa ,sababu neno hilo lina maana nyingi ,hivyo maana rasmi itafanya watumiaji wajue kwanini tunatumia Amirat ,sawa na sasa hakuna maana zaidi ya kutumia Amiri zaidi ya neno "Kamanda " bila kujali jinsia aidha wa kike au kiume.View attachment 1733410
Wewe Muha acha kuzungumzia ubishi wenu wa kiha hapa! Kama kiongozi wa vijana huko ACT Wazalendo kuna mengi ya kujadili sio huo ujinga wa maneno ya kiarabu au kimvita kumuita Rais. Wapo Bakita na wataalamu wengine wa lugha watajua wasemeje.
Acha ujinga bwana!
 
Back
Top Bottom