Nakupenda lakini sikupi mwili wangu hadi unioe.

Nakupenda lakini sikupi mwili wangu hadi unioe.

Eti wadau tujuzane, hivi mambo kama haya bado yapo?

Nimempata mdada mmoja lakini anadai simvui hadi nimwoe, siku ya harusi ndo ataanza kutoa.

Kakiri kuwa yeye sio bikra lakini anadai hataki kufanya aliyofanya nyuma. Naona kama ananizingua vile. Wadau nahitaji ushauri wenu.

Nawasilisha!!!!!!!

Sasa wewe wasiwasi wako nini?Si usubiri kama unampenda kweli?
 
si umuoe sasa ujisevie...:sleepy::sleepy:

Testing Muhimu Neema, dunia hii ina mambo unaweza kuta hana kitu bali ni tundu tu la mkojo. Kuna jamaa yangu imeshawahi kumtokea.
 
Last edited by a moderator:
mito ma bro unaakili sana. Mimi bado namuuliza huyu mkaka hivi mwanamke ni kitu gani kwako? yaani hadi umvue ndipo uone raha? hivi kwanini msivumiliane hadi siku ya ndoa? binafsi sitaki kufunguka sana hapa manake utasema nime kukaripia.

nakuachia swali hili- hivi ingekuwa na kabinti kako ka pendwa sana mtu anataka akarushe maji halafu hajafunga naye ndoa akaja kukuambia wewe kama baba utamshaurije binti yako?

Hizo ni Theory tu mama. Sisi tunazungumzia maisha halisi. Hiyo dunia ya kusadikika imesha pita.
Mbaya zaidi wengi wao wanakunyima wewe halafu kwa wengine wanatoa, matokeo yake anaendeleza kutoa nje hata baada ya ndoa.

Wanaume TAFAKARI NA CHUKUA HATUA.
 
uskubali huo ujinga..

Wakina dada hawapendi kusikia hili. Nia ni njema kabisa nisije oa jitu limekubuhu kabisa.

"Test well before u decide". Kuna kijana mmoja mlokole alisubiri ndoa hivi hivi, Baada ya ndoa alijuta kukuta kitu very used times 100. Na kumbuka ndoa yake ni kifo kumtenganisha.
 
Well...madongo yakirushwa na wewe unarusha, au siyo Lily? Hali yako lakini? Umeadimika sana siku hizi wewe

U know...Tumeumbwa tofauti..sometimes dongo moja unaweza kaa nalo mwaka..hivo ni bora uyakwepe.
Mie ni mzima sana sema huwa tunapishana tu lakn nipo sana tu.
 
Na bado wanaume mtashangaa sana, wadada wamechoka kufunuliwa funuliwa hovyo, na hata ukisema unamuacha humuoi hilo sio big deal sana nowdays wengi tu hawana mpango wa kuolewa

Red: Muongozo wa spika: Sio kwamba hawana mpango bali wamekata tamaa, Ushindani ni mkubwa mno. Wengi nawaona kwa waganga na kwa wachungaji wakililia ndoa.
 
safi sana! Huyo dada anafaa sana msimamo wake unapendeza sana. Wadada wengine emu igeni msimamo wa mwenzenu, kwa nini mkubali kufanywa viwanja vya majaribio? Mwanaume yoyote atakaye anza kutembea na mwanamke kabla ya ndoa hawezi kuwamwaminifu hata ikiingia kwenye ndoa. Kama msichana ukikubali kumvulia nguo kila mwanaume anakuja kwa gia ya kuoa utazeeshwa na wale hutaolewa! Jiheshimuni wadada nyinyi wathamani jithaminini tutawathamani. namaliza kwakusema AZINIYE NA MWANAMKE HANA AKILI KABISA AFANYA JAMBO LA KUANGAMIZA NAFSI YAKE!!!

Usiwapotoshe wenzio. Majuto ni mjukuu.
 
Red: Muongozo wa spika: Sio kwamba hawana mpango bali wamekata tamaa, Ushindani ni mkubwa mno. Wengi nawaona kwa waganga na kwa wachungaji wakililia ndoa.

Utaratibu wa spika.....Mie nadhani wamekata tamaa sio kwa jili ya ushindani ila ni kwa kuwa there are very few 'Husband Material' in the market..Wengi ni matapeli,onja onja na hawana uhakika na wanachokitaka.
 
Utaratibu wa spika.....Mie nadhani wamekata tamaa sio kwa jili ya ushindani ila ni kwa kuwa there are very few 'Husband Material' in the market..Wengi ni matapeli,onja onja na hawana uhakika na wanachokitaka.

Hivi mtu akikuonja hasara ni kwako tu. Yeye haimuhusu. Mi ndio huwa nashangazwa na mabinti, Eti umenichezea!!!. Sema tumechezeana.
 
Back
Top Bottom