Nakuchukia Baba yangu

Nakuchukia Baba yangu

Wakuu,

Nimelelewa na mama yangu kwa asilimia 90 mpaka hapa nilipo.

Baba yangu aliondoka nyumbani mwaka 2011 akamuacha mama yangu akiwa amejifungua wiki mbili akaenda kusikojulikana na mwanamke mwingine, akatuacha hakuna chakula wala matumizi yoyote ya mama na sisi wanafunzi, Ilibidi mama aanze vibarua ili tule na tusome mimi na dada yangu ninaemfuata.

Hata sisi tulipotoka shule ilibidi twende kwenye vibarua kwa ajili ya chakula na madaftari, sabuni na matumizi mengine.

Nimepitia mateso makuu sana mpaka nimefika hapa nilipo kwa sababu ya baba yangu! Siku nyingine nitawaletea mkasa mzima ila kifupi namchukia mno baba yangu!
Najua baba yako haiwezi chukia 'manii' yake..!!
 
Kuna reality tv talk show, huyu mzee kamwita mwanae anamueleza sababu zilizofanya amtelekeze yeye na mama yake.
Alisema kipindi hicho alikuwa bado kijana mdogo, hana pesa wala hakuwa na kazi ndio maana aliamua kuondoka.
Kijana akamuuliza mzee, kwahiyo sasa hivi una pesa? Mzee akajibu hapana, ndio kijana akashangaa sasa umerudi umefuata nini?
 
Ulikuwa na wiki mbili ulijuaje kama kakimbia na mwanamke mwengine? Wazee miyeyisho wapo, ila nimejifunza kuwa makini sana tunapowatuhumu wazee wetu, wengi wamebeba siri nzito sana ambayo wakikuambia utajikana na utaishi maisha ya upweke sana.
Mpe dingi 👊 maisha yaendelee kwenye maisha kuna mambo mengi sana huenda dingi alipigwa msumari akawa hajitambui Bora hata wewe dingi bado yupo wengine wamekua wanakuja pata taarifa dingi alishaga kufa muda sana
 
Ulikuwa na wiki mbili ulijuaje kama kakimbia na mwanamke mwengine? Wazee miyeyisho wapo, ila nimejifunza kuwa makini sana tunapowatuhumu wazee wetu, wengi wamebeba siri nzito sana ambayo wakikuambia utajikana na utaishi maisha ya upweke sana.
.
 
Pole sana Mkuu dah kuna maumivu mengine ni ngumu sana kupona. Pambana wanao wasipitie hayo Mkuu na Mungu hatakuacha kisasi sio kizuri.
 
Ulitaka ukimchukia ndio atakufa.

Unamsamehe tu ila hapati kitu changu chochote........hii kubembelezana ni kulea ujinga.

Pesa zako unakula na mademu na pombe mimi za jasho langu uje kula bure tu? Huu ujinga mimi nilishaacha.

Sikufanyi kitu, wala sifatilii mambo yako ila changu cha jasho langu utakisikia kwenye redio. Maisha yanaendelea

Word.
 
Itapendeza zaidi kama ukijua aina ya ugomvi ndiyo useme haya maneno yako!!
Kwa wanangu sihitaji sababu ya kuwatelekeza. Mke sio ndugu ni raia tu tumekutana. Ila watoto aiseeee tutarara naye mbereee, mpaka nihakikishe wametoboa ndiyo nawaacha. Wala sihitaji malipo yao.
 
Au vipi? Walikuwa wanatutusha eti kuna laana😅😅

Mtu anaye mtelekeza mtoto asiyeweza kujisaidia ni muuaji na wewe mtelekeze hakuna cha laana wala baraka utapata toka kwake. Wabongo waache kujazana upumbavu endelevu tu na kutetea hawa kenge.
 
Unamchukia kwakuwa bado yupo.

Ila akifariki ndio utajutia uamuzi wako.

Tafuta muda utengeneze nae.

Hakuna mtu muhimu kama baba, ingawa feminist wanasema nani kama mama ila nakuambia ndugu yangu Baba ni habari nyingine.

Hata kama hana hela. Ila akisema neno tu linatosha kabisa.
 
Back
Top Bottom