Namna Watanzania wanavyotapeliwa na Waganga wa Kienyeji nchini Kongo

Namna Watanzania wanavyotapeliwa na Waganga wa Kienyeji nchini Kongo

Haya mambo yakuchokozwa na kutukanwa na baadhi ya members humu halafu mimi nikimjibu nakula BAN sidhani kama imekaa sawa.Haiwezekani mtu anatoka huko anakokujua yeye anaanza kuniporomoshea matusi mazito halafu nimuangalie tu!.

Bado sijafikia kiwango hicho cha Utakatifu,kama ni nginja acha iwe nginja.

Wengine hatujaumbwa kuwa watukanaji,mimi nipo kuwaburudisha na kuwaelimisha hadhira yangu na umma wa watanzania wengi wanaojitambua,sasa anatokea mtu anaanza kukuporomoshea matusi ya nguoni kisa tu alikuja Inbox akaomba jambo fulani ukamnyima,ukimjibu kidogo tu anapelekea na wewe kufungiwa,hii siyo sawa moderators,wengine mnatuonea bila sababu ya msingi.

Kama nyuzi zangu zinakupa kero na huzipendi kwanini usipite ukatazame nyuzi zinazokufurahisha?,Kila mtu hapa anasoma anachoona kwake kina manufaa na anachokipenda,kama unaona hutaki usumbufu una-Block au Una - Ignore unaendelea na mishe zako,waachieni watu wanaotaka kujifunza na kuburudika wasome nyuzi zangu.

Hadhira yangu kwa muda wa siku zisizopungua 5 imeshindwa kupata simulizi nzuri na yenye mafunzo kwasababu tu ya watu fulani wajinga ambao hawataki kuniheshimu na kuanza kuniporomoshea matusi mazito,mimi kuwajibu imekuwa nongwa,hili halikubaliki hata kidogo moderators!.

Kuna muda tunachokozwa na kupandishwa hasira na wajinga kadhaa humu JF,sasa ajabu ni kwamba,mtu anapokutukana mara ya kwanza unamripoti hakuna hatua anayochukuliwa,mara ya pili pia ni vivyo hivyo,akikutukana mara ya tatu uzalendo unakushinda unamjibu,ukisha mjibu tu hapo ndipo Moderators wanakuja kuwaadhibu,wanashindwa kumuadhibu toka awali ulipomripoti wao wanakuja kumuadhibu ulipomjibu ambapo wanawaadhibu wote wanashindwa kumuadhibu mtoa matusi au muanzilishi wa matusi,hili halikubariki na nitaendelea kulipigia kelele.

Nimewahi kutoa mapendekezo kwenye uzi wangu mmoja uko kwenye Jukwaa la COMPLAINTS, APPRECIATION AND ADVICE(TO JF) nikasema tuwekeeni Blocking Button yenye nguvu na siyo hiyo Ignore iliyopo sasa,kwasababu kama nikishaona mtu ananitukana nitampiga Block ili aende akawatukane wazazi wake huko kwasababu wao ndiyo walimfundisha ujinga huo.

Aisee nimesikitishwa sana kupigwa BAN kwakosa ambalo limesabishwa na moja ya wapumbavu hapa JF.Wengine tunakiuka taratibu kwasababu ya kuchokozwa na siyo kwamba taratibu hatuzijui!.


Mimi ni mwema na nitaendelea kuwa mwema ila nikitukanwa lazima nijibu mapigo,kama ni kufungiwa nitafungiwa sana na nipo tayari kwa hilo!.

NIMESHINDWA KUSIMULIA STORI KWA SABABU YA WAJINGA KADHAA HAPA JF,HILI HALIKUBALIKI HATA KIDOGO NA NAUMIA SANA.

Huu ni ujumbe wenu Moderators najua uzi huu mnaupitia.


Ni hayo tu.
UMUGHAKA mzee wa kuzugia nakushauri achana na watu aina hiyo alafu kwa level yako humu jamii forum inabidi mtu akiona Quote yako inabidi havijunie au wewe uoni hiyo thamani yako mkuu ?
 
