Zanzibar 2020 Namba 8: Shamsi Vuai Nahodha achukua fomu ya kuwania Urais wa Zanzibar kupitia CCM

Zanzibar 2020 Namba 8: Shamsi Vuai Nahodha achukua fomu ya kuwania Urais wa Zanzibar kupitia CCM

Status
Not open for further replies.
Kwa sifa za awali hawa jamaa wote vichwa vimetulia,sijui labda waripuke mbele.but sina wasi wasi na kila mmoja wao.
 
Ni mpole sana ndo maana akaondolowa wizara ya Mambo ya ndani
Mchakato huu pia utasaidia kupata Makamu wa rais na mawaziri so usiwe na wasiwasi ni mchakato utakaota raking ya scores. Ili kurahisisha picking ya presidential candidate and so on
 
Awezi kumpiku mwinyi
Kama Kura zitakuwa huru bila shinikizo wala kubebwa wala kulazimishwa.
Basi Ndugu SHAMSI VUAI NAHODHA ndiye Raisi Stahiki wa Zanziba.
Ni Mzanzibari aliyeitumikia Zanzibar kwa kipindi kirefu, kwa vyeo mbalimbali, kwa uaminifu mkubwa na kwa Uzalendo uliotukuka.

Huyo Mwinyi ni kiongozi wa huku Bara na hana mchango mkubwa kwa Wananchi wa Visiwani Zanzibar.
Tuache dhana za kurithishana madaraka, Familia nyingine pia zina haki ya kuiongoza Zanzabar.
Karume na mwanaye wameitawala Zanzibar kwa miaka mingi.
Mwinyi, Mwanaye naye anataka aitawale Zanzibar.
Mwisho sasa tutawarithisha hadi Wajukuu.
Hebu tujifunze kuridhika na madaraka tuliyonayo.
Wengine nao wapewe nafasi.
Ni Swala la Busara tu.
 
Kama Kura zitakuwa huru bila shinikizo wala kubebwa wala kulazimishwa.
Basi Ndugu SHAMSI VUAI NAHODHA ndiye Raisi Stahiki wa Zanziba.
Ni Mzanzibari aliyeitumikia Zanzibar kwa kipindi kirefu, kwa vyeo mbalimbali, kwa uaminifu mkubwa na kwa Uzalendo uliotukuka.
mkuu huyo jamaa unamfahamu kiundani?
 
Kweli jamaa kama kazeeka au mpiga picha kamhujumu. Hivi ana miaka 65-70 au?
Hata 60 ajafika jamaa ana miaka 57 kazaliwa mwaka 1962
Kuna shida mahali.
Screenshot_2020-06-18-10-39-27-1-1.jpg
 
mkuu huyo jamaa unamfahamu kiundani?
Namfahamu sana, ni Mtu Mzalendo, Muadilifu na Mwenye tabasamu la Moyoni mda wote.
Yaani ni mtu Mwema.
Sio kwamba nampigia Debe ila naeleza Ukweli, yuko vizuri katika hadhi ya Uongozi wa juu na alishatumikia nafasi ya.
Waziri Mkuu wa Zanzibar ( wenyewe wana jina lao) na akafanya vizuri sana.
 
Waziri kiongozi mstaafu wa Zanzibar ambaye alihudumu kuanzia mwaka 2000 – 2010, Shamsi Vuai Nahodha amechukua fomu
Kastaafu miaka 10 iliyopita anarudi tena ulingoni.Jamani apumzike tu aachie wengine .Kupata hawezi kupata.Anyway ni haki yake kuchukua fomu
 
Namfahamu sana, ni Mtu Mzalendo, Muadilifu na Mwenye tabasamu la Moyoni mda wote.
Yaani ni mtu Mwema.
Sio kwamba nampigia Debe ila naeleza Ukweli, yuko vizuri katika hadhi ya Uongozi wa juu na alishatumikia nafasi ya.
Waziri Mkuu wa Zanzibar ( wenyewe wana jina lao) na akafanya vizuri sana.
Hafai huyo, atavunja muungano
 
Hafai huyo, atavunja muungano
Ha...ha....ha....
Kwanza kwa taarifa, huyo alipata Uwaziri Kiongozi akiwa Yanki tu.
Hajafikisha miaka 60.

Basi kwa taarifa huyo ni Muumini wa Muungano sana.
Katika watu walioipigania zanzibar kuiondoa katika Utawala wa Kimwinyi wa Kisultani basi ni Mzee Vuai. Someni Historia ya Mapinduzi.
Huyo ni Mwanawe na Amerithi Uzalendo toka kwa Baba yake.
Ni maisha tu huyo bado Dogo Sana.
 
Acha tu atest zari, ila Rais mstaafu Ally Hassan Mwinyi ameonyesha ukaribu sana na Rais wa sasa.

Ni kweli, na urais haupatikani kwa kupigiwa kura na wananchi, bali kwa ukaribu na rais wa wakati huo!
 
Ha...ha....ha....
Kwanza kwa taarifa, huyo alipata Uwaziri Kiongozi akiwa Yanki tu.
Hajafikisha miaka 60.

Basi kwa taarifa huyo ni Muumini wa Muungano sana.
Katika watu walioipigania zanzibar kuiondoa katika Utawala wa Kimwinyi wa Kisultani basi ni Mzee Vuai. Someni Historia ya Mapinduzi.
Huyo ni Mwanawe na Amerithi Uzalendo toka kwa Baba yake.
Ni maisha tu huyo bado Dogo Sana.

Alikuwa na maisha gani magumu mpaka awe hivyo? Hivi mtu akiwa above 50 Ni dogo, au mimi ndio sijui maana ya dogo? Sasa kama mtu yuko above 50 Ni dogo, akiwa na 20 si atakuwa bado anajisaidia kwenye poti?
 
Mkimuona Mbarawa au Mama Suluhu wamechukua fomu basi mjue baraka zimetoka kwa Jiwe a.k.a. Pogba a.k.a "yesu" na mmojawapo ndio mteule maana sauti ya Jiwe kutokea Chimwaga huwa inavuma mashariki mpaka magharibi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom