Wadau poleni kwa majukumu. Kuna picha mitandaoni inayomwonesha muimba nyimbo za Injili, Emmanuel Mbasha akiwa beach (nadhani), amevaa taulo tu huku sehemu ya boxer ikionekana.
Wachangiaji wamemshauri kwa hekima kwamba, angejisitiri vizuri maana yeye ni mtumishi wa Mungu (pengine kweli).
Lakini pia siku za nyuma, huyuhuyu Mbasha aliwahi kupost picha ya nyani (au sokwe) wakijamiiana!! Nayo ikazua balaa. Pia aliwahi kupost picha akiwa Zanzibar na binti yake (huku ikijulikana kwamba hakuwa na mkewe, walishaachana).
Sasa mimi najiuliza, Mbasha kama kweli ni mtumishi wa Mungu kwa nini hawi kioo?
Mambo anayoyafanya si kielelezo hata kidogo kwamba, kwa matendo yake mwingine anaweza kusema 'awe kama yeye.'
Ninavyojua Mimi, mtu anayejipambanua kuwa ni mtumishi wa Mungu anatakiwa awe kielelezo. Afanane tabia na uadilifu wa jamii yake. Huwezi mtaani kusema umeokoka au unamwimbia Bwana huku unaoneshewa kidole kwa matendo yako yenye kutia shaka.
Yesu walipomshutumu kwamba alikuwa kinyume na mafundisho ya uadilifu, aliwataka mafarisayo wataje kazi zake mbaya, mafarisayo wakashindwa kuzitaja (hazikuwepo).
Uadilifu wa Yesu uliingia mpaka kwa wanafunzi wake. Walimuiga kila kitu. Ndiyo maana Petro alipomfuata Yesu, kwa Kuhani Mkuu baada ya kukamatwa, watu waliomuona walimjua kuwa, alikuwa mwanafunzi wake, licha ya Petro kukataa.
Lakini wakasema 'hata kutembea kwake' kunafanana na Yesu, achilia mbali ongea yake. Mtu anayesema ameokoka anategemewa awe mfano mzuri kwa matendo yake ili watu waseme zamani alikuwa hivi, kabadilika, kweli wokovu upo (Kama jambazi anapoacha ujambazi wake).
Ndugu yangu Mbasha amekuwa kama ameokokea fasheni. Akumbuke zamani alikuwa Muislamu, akaenda ukristo. Kwa hiyo anatakiwa kusimama sawasawa bila kutia mbwembwe.
Nasema mbwembwe kwa sababu anayoyafanya huwezi kusema 'ni ubinadamu', bali anajiendekeza na kujipuuza, pia hajijali kwamba yeye ni nani!
Anasahau kwamba, kuwa mtumishi wa Mungu maana yake Mungu ndiyo bosi (mkuu), Sasa inakuaje mkuu awe mwema, lakini msaidizi wake ndiyo Mbasha? Mimi namshauri Mbasha kutafakari sawasawa, ayafanyayo hayana ubinadamu bali ni ushamba au kutotumia akili kuwaza sawasawa kabla ya kuamua kutenda.
Vyema kila mara kumwomba Mungu hekima kwani mwisho wa siku uzee utamfika na watu hawataweza kumpa cheo cha 'ana hekima' kwa sababu ya uzee kwani hata wajinga nao huzeeka!!
Kwa matendo yake ya mitandaoni, itafika nahali watu hawatakuwa na shaka na yeye, bali huyo mchungaji wake, kwamba anashindwa wapi kumnyoosha 'bwana mdogo' kama Mbasha?
Sent using Jamii Forums mobile app
Wachangiaji wamemshauri kwa hekima kwamba, angejisitiri vizuri maana yeye ni mtumishi wa Mungu (pengine kweli).
Lakini pia siku za nyuma, huyuhuyu Mbasha aliwahi kupost picha ya nyani (au sokwe) wakijamiiana!! Nayo ikazua balaa. Pia aliwahi kupost picha akiwa Zanzibar na binti yake (huku ikijulikana kwamba hakuwa na mkewe, walishaachana).
Sasa mimi najiuliza, Mbasha kama kweli ni mtumishi wa Mungu kwa nini hawi kioo?
Mambo anayoyafanya si kielelezo hata kidogo kwamba, kwa matendo yake mwingine anaweza kusema 'awe kama yeye.'
Ninavyojua Mimi, mtu anayejipambanua kuwa ni mtumishi wa Mungu anatakiwa awe kielelezo. Afanane tabia na uadilifu wa jamii yake. Huwezi mtaani kusema umeokoka au unamwimbia Bwana huku unaoneshewa kidole kwa matendo yako yenye kutia shaka.
Yesu walipomshutumu kwamba alikuwa kinyume na mafundisho ya uadilifu, aliwataka mafarisayo wataje kazi zake mbaya, mafarisayo wakashindwa kuzitaja (hazikuwepo).
Uadilifu wa Yesu uliingia mpaka kwa wanafunzi wake. Walimuiga kila kitu. Ndiyo maana Petro alipomfuata Yesu, kwa Kuhani Mkuu baada ya kukamatwa, watu waliomuona walimjua kuwa, alikuwa mwanafunzi wake, licha ya Petro kukataa.
Lakini wakasema 'hata kutembea kwake' kunafanana na Yesu, achilia mbali ongea yake. Mtu anayesema ameokoka anategemewa awe mfano mzuri kwa matendo yake ili watu waseme zamani alikuwa hivi, kabadilika, kweli wokovu upo (Kama jambazi anapoacha ujambazi wake).
Ndugu yangu Mbasha amekuwa kama ameokokea fasheni. Akumbuke zamani alikuwa Muislamu, akaenda ukristo. Kwa hiyo anatakiwa kusimama sawasawa bila kutia mbwembwe.
Nasema mbwembwe kwa sababu anayoyafanya huwezi kusema 'ni ubinadamu', bali anajiendekeza na kujipuuza, pia hajijali kwamba yeye ni nani!
Anasahau kwamba, kuwa mtumishi wa Mungu maana yake Mungu ndiyo bosi (mkuu), Sasa inakuaje mkuu awe mwema, lakini msaidizi wake ndiyo Mbasha? Mimi namshauri Mbasha kutafakari sawasawa, ayafanyayo hayana ubinadamu bali ni ushamba au kutotumia akili kuwaza sawasawa kabla ya kuamua kutenda.
Vyema kila mara kumwomba Mungu hekima kwani mwisho wa siku uzee utamfika na watu hawataweza kumpa cheo cha 'ana hekima' kwa sababu ya uzee kwani hata wajinga nao huzeeka!!
Kwa matendo yake ya mitandaoni, itafika nahali watu hawatakuwa na shaka na yeye, bali huyo mchungaji wake, kwamba anashindwa wapi kumnyoosha 'bwana mdogo' kama Mbasha?
Sent using Jamii Forums mobile app