Hii si s
SEHEMU YA TANO



Hali ilizidi kuwa mbaya sana kwasababu maji yaliendelea kujaa kwa wingi,Baada ya yule Ustadhi aliyekuwa akiendesha kile chombo kuona mambo yanazidi kwenda mlama,alijaribu kuwasiliana na watu wa nchi kavu kule bandari ya Kirando kuona kama tutapata msaada,Mungu alisaidia mpaka wakati huo mawasiliano kwa hiyo sehemu ya katikati ya ziwa yenye mkondo mkali mawasiliano yalikuwa yakipatikana.

Alimpigia yule Seif usiku huo na bahati nzuri akapatikana,sasa ishu ikawa na kutufikia kwasababu tulikuwa mbali mno,sasa kumbe Seif alimwambia Ustadhi tuanze kutupa mizigo ziwani.

Utaratibu huwa ni kwamba,mnapopata matatizo ya msukosuko mkiwa ziwani huwa hakuna namna,mnaambiwa muanze kutupa mizigo kwenye maji,hapa huwa kuna imani za aina mbili.

1.Huamini mkitupa mizigo ziwani basi hali ya hewa itakuwa shwari.

2.Ni kupunguza uzito kwenye boti angalau kuweka uwiano sawa ili mpone.

Ustadhi "Anzeni kutupa mizigooooooo!"

Aliendelea "Tupeni mizigoooooo hiyoooo!"

Kila mtu aliyekuwa kwenye ile boti alianza kushika mzigo anaohumudu na kuurusha kwenye maji,mimi wakati huo kwakweli sikujua nifanyeje kwasababu hali yangu ilikuwa mbaya sana na nilidhani uenda siku hiyo ndiyo ilikuwa mwisho wa maisha yangu hapa duniani.Nilikuwa nawaza itakuwaje kwasababu niliondoka bila mtu yeyote kufahamu naenda wapi.

Pamoja na kutupa mizigo kwenye maji,bado hali ikazidi kuwa mbaya sana,Yule ustadhi niliona amechua boya akavaa akachukua na kamba akakamata dumu akaifunga kwenye dumu akawa tayari kwa lolote.

Wasaidizi wake nao nikaona kila mmoja amejiandaa kisaikolojia;Sisi ambao tulikuwa abiria kila mtu alikuwa akilia na kusali kivyake,wakati wenzangu kila mtu alikumbatia dumu lake,mimi kuna dumu lilikuwa na mafuta ambalo lilikuwa kando yangu,nikalichukua nikamwaga yale mafuta ziwani kisha nikafunga mfuniko nikaliweka chini ya miguu yangu.

Ustadhi na wasaidizi wake kumbe wao wote walikuwa wamejifunga kamba kiunoni kisha wakazifunga kwenye yale madumu, baadae nilipokuja kuuliza nikaambiwa madumu huwa yanakawaida ya kuponyoka mkononi ukiwa kwenye maji,hivyo ukifunga kama itakusaidia katika purukushani za mawimbi ya maji lisikimbie kwenda mbali ukafa maji.

Nakumbuka ilibidi nimuombe Mungu anisamehe dhambi zangu kwakuwa nilikuwa nimekosea sana.

Mimi "Eeeh Mungu nimekutenda dhambi,naomba unisamehe,Ikikupendeza nikalala mauti naomba unikumbuke katika ufalme wako utakaokuja"

Hayo ndiyo maombi nilimuomba Mungu wangu kwa wakati huo,kiukweli nilikuwa nimeshakata tamaa na nilijua sitoiona tena nchi kavu.

