Namna/njia sahihi za kutunza ini na figo yako.

nosimo

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2015
Posts
247
Reaction score
50
Habari za jumapili, natumai wale wakristo tumesali na wengine wanaendelea vyema na shughuli zao.
Madokta wa jf Nina kitu kinanisumbua sana, mama yangu ametangulia mbele ya haki kwa "renal failure" daktari alipoulizwa alidai ni kufeli/kushindwa kwa Figo na INI kufanya kazi, je ni njia zipi za kuishi ili kuepuka magonjwa haya?? NA JE YANARITHIWA??? MAANA MAMANGU MKUBWA NAYE AMEANZA MARA FIGO NA DADANGU AMENIPIGIA SIMU KUNIAMBIA KUNA DAWA AMEPEWA ZA FIGO ETI INAMUUMA. sasa naombeni mnifahamishe, shukrani.
 
Miongoni mwa layman methods za kutunza ini na figo zako ni hizi

:Figo ndio chujio kubwa hasa la damu,epuka kuirundika damu yako na kemikali kama vile madawa na synthetic food.Hapa nina maana hivi vitu hata kama unavitumia viwe ni kwa kiasi kidogo

:Kunywa maji mengi kuisaidia figo yako kuchuja damu kwa urahisi..Kama damu yako ni concentrated kazi inakuwa ngumu na inaweza pelekea figo kucease

:Epuka kutumia vyakula vitakavyoboost levels za Uric Acid kwenye damu(nyama nyekundu),,hii itakusaidia kuepuka mawe ya kwenye figo

:Hakikisha unamaintain pressure ya damu mwilini mwako..Epuka mafuta mengi..kunywa maji ya kutosha..Fanya mazoezi to avoid idle fats

:Epuka kunywa pombe kupita kiasi.Unaliweka ini lako kwenye hatari

Matatizo mengi huwa yanakuwa kwenye chain..Hili linasababisha lile..lile linasababisha lingine


Mimi sio daktari
 
Asante sana mkuu. Mungu akubariki.
 
Akina mzizi mkavu na wengine njooni huku mniondoe hofu juu ya hili.
 
Alafu dawa za ARV zinaweza sababisha shida ya FIGO??
 
Last edited by a moderator:
Madaktari wameenda wapi Leo!njooni plz
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…