Namba zinanuka: Naunga mkono TANESCO ifumuliwe, na ikiwezekana ibinafsishwe kabisa, Makamba yupo sahihi 100000%. TANESCO ni janga

Cha msingi ,mtu aipate huduma ya umeme kwa bei rahisi.

Tz tunanunua unit moja kwa bei rahisi kuliko uganda.na kuunganishiwa umeme ni wastani wa 27,000.kwa hiyo ni bei nafuu kwa mtu wa kawaida.na hilo ndio lengo kuu la huduma za umma
Ni bei nafuu ila kwa kusubiria miezi 6 au zaidi huo muda una thamani kuliko hio elfu 27!
Siku tukijua kuthamini muda watanzania tutafanikiwa kuondoa umaskini japo kwa 50% toka tulipo sasa!
 
Gambino ni MWONGO. Katika mashirika ambayo hayakukaguliwa na CAG kwa mwaka 2019/20 ni pamoja na TANESCO. Swali hiyo faida unayoisema wewe imethibitishwa na nani?
 
Hata kwa macho ya kawaida yasiyohitaji kuumiza kichwa..TANESCO ya mwendazake IMEOZA.

JMakamba ana mzigo mzito sana, akijichanganya na Siasa kwenye hii reformations anayotegemea kuifanya amekwenda na Maji.
Duuu kwa hiyo sababu ya kuweka kuanzia 2016 ni kujustify mnachotaka kufanya na kuonyesha kwamba Magu alivurunda TANESCO,haya sawa
 
Gambino ni MWONGO. Katika mashirika ambayo hayakukaguliwa na CAG kwa mwaka 2019/20 ni pamoja na TANESCO. Swali hiyo faida unayoisema wewe imethibitishwa na nani?

Mkuu haikukaguliwa CAG hizi findings alizitoa wapi?

Kuna vitu havikukaguliwa lakini sio vyote, nilifuatilia huo mtanange hadi kwenye kamati za bunge kwa mashirika yale ambayo yalisemekana hayakukaguliwa.

Tuwe tunajitahidi kusoma kwanza, usipende tu kupewa summary.
 
Nimemnukuu Spika Job Ndugai alivyosema alipokuwa anahitimisha mkutano wa Bunge mwezi June.

Aidha wewe mwenyewe umekiri kuwa kuna baadhi ya vitu havikukaguliwa na CAG. Kwa hiyo hayo majedwali uliyoweka yatumie tu kama course work ya chuo. Ila siyo conclusive kwa kupimia utendaji wa Taasisi
 
Ndio maana serikali imeamua kuteua wajumbe wa bodi wanabiashara Ili kulisaidia shirika kujiendesha.

Na imesema haitaingilia mambo ya management na Kwa maana Hiyo serikali ilipe madeni yake.
Mkuu, hii ni ngumu aisee. Hakuna mwananchi wa kawaida atayeweza kulipa tsh 600 kwa unit moja ya umeme! Na Znz haitakubali kuanza kulipia umeme sasa, hii pia itafanya bei ya umeme ipande zaidi.

Biashara ni kuuza kwa faida. Ngeleja alifikiria kufanya hivyo kwa kuligawa shirika vipande vitatu, UZALISHAJI, USAFIRISHAJI na USAMBAZAJI, kwamba serikali ibakiwe na Usafirishaji tu. Hoja ikawa, Uzalishaji na Usafirishaji wataweza kufanya biashara ya faida, mzigo utabaki kwa huyu msambazaji ambaye ukiachilia mbali wezi wa umeme, ataweza kusubiri malipo ya serikali yamachuwe? Kwamba watumie leo wakulipe baada ya mwaka mmoja? Yeye atapaswa kununua umeme kwa cash kutoka kwa wazalishaji ambao kwa wakati huo sasa ni kina Dowans, Symbion, IPTL, Richmond, Aggreko n.k kisha alipie usafirishaji kwa serikali mwenye hiyo miundombinu, lakini kwakuwa anamdai serikali, atafidia hapo, hivyo kampuni ya Usafirishaji umeme ya serikali itakumbwa na ukata, ishindwe kuhudumia miundombinu, kisha nini kitatokea?