Sasa kumbe Seif aliwapigia simu kikosi cha uokoaji cha JWTZ ambao wapo jirani na Kirando kwenye mji wa Kipili,baada ya kikosi kazi cha Uokoaji cha JWTZ kupewa taarifa ile waliwasha Boti zao aina ya Fiber ambazo zinakimbia hatari,sasa kwakuwa Seif aliwaambia tupo Gezini jamaa waliondoka hadi Kirando kumchukua Seif waje nae maeneo ambayo tulikuwepo,walipofika Kirando Seif aliwapa mashine 2 za kuvuta maji kwenye boti kisha wao wakaondoka kutufuatilia tulipokuwa na Seif yeye akawasha boti yake akawa anakuja na watu wengine kwa ajili ya ukoaji.

Zile Boti za Jeshi zilifika eneo tulilokuwepo mida ya 8 usiku,walivyofika wakaanza kutuokoa kutoka kwenye ile Boti iliyokuwa inazama taratibu kwa kuzidiwa na maji,baada kuhakikisha watu wote tumeokolewa,walichukua zile mashine za kuvuta maji wakazihamishia kwenye ile boti kisha wanajeshi wengine wakabaki pale na ile fiber yao wakawa wanasaidia.Sisi tuliondolewa pale na kurudishwa hadi Kipili zilipo Kambi ya jeshi pamoja na kituo cha polisi.

Pamoja na zile Fiber kukimbia kwa spidi kali lakini tulitumia masaa 3 hadi kufika Kipili,kumbuka walifika kutuokoa ilikuwa saa 8 usiku,sasa kuondoka hapo Gezini hadi kufika Kipili ilikuwa saa 11 Afajiri.

Aisee sitokaa nisahau lile dhoruba na hata Wanajeshi walituambia Mungu alikuwa upande wetu siku hiyo kwasababu walidai huwa ni nadra kufika sehemu ya tukio wakakuta watu bado wapo hai,walisema ajali nyingi za hapo Gezini huwa wanafika kuokoa wanakuta watu walishakufa kitambo.

Bado hadi leo namshukuru Mungu sana kwasababu naamini bado anamakusudi na mimi,sema mimi ndiye muda mwingine najizima data na kuendelea kufanya maovu.

Baada ya kufika Bandarini nakumbuka simu zilipigwa sana siku hiyo kutoka kwa wakubwa,baada ya kuhesabiwa idadi yetu tulikabidhiwa kwa jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano wakitaka kufahamu ni kitu gani kilitokea.

Kamanda wa Jeshi "Poleni sana ndugu zetu,Mungu amewasaidia na mmenusurika,msiwe na hofu hapa ni sehemu salama na mtahudumiwa hadi pale mtakapopata usafiri mwingine au hadi dhoruba zitakapotulia"

Aliendelea "Sisi kama Jeshi lenu tumeshakamilisha kazi yetu,tunawakabidhi sasa kwa Jeshi la polisi nao waendelee na utaratibu wao,ila muwe na amani kabisa hapa mtaishi kama mpo kwenu vile"

Sasa kumbe kesho yake mkuu wa Mkoa alimwambia mkuu wa wilaya aje atuone na kutupatia Pole,kiukweli Polisi na Jeshi la wananchi(JWTZ) Kwa upande wa kule wanajali sana wananchi wa Tanzania kuliko nilivyokuwa nikidhani,nadhani ni kwasababu ya mipakani na mavurugu vurugu ya waasi wa Kongo.

Mtanzania upande ule wa Sumbawanga hadi Kigoma wanathaminiwa sana majeshi yao.


Basi,baada ya kuwa kila kitu kimekamilika,tulitafutiwa boti nyingine ambayo ilikuwa ikielekea Congo siku iliyokuwa ikifuatiwa na tukaombewa nafasi na kiongozi wa pale bandari ya kipili,boti ile ilikuwa inaelekea Congo sehemu moja inaitwa Fungo,sasa tukifika hapo kuna mizigo ishushwe kisha ndiyo turudishwe Moba.Ile safari kiukweli kutokea Kirando hadi Moba ilituchukua siku 5 kwasababu kadhaa wa kadhaa.

