Una urefu kiasi gani?
nimeamua kuanza kula mlo mmoja wa mchana tu huku jioni nikipitisha na maji tu.Breakfast nayo ni Mara moja moja.Lengo langu ni kufika 85kgs.
Kutokula haimaanishi kuwa ndio dawa ya kupunguza uzito wa mwili...
Mtu anaweza kuendelea kula kama kawaida na uzito wake ukapungua...
Hili linawezekana kama tu ukifuata kanuni sahihi ya ulaji mlo kamili pamoja na mazoezi ya kupunguza nishati ya ziada mwilini...
Jaribu kufuata utaratibu huu,
Asubuhi jitahidi upate matunda au juisi halisi ya matunda, wanga kidogo sana...
Mchana kula mlo kamili wenye wanga, hamirojo na vitamini...
Usiku kula chakula chenye hamirojo tu na vitamini, usilie wanga...
Zingatia kunywa maji na usiache mazoezi ya mwili angalau kwa siku mara moja...
Je nini hasara ya njia hii ya kupunguza mwili?
Utapata hasara za kiafya ambazo badala ya kupungua mwili utadhoofu mwili kwa kukosa virutubisho stahiki...
Unaweza ukaishia kupata vidonda vya tumbo na magonjwa mengine yasiyo ya kuambukiza...
Faida pia napenda kuzijua.
Hakuna faida ya kiafya...
Labda sana kama ni mbahili utasema una-save pesa...