SA na Escom yao sasa hivi ni majanga, kisa ni miundombinu inakufa kwakuwa serikali haiwezi kuihudumia, jamaa wana mgao siku hizi.
 
Duuu kwa hiyo sababu ya kuweka kuanzia 2016 ni kujustify mnachotaka kufanya na kuonyesha kwamba Magu alivurunda TANESCO,haya sawa
Hapa wanafeli kwakweli, hata zile stori za maji kukauka ziliisha kipindi cha mwana, mimi mwananchi wa kawaida nimewahi kuishi miezi 3 mfululizo bila kuona katizo la umeme, hili ni jambo lililokuwa muujiza kwa miaka 55 ya uhuru.

Kama wafanyakazi wa Tanesco hawakuwa na furaha kipindi cha jiwe lakini umeme ukawa wa uhakika, basi waendelee tu kununa kwa manufaa ya nchi na huo ndio uzalendo.

Waulize wenye viwanda, tatizo la availability lilishaisha, lilibakia tatizo la quality. Ila sasa, tafuta mtu mmoja aliye kwenye magroup ya Tanesco akuambie jinsi malalamiko yalivyo mengi.
 
unajjua impact ya kubinfsisha shirika kama tanesco wewe? hapo ni sawa sawa kusema hospitali kubwa kama muhimbili ibinafsihwa. tanesco ikibinafsishwa lazima umeme utauzwa bei kubwa, oparation cost ya viwanda itaongezeka na definately products zitapanda bei. hapo cost of living itaongezeka na std of living ya wananchi itashuka. kubinafsisha tanesco ni hatari mno. ndio maana tuna mixed economy kind of economic system. acheni mihenko
 
Hata kwa macho ya kawaida yasiyohitaji kuumiza kichwa..TANESCO ya mwendazake IMEOZA.

JMakamba ana mzigo mzito sana, akijichanganya na Siasa kwenye hii reformations anayotegemea kuifanya amekwenda na Maji.
Kwani ya JK ilikuwaje, tuletee na hio bwashee!
 
1. Form za maombi ya kuunganishiwa umeme ziliondolewa tukashangilia

2. Service charge ziliondolewa tukashangilia.

3. Service line cost zilishushwa mpaka Tsh 320,900/= kwa single phase ndani ya mita 30 tukashangilia.

4. Service line cost zimeshushwa mpaka Tsh 27,000/= kwa wateja walio na umbali mpaka mita 120 tukashangilia.

5.Gharama za uzalishaji kila siku zinapanda

Kutokana na hayo hapo juu mnategemea TANESCO ifanye vizuri?

Tunapenda vitu cheap na ndio maana matatizo ni mengi.
 
Aliyependekeza JM apewe uwaziri wa nishati has done us a favour this was a ‘litmus test’ for him on his long term political ambitious.

Mtu yoyote mwenye uelewa wa kawaida tu wa biashara, without trying to be the ‘prophet of doom’ maamuzi yake ya awali tu ameshafail.

Matatizo ya TANESCO ukisoma statement yao na malalamiko ya wananchi kuna issue za engineering technicalities na capacity planning za project management; mfano kwenye statement niliyosoma mimi wameshachukua zaidi ya billioni 2 za kuwafungia watu umeme kazi ambayo aijafanyika hiyo ni loss of income tatizo ni nini? uzembe au limited resources ya kuongeza kasi. Solution yake unahitaji mtu mwenye skills za project management za infrastructure au engineer.

Then kuna issue ya kukatika umeme ideally you need an engineer with succession planning ambae ameshapewa managerial training along the way za kusimamia hilo tatizo a substitute is someone with energy management qualification.

Put it this way logic says huyo mtu ameshafeli kabla hata ajafungua mlango wa ofisi.

Muhimu zaidi lengo la Magufuli lilikuwa ni kuzalisha umeme at low unit cost karibu na nchi za west zineweza ivyo; sasa mtu kama Nehemia solution zake ni price hike.

Personal nimeshamfuta Makamba as a likely future presidential candidate, alikuwa na hiyo risk he is too unrealistic ambitious.

Watch this space hiyo team yake inaenda tengeneza matatizo zaidi TANESCO.
 