Sasa tukafanikiwa kufika Moba,tulipokamilisha taratibu zote za uhamiaji upande wa Congo tukaondoka zetu kuelekea mji mmoja ambao haukuwa mbali na hapo Moba unaitwa Kirungu.Sasa hapo Moba ni Jimbo au Mkoa na makao makuu yake ndiyo hapo Kirungu.

Naendelea...................
Hii simulizi ya Lwanda magere hii , Lwanda magere si ndio alienda hapo Congo Kirungu kusaka uchawi ?
 
SEHEMU YA SABA

Sauti ile ilikuwa kama ya mzee ambaye ilionyesha kabisa alikuwa amekabwa na kitu kooni,baada ya kuongea lugha na matashi yasioeleweka kwetu,ile sauti ilipokoma,mwanamke wa yule mtaalamu alikuja kutuita akasema jamaa anasema tuingie ndani.Tulipoingia kwenye chumba alichokuwepo huyo mtaalamu tulikuta chini kumetandikwa shuka jekundu na kumewashwa udi za kutosha,pia kulikuwa na chupa za bia za kutosha yaani unaweza sema kile chumba ilikuwa ni stoo ya kuhifadhia chupa za pombe.

Basi bhana tukafika tukaambiwa tukae chini ya lile shuka jekundu,sasa yule mtaalamu akachukua unga mweupe uliokuwa kama poda akaanza kutupaka usoni pamoja na mikononi,baada ya kutupaka akachukua kisosi cha udongo akaweka dawa moja iliyokuwa nyeusi kisha akaanza kusema.

Yeye "Mmekuya....naona mmekuya"

Aliendelea "Hapa mtapata mambo yenu ya kwende mzuri!"

Aliendelea "Naomba msiwe na hofu"

Kuna maneno mengine ambayo tulikuwa hatufahamu kamaanisha kitu gani,Jentre ndiye akawa anatutafsiria.Baada ya kupiga manyanga yake na kujiongelesha lugha tusizozifahamu,akaanza kutuambia mambo yafuatayo.

Yeye "Milimo ya bankoko elobaka boye,memela ngai deukshi litambala pona mwasi na ngai"

Yeye "Milimo ya bankoko elobaka boye,memela ngai troisi Khanga pona mwasi na ngai"

Jentre "Anasema,mizimu ya mababu imemwambia mumletee shuka mbili ya kujifunika kwa ajili ya mke wake"

Aliendelea "Pia anasema mizimu ya mababu zake imewataka mumletee vitenge pea tatu kwa ajili ya mke wake"

Yeye "Soki osali bongo,makambo ekozala malamu"

Jentre "Anasema,mkifanya hivyo walivyosena wazee mambo yenu yatakuwa mazuri!"

Kamugisha "Sawa sisi tumekuelewa,mimi nataka mambo yawe mazuri zaidi,Je tunaweza kumnunulia mke wake na vitu vingine kama zawadi?"

Mimi niliendelea kumtazama Kamugisha alivyokuwa na ujasiri wa kusema akamnunulie yule mke wa jamaa zawadi wakati hata mafanikio yenyewe hatujayaona.

Yeye " Nalingaka yo mingi mpe okozala na elonga mingi,bilimu bikosepela mpe mwasi na ngai mpe akosepela"

Jentre " Anasema,Wewe amekupenda sana na utafanikiwa sana,mizimu itafurahi na mke wake pia atafurahi"

Baada ya kuonekana tutakuwa watu wa mafanikio,alituambia usiku huo turudi tukapunzike halafu asubuhi hizo zawadi za mke wake zinunuliwe ili itakapofika jioni twende kuianza kazi ya kuyatafuta mafanikio yenyewe;Kwakuwa Kamugisha alikuwa amebaki kidogo na pesa za Kikongo tuliona siku iliyofuata tuondoke turudi pale Moba ili tukabadirishe angalau Dola 100 kwa ajili ya matumizi na mahitaji hayo.

