Namba zinanuka: Naunga mkono TANESCO ifumuliwe, na ikiwezekana ibinafsishwe kabisa, Makamba yupo sahihi 100000%. TANESCO ni janga

Takwimu za kupikwa hadi uchumi wa kati na world Bank ikathibitisha.

Umeme ulikatikakatika mara kwa mara tena ulikuwa na gharama za juu sana.

chuki ikizidi ni ugonjwa unaoweza kukusababishia kansa na hata kukutoa ktk reli ya kuuona ufalme wa milele.
jamaa wana chuki na jiwe noma waambie wana kera mno
 
Unapimaje hasara wakati kuna service imefanyika..., ni sawa sawa useme wewe sababu kila siku unakula basi ni hasara wakati kula kwako wewe ndio kunakufanya upate nguvu za kufanya kazi....

Hata Tanesco ikipata ruzuku kama umeme ni affordable na ni wa kiwango hio ni job well done..., kuunganisha watu wengi hata wakiunganishwa bure hio mwisho wa siku ni investment for future gains..., hao watu wataweza kulipia matumizi ambayo wasingeunganishwa wasingelipa...

Power generation itaongezeka kwa 2100mw baada ya Bwawa la Nyerere wakati sasa hivi peak ilikuwa 1600MW alafu wakati mambo yanataka kukaa sawa ndio tukaribishe watu waje kufaidi faida ambazo kila mwananchi amekuwa na anaendelea kuzigharamikia..., Dawa sio kuwapa wengine dawa ni kuongeza efficient kwa waliopo Au Private sectors watatoa wafanyakazi kutoka Mwezini au Mars na sio hawa hawa ambao sasa hivi tunasema ni wazembe ? (Give them Targets) na Tanesco wapewe meno ya kuwadai / kuwafungia wadaiwa sugu hata kama ni Serikali...
 
Umetumwa kupigia chapuo hoja za mafisadi wanaojidai tanesco haina performance ili wajiingize kuila au kukwapua. Ukiwaambie walinunue shirika watataka kuliiba maana thamani yake ni kubwa na wanajua hawawezi kuendesha shirika kama tanesco kwa faida. Assets kua nyingi sio sign ya poor performance hiyo ni kumisslead watu.
Kumefanyika na kunafanyika uwekezaji mkubwa kama mitambo ya gas na bwawa la nyerere na reli ya kutumia umeme itakua soko kwa tanesco. Wajanja they only want to water their bics katika mapato siku zijazo ya tanesco huku gharama zikibebwa na umma.
Mlaaniwe vibaka wa umma.
 
Mkuu huyo jamaa ni watu wanao andika uongo hizo takwimu zake sijui kazitoa wapi ili kujenga hoja yake ya kupandisha bei.

Apparently hizi siku mbili tatu TANESCO wame publish latest statement zao ya mwaka 2019-20 na previous year (may be kwa sababu watu hivi karibuni waligusia kutotoa latest data).

Ukiangalia trend ya faida kila mwaka since Magufuli amekuwa madarakani shirika likikuwa linapunguza kiwango cha hasara kila mwaka atimae mwaka ulioisha wametengeneza faida ya tsh 45 billion, baada ya kulipa kodi za serikali na commitment zao za madeni.

Hiyo ni mara kwanza Tanzania sijui baada ya miaka mingapi kama sio tangia uhuru.

So strategy ya TANESCO was working pamoja na uzembe wa kuacha fursa za wateja.


Report yote ya mwaka jana hiyo hapo na uwezi kusema ni data za kupikwa kwa sababu mkaguzi wa nje ni ‘Earnest & Young’ ndio alie verify hesabu zao.
 
If you want to kill a Dog give it a Bad name....

Hapa tunatayarishwa kuna kitu kinakuja....
 
Shida iliyopo inawezekana atayekuja atakuwa zaidi ya huyo, baada ya mwaka akamiliki ndege kabisa.
 
