Namna Ya Kuimarisha Mapenzi Katika Urafiki Wa Kawaida

Namna Ya Kuimarisha Mapenzi Katika Urafiki Wa Kawaida

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20250131_173701_Google.jpg


Hapa nazungumzia kuimarisha mapenzi katika mahusiano ya kawaida au kwa namna nyingine mahusiano ambayo sio ya kimapenzi

Kwanza ni kuonyesha unavutiwa na mambo ya rafiki zako au watu ambao huwa mnakuwa pamoja,nikwambie kitu expert?

Hakuna watu ambao hawapendi kujua kwamba upo interested na mambo yao,mfano kuulizia familia zao zinaendeleaje,kama ni mtu ambaye alikwambia kuhusu jambo lake fulani basi ukamuuliza vipi biashara inaendeleaje au ufugaji unaendeleaje

Kwa kufanya hivyo unaonyesha unajali na kuwafanya wavutiwe na wewe na wakupende,kwahiyo onyesha kujali nao watakupenda pia

Jambo la pili,ni kuwa na uso wa bashasha mara ukutanapo na wapendwa wako,onyesha uso mkunjufu na kuonyesha umefurahi kuwaona,ongea nao kwa tabasamu,hakika watajisikia vizuri na kufurahi kampani yako,na utaimarisha mahusiano yenu

Jambo la tatu ni kujichanganya na watu,usiwe mtu wa peke yako peke yako tu,sometime unajichanganya na watu na kujenga urafiki na mazungumzo ya hapa na pale,ebu angalia watu ambao ni wacheshi na waongeaji huwa wanazoeleka mapema na kupendwa na watu

Ni hayo tu!
 
Back
Top Bottom