Kabla ya kushuka Moba Kamugisha aliwasiliana na Jentre na kumueleza tulipokuwa tunaelekea na Jentre akamshauri hatuna haja ya kwenda huko kote na wakati hapohapo Kirungu kulikuwa kuna mtanzania aliyekuwa na duka la kuuza magodoro huwa anabadiri pesa,kwakuwa jamaa alisema ni mtanzania basi tukaona ni heri tukamuungishe mtanzania mwenzetu kuliko kushuka Moba.

Jentre alikuja akatupeleka hadi kwenye lile duka la mtanzania na bahati nzuri tulimkuta.

Kamugisha "Mambo vp kaka"

Mtanzania " Shwari ndugu zangu,nyie wabongo nini!"

Sisi "Eeeh!"

Mtanzania "Kiswahili tu namna tunavyoongea ndicho kinawatambulisha waswahili huku"

Aliendelea "Karibuni"

Kamugisha "Tulikuwa tunahitaji kubadili dollar 100 kaka"

Mtanzania "Hakuna tatizo karibuni sana"

Aliendelea "Mmekuja kuangalia fursa za kibiashara nini ndugu zangu!"

Kamugisha "Aaah hapana tumekuja kutembea tu na kubadili upepo!"

Mtanzania "Aaaah Kaka,haya bhana"

Aliendelea "Nilitaka kama mmekuja kuangalia fursa mnishirikishe nitawasaidia,mimi hapa ni mwenyeji huu ni mwaka wa 14 napambana hapa"

Kamugisha "Mazingira ya kibiashara yakoje hapa?"

Mtanzania "Ndugu zangu huku kuna hela ila sema tatizo haya makongomani yanapenda sana hela,kuna usumbufu mdogo mdogo kwa wapenda hela ila kuhusu hela hapa ipo,unajua bidhaa nyingi zinatoka Tanzania kwa njia ya maji kwasababu huku mabarabara hakuna"

Aliendelea "Hivyo kama ukiamua kuwekeza nyie njooni mpambane,pesa ipo!"

Kamugisha "Sawa kaka ila kwakuwa wewe ni mbongo mwenzetu sisi tulikuwa tumekuja kwa mtaalamu kwa ajili tu ya mambo yangu ya kazini"

Sasa jamaa alimwambia yule mtanzania japo kwa kumficha lakini alimueleza,mimi sikutaka kabisa jamaa amueleze mambo yetu na nilitaka iwe siri lakini jamaa akaamua kufunguka,japo hakumwambia kilichotupeleka ni kitu gani yeye alimwambia alienda kwa ajili ya mambo ya kazini kwake.

Mtanzania "Kuweni makini tu huku watanzania huwa wanajifanya wajuaji na wanatapeliwa sana"

Kamugisha "Kweli eeeh!"

Mtanzania "Siwadanganyi,nyie ni ndugu zangu ni lazima niwatahadharishe"

Aliendelea "Kwani mmefikia wapi?"

Kamugisha "Tulifikia Guest moja ipo kule chini ila kwasasa tunalala kwa ndugu yake mtaalamu"

Mtanzania "Wakati mnakuja nimewaona na jamaa mmoja mmeongozana nae,mnafahamiana nae?"

Kamugisha "Yes,jamaa tumekutana nae pale Kirando"

Mtanzania "Kwahiyo siku hizi yupo Kirando!"

Kamugisha "Unamfahamu mshikaji"

Mtanzania "Jamaa alikuwa fundi simu alipoona nadhani mambo hayaendi sawa akabadili upepo"

Kamugisha "Alikuwa fundi simu?,Mbona jamaa kwasasa ni mtaalamu na anafahamika sana pale Kirando!"

Mtanzania "Huyo muhuni tu,hana uganga wala bibi yake na uganga,huko Kirando anawaibia watu tu!"

Kamugisha "Kaka sema ukweli!"

Mtanzania "Mi siwatanii,jamaa alikuwa fundi simu,baada ya uongo uongo mwingi nadhani akaona ajifanye mganga ili awaibie watu na kama yuko huko Kirando basi huyo anawaibia sana watanzania!"