Lengo la Magufuli lilikuwa ni kutumia vyanzo vyenye unit cost nafuu or a mixture of different sources which reduces the average unit cost, kumpa unafuu mtanzania.

So msianze mambo ya NHC public housing kupanga rent za private landlords; muende waumiza watu wenye income ndogo with price hike ambazo awawezi zimudu kama ilivyotokea NHC chini ya Nehemia.
 
Kuna kitu kinaandaliwa kwa ustadi mkubwa sana, huoni puppets wa February wanazidi kujaa humu? Ngoja tusubiri
 
Sijapinga lengo la JPM ni zuri sana. Na kati ya kitu ambacho nilikubaliana na JPM ni hicho. Kabla hatujafikia huko hapa tuna survive vipi kila kitu kiende sawa. Taarifa zinasema mwaka jana TANESCO ilikusanya 1.8T na kilichotumika ni 1.8T maana yake hakuna faida. Sasa bei zimeshushwa za Service line tutarajie matumizi makubwa kuliko mapato maana yake ni hasara.
Tukumbuke vitu vizuri vyote ni gaharama.
 
Matumizi na mapato kulingana, ni either haukusanyi vizuri mapato au unatumia vibaya unachopata.
Kwa issue ya Tanesco ni kwamba hawakusanyi vizuri, ilipaswa wakusanye zaidi ya hiyo 1.8T. bado Hadi leo Kuna taasisi nyingi za serikali zinatumia umeme bure.
Fikiria tu Zanzibar umeme wao unatoka bara, Ila wanachokusanya kinabaki hukohuko.
Kuna mwaka jiwe alikuja na amri ya KATA, Yani kwa kila wanaodaiwa wakatiwe umeme. Uliibuka mgogoro mkubwa sana Kati ya Zanzibar na jiwe. Shein hakupenda Hilo suala.
Hivyo tulikosea tokea zamani, kutoka hapa tulipo sio kazi ndogo. Maana kuwaambia wote wanaodaiwa walipe na zile taasisi ambazo hazilipi umeme zianze kulipa sio kazi ndogo.
 
Umemjibu vizuri Sana

Kwanza Tanesco makusanyo wanakabidhi hazina..

Unakuja walaumu kwa lipi??
 

Kwenye viongozi wote wa Tanesco ambao ni mainjinia ukose mmoja wa kumpandisha awe CEO?!! Huu uteuzi mzima umebebwa na ile hoja ya mimi kama Waziri sitaki kupigiwa simu kuna nguzo imeanguka Kigamboni. Mfumo wa kidigitali kugundua fault ilipo ambao inawezekana Tanesco wataununua. Wala usishangae wakina maxmanini wakipewa tena kandarasi za kutuuzia LUKU.
 

Magufuli ni mtu aliekuwa akifanya informed decision nadhani alielewa sana standing costs za shirika bado zipo juu kushinda income.

Mipango yake ni ya muda mrefu shusha bei ya kuunganisha umeme, lower production costs na unganishia watu wengi zaidi eventually utakuwa on profit.

Na it was working, sasa kaangalie tena customer reserve capital watu wangapi washalipia deposit bado awajafungiwa umeme hiyo ni future revenue loss kwa sababu ya uzembe unaacha wateja wakati wewe una fixed costs; how are you gonna break even.
 


Wasomi wa JF kama wewe kichefu chefu Sana

Unalaumu management ya Tanesco as if walikuwa na power ya kufanya lolote

Chini ya Magufuli mapato yote walikuwa wanapeleka hazina na matumizi yeyote lazima waombe kibali..
Mara nyingi vibali hawapewi zaidi ya matumizi ya kawaida

Wasomi wa Jf kama wewe kichefu chefu sana
Tanesco chini ya Magufuli walikuwa wanakabidhi mapato yote serikalini na spending yeyote Ile tofauti na mishahara wanaomba kibali...

Hao waganda wanafanya kazi kwenye setu ya aina hii??..

Nina thread kama 3 humu nalalamikia centralisation ya Magufuli ilivyo haribu uchumi....

Dig deeper..
 

Nilifikiri ni mimi tu kuwa locked out hiyo j1 kumbe wako wengine. Ila kwa vile ni bure hapajF ilibidi kuwa mpole tu na najua hayuko wa kuzuia kusudi la Mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…