Shirika au taasisi inapimwa ufanisi wake kwa kuangalia vitu/ mambo mengi kabla ya kuhitimisha kuwa haifanyi vizuri.
Mashrika mengi huwa wanatoa taarifa za kila miezi3 au mwaka zinazozungumzia mtizamo wa menejimenti-,Mizania(Balance Sheet), Taarifa ya Mapato(Income Statement), Taarifa ya mtiririko wa fedha(Cashflow statement),Majedwali yanayoambatana na taarifa na taarifa ya Mkaguzi.
Ni kweli namba zinaweza kudanganya,lakini zitadanganya kidogo kuliko menejimenti.
Kuna mbinu mbalimbali za kuchambua ufanisi wa Shirika.
(1).vertical analysis-unalinganisha financial statement za Shirika kipindi cha mwaka mmoja na miaka mingine au Shirika moja na Mashirika mengine kwa kipindi kirefu.unapolinganisha items za kwenye Mizania,jumla kuu ya rasilimali (total assets) huwa ndiyo base(100), na unapolinganisha items za kwenye taarifa ya Mapato (Income Statement) mauzo huwa ndiyo base(100).
(2). Horizontal analysis-huangalia asilimia ya badiliko kwenye line items za kwenye Mizania au income statement kutoka kipindi kimoja na mingine, ongezeko/badiliko unagawa kwa mwaka uliotangulia.
(3).Ratio analysis-unaangalia ufanisi wa Shirika ukilinganisha na viwango vilivyowekwa na sekta husika,na hapa unaweza kuangalia ukwasi(Liquidity ratios), efficiency (Assets Management) ratios -huangalia ni jinsi gani Shirika Linatumia rasilimali (how the firm manage resources (assets) efficiently and effectively in generating revenue or earnings etc)
(4).Trend Analysis-huangalia. Mwenendo/ufanisi wa Shirika kwa kipindi kirefu(actual values, ratios and other relationships)
(5). Cross-sectional analysis-ufanisi wa Shirika unalinganishwa na Mashitika mengine kwenye sekta moja.

Ushauri.
Ni vema tunapofanya utafiti/tathimini ya taasisi yoyote tupate taarifa za kutosha,ili kufikia hitimisho sahihi.
 
Hata kwa macho ya kawaida yasiyohitaji kuumiza kichwa..TANESCO ya mwendazake IMEOZA.

JMakamba ana mzigo mzito sana,
akijichanganya na Siasa kwenye hii reformations anayotegemea kuifanya amekwenda na Maji.

Nilitaka kuona point ila baadaye nimegundua kumbe umetumwa.

Ni yule mzee baba late Pombe ndiye anawaumiza kichwa yaani jinsi ya kumuondoa akilini mnashindwa ila mnatumia wrong data kumjengea hoja.

Hakika hataondoka akilini mwenu, labda vunjeni mikataba ya Nyerere Power Plant Dam, SGR, uzeni midege mnayosema inaleta hasara huku mnaongeza mengine, ondosheni elimu bure, vunja daraja la kigongo busisi na Salender, Ondoeni sheria ya makao makuu Dodoma, kesho mkavunje ule uzio pale Malelani, nk.

Baada ya hapo ndipo uanze hizo ngonjera ikiwepo na hilo ka Tanesco ambayo unasema inaboronga kwa sababu ya Magufuri!.
 
Hata kwa macho ya kawaida yasiyohitaji kuumiza kichwa..TANESCO ya mwendazake IMEOZA.

JMakamba ana mzigo mzito sana, akijichanganya na Siasa kwenye hii reformations anayotegemea kuifanya amekwenda na Maji.
Acha ushabiki maandazi.....una zivu ww
 
There can be SOME TRUTH in what you are saying and your ANALYSIS AND ANALYTICAL COMPARISON kati ya hayo mashirika ya Umma mawili, BUT SIKUBALIANI NA WEWE juu ya suala la kubinafsisha TANESCO yetu haijarishi iko kwenye hali gani ya kiutendaji na kifedha. NO ubinafsishaji wa TANESCO! Kufanya hivyo ni kukaribisha ufisadi na wizi wa rasilimali zetu ikiwa ni pamoja na KINYEREZI 1-4 na Bwawa la Mwalimu Nyerere la Umeme huko Rufiji (to mention a few strategic investments zinazomezewa mate na MAFISADI, wa nje na wa ndani). It is my hope kuwa HII SI AJENDA ya Waziri Mpya wa Nishati VIA YOU!
 