Aliendelea "Kama ndiyo huyo anayewafanyia kazi yenu basi mtatapeliwa ndugu zangu huyo dogo hana uganga wowote,Kwanza hapa Kirungu hakuna waganga wengi hapa ni matapeli na wanawatapeli sana watanzania"

Baada ya jamaa kutuambia vile nikakumbuka maneno niliyokuwa nikimwambia Kamugisha kuhusu yule mganga ila kwasababu alikuwa na kichwa kigumu nikabaki nisikilizie.

Kamugisha "Duuuh kaka mbona unanishitua!"

Mtanzania "Labda kawa mganga kweli lakini yule dogo ninavyomjua hana uganga wowote ni mganga njaa tu!"

Aliendelea "We unadhani kwanini hajataka kuwasubiri hapa!,ananijua ndiyo maana kaona asogee huko mbele!"

Kamugisha "Yeye ametuleta kwa mtaalamu mmoja ndiyo tunasubiri tiba"

Mtanzania "Huyo mtaalamu amewaomba hela?"

Kamugisha "Yeah kuna hela tumempa!"

Mtanzania "Aisee mmnahela za kuchezea!"

Aliendelea "Ngoja kuna jamaa niwaitie alikuwa fundi mwenzie aje mmulize nisemacho,unajua watanzania huwa wandhani tunawazibia riziki"

Yule jamaa mtanzania alitoka akaelekea mahali ambapo alisema ndipo ilikuwa kibanda cha kutengenezea simu cha Jentre na hakikuwa mbali,jamaa alivyotoka tukawa tunamuangaza Jentre lakini hatukumuona,Kamugisha alichukua simu akampigia akasema ametoka kidogo hayuko mbali na kama tumemaliza tuseme ili aje atupeleke sokoni tukanunue mahitaji,Kamugisha alimwambia asubiri kidogo.

Sasa yule mtanzania haukupita muda akaja ameongozana na mshikaji yuleyule ambaye ndiye tuliamini ni mganga,jamaa baada ya kutuona alitaka kufa kwa presha!

Inaendelea ...................
 
SEHEMU YA SABA




Sauti ile ilikuwa kama ya mzee ambaye ilionyesha kabisa alikuwa amekabwa na kitu kooni,baada ya kuongea lugha na matashi yasioeleweka kwetu,ile sauti ilipokoma,mwanamke wa yule mtaalamu alikuja kutuita akasema jamaa anasema tuingie ndani.Tulipoingia kwenye chumba alichokuwepo huyo mtaalamu tulikuta chini kumetandikwa shuka jekundu na kumewashwa udi za kutosha,pia kulikuwa na chupa za bia za kutosha yaani unaweza sema kile chumba ilikuwa ni stoo ya kuhifadhia chupa za pombe.

Basi bhana tukafika tukaambiwa tukae chini ya lile shuka jekundu,sasa yule mtaalamu akachukua unga mweupe uliokuwa kama poda akaanza kutupaka usoni pamoja na mikononi,baada ya kutupaka akachukua kisosi cha udongo akaweka dawa moja iliyokuwa nyeusi kisha akaanza kusema.

Yeye "Mmekuya....naona mmekuya"

Aliendelea "Hapa mtapata mambo yenu ya kwende mzuri!"

Aliendelea "Naomba msiwe na hofu"

Kuna maneno mengine ambayo tulikuwa hatufahamu kamaanisha kitu gani,Jentre ndiye akawa anatutafsiria.Baada ya kupiga manyanga yake na kujiongelesha lugha tusizozifahamu,akaanza kutuambia mambo yafuatayo.

