Natumai double standard haitatumika
Scenario tofauti.
2021 kosa lilikua la wasimamizi wa ligi kwa lengo la kuwafurahisha watawala baada ya kupokea amri ili No.1 aweze kushuhudia mtanange.
Kolo siwapendi kutokana na kamdomo pamoja na utani wetu wa jadi kugeuzwa uadui wa jadi. Lakini kahuruma kamenijia ghafla Bora niushauri uongozi wa Simba.
Kwakua uongozi umeshawaharibu kisaikolojia wachezaji wao na kuwapandisha Mori wale wa upande wa pili, magoli 6 mpaka 10 hayaepukiki wakiamua kuingiza timu, wasipoingiza timu uwanjani kuteremshwa daraja kunawahusu, na Uto walivyo na usongo watahakikisha kanuni inatekelezwa.
Nini Cha kufanya kuepuka aibu hii?
Pelekeni timu uwanjani lakini si kwa nia ya kucheza Bali kuahirishwa mchezo.
Ujanja gani utumike?
Anzisheni washezaji kama 4 hivi ambao ni wakaa benchi, mechi ikianza hakikisheni wachezaji wote 11 wanalinda lango wasiruhusu uto kupata goli.
Halafu wale wachezaji wanaokaa benchi mara kwa mara wafanye makosa yatayosababisha red card. Wakitolewa wachezaji hao wote 4 kikanuni mchezo hauwezi kuendelea.
Hapo itabaki kanuni inaseje kuhusu mazungira hayo.
1.mchezo urudiwe
2.matokei yalio ishia ndio hayo hayo yatayotambulika
3. Uto atapewa ushindi wa mezani.
Yote kwa yote ni Bora kuliko kupigwa makono ya nyani mawili au kuteremshwa daraja.
Ni hayo tu kwa Leo.