Nami naamini hawa siyo wenye hii ajenda, hawa WAMETUMWA TU kupima maji kwa miguu! Kw mantiki hiyo, nawaasa waangalie hayo maji wanayo ya testi kwa miguu, yasije yakawasomba!
 
Cha msingi ,mtu aipate huduma ya umeme kwa bei rahisi.

Tz tunanunua unit moja kwa bei rahisi kuliko uganda.na kuunganishiwa umeme ni wastani wa 27,000.kwa hiyo ni bei nafuu kwa mtu wa kawaida.na hilo ndio lengo kuu la huduma za umma
Safi sana, watu hawaangalii hicho, wanalinganisha vile wanavyo penda kuviona. Nimemsoma mdau mmoja hapo juu anailaumu Tanesco ya mwendazake kwamba ilioza??? Nimeshangaa sana; hivi unaweza kulinganisha availability ya umeme wa majumbani enzi za mwendazake na rais gani? Labda Nyerere; miaka yote tulikua na mgao unao zidi masaa 16, sasa hivi umeme unakatika na kurudi fasta. Ukitaka kujua hilo angalia biashara ya majenerata kwasasa linganisha na enzi za marais waliopita ikoje? Obvious kwasasa wafanyabiashara wa vifaa hivyo watakua wanalaumu cause hakuna biashara; kingine ni biashara ya power bank zile tulikua tunachajia simu, mbona ni kama imekufa, nani sasa hivi unamuona anatembea na power bank, mimi nina zaidi ya miaka 5 sijamuona mtu akiwa na simu plus power bank, kipindi cha nyuma ilikua kawaida tu, simu na power bank, maduka ya simu na yenyewe yalikua yanauza simu plus power bank, sasa hivi hiyo biashara ni kama IMEKUFA, kwanini? availability ya umeme ni kubwa; mwendazake alikua na mabaya yake mengi tu but kwa issues za UMEME tunaongea UNAFIKI, the guy was smart on this area, tusidanganye
 
Hata kwa macho ya kawaida yasiyohitaji kuumiza kichwa..TANESCO ya mwendazake IMEOZA.

JMakamba ana mzigo mzito sana, akijichanganya na Siasa kwenye hii reformations anayotegemea kuifanya amekwenda na Maji.
Hi habari nadhani ni wajinga tu ndio wanaweza kuiamini, unless mkuu either ulikua mtoto from Kikwete kurudi nyuma au ulikua nje ya nchi, vinginevyo basi wewe utakua na shahada 3 au PHD ya UONGO. Huwezi kulinganisha availability ya umeme kipindi cha mwendazake na rais yeyote Tanzania hi, labda Nyerere lakini hata Nyerere mwenyewe, ni nyumba ngapi zilikua na umeme? Mgao wa Umeme Tanzania umeanza mwanzoni mwa miaka ya 90, hasa mwaka 92, kila mwaka kumekua na mgao wa umeme ili hali kulikua na wilaya nyingi sana hazina umeme, mshkaji hadi anakufa, alibakiza vijiji vingapi (sio wilaya, vijiji) kua na umeme? Halafu umeme ulikua unawaka muda wote, ukikatika labda ni break down au kuna planned maintanance otherwise watu mnatumia vipaji nyenu vya kudanganya hata mambo ya JUZI tu
 
Wakubwa huwa wanapiga pesa ya umma kupitia TANESCO, mkuu wewe nyama nchi itafunwe vizuri
 
Well said kila mtu ana mabaya yake lakini dikteta kwenye umeme aliweza sn
 
NAPE ANASEMAJE? YEYE NDO HUWA ANGALAU ANAWEZA KUSEMA UKWELI NA ANAOUWEZO WA KUMWAMBIA UKWELI MAKAMBA
 
Nami naamini hawa siyo wenye hii ajenda, hawa WAMETUMWA TU kupima maji kwa miguu! Kw mantiki hiyo, nawaasa waangalie hayo maji wanayo ya tessti kwa miguu, yasije yakawasomba!
Wajinga sana hawa watu, ndiyo wale wanaoandikiwa article wanakuja kifua mbele, wakiulizwa maswali wanakimbilia kwa boss wao kupata jibu.
 
Aisee, yaani unamsikiliza Mgeni kutoka Galilaya!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…