Yeye "Milimo ya bankoko elobaka boye,memela ngai deukshi litambala pona mwasi na ngai"

Yeye "Milimo ya bankoko elobaka boye,memela ngai troisi Khanga pona mwasi na ngai"


Jentre "Anasema,mizimu ya mababu imemwambia mumletee shuka mbili ya kujifunika kwa ajili ya mke wake"

Aliendelea "Pia anasema mizimu ya mababu zake imewataka mumletee vitenge pea tatu kwa ajili ya mke wake"

Yeye "Soki osali bongo,makambo ekozala malamu"

Jentre "Anasema,mkifanya hivyo walivyosena wazee mambo yenu yatakuwa mazuri!"


Kamugisha "Sawa sisi tumekuelewa,mimi nataka mambo yawe mazuri zaidi,Je tunaweza kumnunulia mke wake na vitu vingine kama zawadi?"

Mimi niliendelea kumtazama Kamugisha alivyokuwa na ujasiri wa kusema akamnunulie yule mke wa jamaa zawadi wakati hata mafanikio yenyewe hatujayaona.

Yeye " Nalingaka yo mingi mpe okozala na elonga mingi,bilimu bikosepela mpe mwasi na ngai mpe akosepela"

Jentre " Anasema,Wewe amekupenda sana na utafanikiwa sana,mizimu itafurahi na mke wake pia atafurahi"


Baada ya kuonekana tutakuwa watu wa mafanikio,alituambia usiku huo turudi tukapunzike halafu asubuhi hizo zawadi za mke wake zinunuliwe ili itakapofika jioni twende kuianza kazi ya kuyatafuta mafanikio yenyewe;Kwakuwa Kamugisha alikuwa amebaki kidogo na pesa za Kikongo tuliona siku iliyofuata tuondoke turudi pale Moba ili tukabadirishe angalau Dola 100 kwa ajili ya matumizi na mahitaji hayo.

Kabla ya kushuka Moba Kamugisha aliwasiliana na Jentre na kumueleza tulipokuwa tunaelekea na Jentre akamshauri hatuna haja ya kwenda huko kote na wakati hapohapo Kirungu kulikuwa kuna mtanzania aliyekuwa na duka la kuuza magodoro huwa anabadiri pesa,kwakuwa jamaa alisema ni mtanzania basi tukaona ni heri tukamuungishe mtanzania mwenzetu kuliko kushuka Moba.

Jentre alikuja akatupeleka hadi kwenye lile duka la mtanzania na bahati nzuri tulimkuta.

Kamugisha "Mambo vp kaka"

Mtanzania " Shwari ndugu zangu,nyie wabongo nini!"

Sisi "Eeeh!"

Mtanzania "Kiswahili tu namna tunavyoongea ndicho kinawatambulisha waswahili huku"

Aliendelea "Karibuni"

Kamugisha "Tulikuwa tunahitaji kubadili dollar 100 kaka"

Mtanzania "Hakuna tatizo karibuni sana"

Aliendelea "Mmekuja kuangalia fursa za kibiashara nini ndugu zangu!"

Kamugisha "Aaah hapana tumekuja kutembea tu na kubadili upepo!"

Mtanzania "Aaaah Kaka,haya bhana"

Aliendelea "Nilitaka kama mmekuja kuangalia fursa mnishirikishe nitawasaidia,mimi hapa ni mwenyeji huu ni mwaka wa 14 napambana hapa"

Kamugisha "Mazingira ya kibiashara yakoje hapa?"

Mtanzania "Ndugu zangu huku kuna hela ila sema tatizo haya makongomani yanapenda sana hela,kuna usumbufu mdogo mdogo kwa wapenda hela ila kuhusu hela hapa ipo,unajua bidhaa nyingi zinatoka Tanzania kwa njia ya maji kwasababu huku mabarabara hakuna"

Aliendelea "Hivyo kama ukiamua kuwekeza nyie njooni mpambane,pesa ipo!"

Kamugisha "Sawa kaka ila kwakuwa wewe ni mbongo mwenzetu sisi tulikuwa tumekuja kwa mtaalamu kwa ajili tu ya mambo yangu ya kazini"

Sasa jamaa alimwambia yule mtanzania japo kwa kumficha lakini alimueleza,mimi sikutaka kabisa jamaa amueleze mambo yetu na nilitaka iwe siri lakini jamaa akaamua kufunguka,japo hakumwambia kilichotupeleka ni kitu gani yeye alimwambia alienda kwa ajili ya mambo ya kazini kwake.

Mtanzania "Kuweni makini tu huku watanzania huwa wanajifanya wajuaji na wanatapeliwa sana"

Kamugisha "Kweli eeeh!"

Mtanzania "Siwadanganyi,nyie ni ndugu zangu ni lazima niwatahadharishe"

Aliendelea "Kwani mmefikia wapi?"

Kamugisha "Tulifikia Guest moja ipo kule chini ila kwasasa tunalala kwa ndugu yake mtaalamu"

Mtanzania "Wakati mnakuja nimewaona na jamaa mmoja mmeongozana nae,mnafahamiana nae?"

Kamugisha "Yes,jamaa tumekutana nae pale Kirando"

Mtanzania "Kwahiyo siku hizi yupo Kirando!"

Kamugisha "Unamfahamu mshikaji"

Mtanzania "Jamaa alikuwa fundi simu alipoona nadhani mambo hayaendi sawa akabadili upepo"

Kamugisha "Alikuwa fundi simu?,Mbona jamaa kwasasa ni mtaalamu na anafahamika sana pale Kirando!"

Mtanzania "Huyo muhuni tu,hana uganga wala bibi yake na uganga,huko Kirando anawaibia watu tu!"

Kamugisha "Kaka sema ukweli!"

Mtanzania "Mi siwatanii,jamaa alikuwa fundi simu,baada ya uongo uongo mwingi nadhani akaona ajifanye mganga ili awaibie watu na kama yuko huko Kirando basi huyo anawaibia sana watanzania!"

Aliendelea "Kama ndiyo huyo anayewafanyia kazi yenu basi mtatapeliwa ndugu zangu huyo dogo hana uganga wowote,Kwanza hapa Kirungu hakuna waganga wengi hapa ni matapeli na wanawatapeli sana watanzania"

Baada ya jamaa kutuambia vile nikakumbuka maneno niliyokuwa nikimwambia Kamugisha kuhusu yule mganga ila kwasababu alikuwa na kichwa kigumu nikabaki nisikilizie.

Kamugisha "Duuuh kaka mbona unanishitua!"

Mtanzania "Labda kawa mganga kweli lakini yule dogo ninavyomjua hana uganga wowote ni mganga njaa tu!"

Aliendelea "We unadhani kwanini hajataka kuwasubiri hapa!,ananijua ndiyo maana kaona asogee huko mbele!"

Kamugisha "Yeye ametuleta kwa mtaalamu mmoja ndiyo tunasubiri tiba"

Mtanzania "Huyo mtaalamu amewaomba hela?"

Kamugisha "Yeah kuna hela tumempa!"

Mtanzania "Aisee mmnahela za kuchezea"

Aliendelea "Ngoja kuna jamaa niwaitie alikuwa fundi mwenzie aje mmulize nisemacho,unajua watanzania huwa wandhani tunawazibia riziki"

Yule jamaa mtanzania alitoka akaelekea mahali ambapo alisema ndipo ilikuwa kibanda cha kutengenezea simu cha Jentre na hakikuwa mbali,jamaa alivyotoka tukawa tunamuangaza Jentre lakini hatukumuona,Kamugisha alichukua simu akampigia akasema ametoka kidogo hayuko mbali na kama tumemaliza tuseme ili aje atupeleke sokoni tukanunue mahitaji,Kamugisha alimwambia asubiri kidogo.

Sasa yule mtanzania haukupita muda akaja ameongozana na mshikaji yuleyule ambaye ndiye tuliamini ni mganga,jamaa baada ya kutuona alitaka kufa kwa presha!

Inaendelea ...................
Kufa kwa presha[emoji28][emoji16]
 
Back
Top Bottom